OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
Jumapili ijayo tutaenda kwenye vituo husika kupiga kura zetu,.Sote wana Arumeru tumesikiliza kampeni za vyama na wagombea na ninaamini tumeshafanya maamuzi.Kwa wale ambao bado hawajafanya maamuzi au wamefanya maamuzi mabaya wiki inayooanza kesho ndio fursa pekee iliyobaki.Fuatilia kampeni za lala salama na hakika mpe kura yako mgombea au chama kilichokujibu au kuwekea mkakati kero zifuatazo hapa meru!!
1.Uhaba wa Ardhi
2. Uhaba wa Maji
3. Elimu ( uhaba wa shule,kumbuka shule ya msingi usa river ilifutiwa matokea kwa sababu za kijinga sana)
4.Uhaba wa hospitali na vituo vya afya kwa meru yote
5. Barabara mbovu (kumbuka zilivopigwa greda wakati wa mvua na kutuongezea mateso kutokana na tope)
6. Ukosefu wa kituo cha mabasi hapa usa madukani
7. Hali mbaya ya soko la Usariver, Tengeru, kikatiti( wakati tunalipa ushuru)
Nakusihi sana usimchague aliyefanya yafuatayo
1. Bingwa wa kutukana, kukashifu wengine kusambaza nyaraka za kuchafuana
2. Bingwa wa kugawa kanga, vitenge, kofia, t-shirt pesa taslimu pombe na vyakula
3. Aliyekuwa chanzo cha fujo na vurugu kwenye kampeni
Jimbo la Arumeru mashariki lipo nyuma sana kimaendeleo ukizungumzia sekta zote,.Tunatakiwa wakati majimbo mengine wanatembea sisi tukimbie ilituwafikie,. tunahitaji kamanda mkakamavu wa kuongoza hizi mbio, Chagua mtu anayeyajua matatizo ya meru na amewahi kuyaisha na kupata adha yake, huyo atatusaidia lakini mtu ambaye hayjawahi kuishi meru, matatizo yetu anayasikia tu kwa watu hataweza kuongoza mbio hizi za kuyatatua,. Nawatakieni week njema ya lala salama, na hatimaye uchaguzi mzuri wa haki na huru,...
1.Uhaba wa Ardhi
2. Uhaba wa Maji
3. Elimu ( uhaba wa shule,kumbuka shule ya msingi usa river ilifutiwa matokea kwa sababu za kijinga sana)
4.Uhaba wa hospitali na vituo vya afya kwa meru yote
5. Barabara mbovu (kumbuka zilivopigwa greda wakati wa mvua na kutuongezea mateso kutokana na tope)
6. Ukosefu wa kituo cha mabasi hapa usa madukani
7. Hali mbaya ya soko la Usariver, Tengeru, kikatiti( wakati tunalipa ushuru)
Nakusihi sana usimchague aliyefanya yafuatayo
1. Bingwa wa kutukana, kukashifu wengine kusambaza nyaraka za kuchafuana
2. Bingwa wa kugawa kanga, vitenge, kofia, t-shirt pesa taslimu pombe na vyakula
3. Aliyekuwa chanzo cha fujo na vurugu kwenye kampeni
Jimbo la Arumeru mashariki lipo nyuma sana kimaendeleo ukizungumzia sekta zote,.Tunatakiwa wakati majimbo mengine wanatembea sisi tukimbie ilituwafikie,. tunahitaji kamanda mkakamavu wa kuongoza hizi mbio, Chagua mtu anayeyajua matatizo ya meru na amewahi kuyaisha na kupata adha yake, huyo atatusaidia lakini mtu ambaye hayjawahi kuishi meru, matatizo yetu anayasikia tu kwa watu hataweza kuongoza mbio hizi za kuyatatua,. Nawatakieni week njema ya lala salama, na hatimaye uchaguzi mzuri wa haki na huru,...