Joannah
JF-Expert Member
- May 8, 2020
- 18,404
- 42,489
Hapa kwetu nyumbani Tanzania ndio tunalala Sasa kupumzisha mwili, Huko UGHAIBUNI ndio mnaamka sijui? anyways nitajua vizuri nikifika hukohuko....
Basi bwana, leo weekend nikasema nipite kuhemea vitu huko masokoni na madukani, Basi Mambo ndio yalikuwa Ni hivi🔥🔥
Picha linaanza. Amita Bachani kafia kwenye maua.
Litre moja ya mafuta ya kupikia 6600
Mchele 2000@1kg
Unga wa mahindi 1600@1kg😳
Mkate 1500mdogo,mkubwa wake 3000
Tunda nyanya la kupikia 150 @1
Nyama 8000@1kg
Dagaa wa Bukoba 10000@1kg
Samaki Sato 10000@1kg
Mkononi Nina kijipesa kidunchu nilichopambana week mzima kwa jasho na damu, nikabaki nazungukazunguka humo madukani Kama mtalii kafika Zanzibar,
Nimeisikitia Sana nchi yangu nzuriii Tanzania , yenye MITO na mabonde mengi ya NAFAKA, imekumbwa na Nini nchi yangu? Ile Mito na bahari na maziwa hayazalishi Tena samaki? vipi kuhusu mabonde yetu hatuna Tena nafaka?
jamani mkate 1600tsh na wasivyo na huruma wamepunguza tuvipande tuwili, usiulize nimejuaje Mimi Ni mama najua!!
Jamani unga wa mahindi ndio 1600 kweli? au ndio wamechanganya na soya kidogo ndani yake? Hapana kwa kweli.
Jamani, ndugu zangu wa Tanzania haya mambo yanaanzaga hivi hivi , hatua thabiti zisipochukuliwa mapema tukifika mwakani miezi Kama hii Ndio tutajua hatujui.
Basi Mimi kama Mimi,nimeamua kwenda nchi za mbalii hukooo ughaibuni, watanzania wenzangu mnipokee jamani , hii nchi hii wabaki wenye mizinga ya nyuki. Niko hapa Nina hasira zangu nasearch search niende zangu nchi gani kwenye fursa. SIELEWIII🤯🤯🤯
NB: MY HEART IS BLEEDING FOR MY MAMALAND
Basi bwana, leo weekend nikasema nipite kuhemea vitu huko masokoni na madukani, Basi Mambo ndio yalikuwa Ni hivi🔥🔥
Picha linaanza. Amita Bachani kafia kwenye maua.
Litre moja ya mafuta ya kupikia 6600
Mchele 2000@1kg
Unga wa mahindi 1600@1kg😳
Mkate 1500mdogo,mkubwa wake 3000
Tunda nyanya la kupikia 150 @1
Nyama 8000@1kg
Dagaa wa Bukoba 10000@1kg
Samaki Sato 10000@1kg
Mkononi Nina kijipesa kidunchu nilichopambana week mzima kwa jasho na damu, nikabaki nazungukazunguka humo madukani Kama mtalii kafika Zanzibar,
Nimeisikitia Sana nchi yangu nzuriii Tanzania , yenye MITO na mabonde mengi ya NAFAKA, imekumbwa na Nini nchi yangu? Ile Mito na bahari na maziwa hayazalishi Tena samaki? vipi kuhusu mabonde yetu hatuna Tena nafaka?
jamani mkate 1600tsh na wasivyo na huruma wamepunguza tuvipande tuwili, usiulize nimejuaje Mimi Ni mama najua!!
Jamani unga wa mahindi ndio 1600 kweli? au ndio wamechanganya na soya kidogo ndani yake? Hapana kwa kweli.
Jamani, ndugu zangu wa Tanzania haya mambo yanaanzaga hivi hivi , hatua thabiti zisipochukuliwa mapema tukifika mwakani miezi Kama hii Ndio tutajua hatujui.
Basi Mimi kama Mimi,nimeamua kwenda nchi za mbalii hukooo ughaibuni, watanzania wenzangu mnipokee jamani , hii nchi hii wabaki wenye mizinga ya nyuki. Niko hapa Nina hasira zangu nasearch search niende zangu nchi gani kwenye fursa. SIELEWIII🤯🤯🤯
NB: MY HEART IS BLEEDING FOR MY MAMALAND