Website/Tovuti zinapata pesa kupitia MB zako? (Hapana!!)

Kuchwizzy

JF-Expert Member
Oct 1, 2019
1,072
2,306
5acd27b2146e712c008b4b21.jpg

Kuna hii kasumba ambayo watumiaji wengi wa Internet,haswa sisi wa Tanzania tunayo.Aidha tuna amini hivi au tumeshawahi kusikia kutoka kwa watu na sisi tukawaamini bila kutafiti
Na cha ajabu huwa na bishana na watu wengi sana kuhusu hili swali nikiwa najaribu kuwaelewesha

So baada ya kupitia baadhi ya nyuzi kadhaa humu Jukwaani nikaona pia kuna baadhi ya wana JF wengi tu pia tunaamini hivyo
Kuwa Tovuti au Applications kama Facebook,google,instagram,youtube,jamiiforums etc kwa kiasi fulani zinaingiza pesa kwa kutumia MB zetu

Au kwa namna fulani hivi zinabadili MB tunazozitumia kuwa Pesa

Ukweli ni kwamba,hakuna tovuti au App inayoingiza hata TSH 1 kupitia MB zako,
Tovuti au Apps karibia zote ni free,ikiwa na maana ya kuwa hakuna gharama yoyote utakayo itoa ku access hio tovuti
Kwanzia facebook,google,tiktok au tovuti na app yoyote unayoitumia

So swali litakalokuja kwako ni,kama hizi tovuti zote nazitumia bure,zenyewe zinaingiza vipi pesa?

Fun fact: Mark Zuckerberg mwanzilishi na mkurugenzi wa Facebook Inc anautajiri wa dola za kimarekani Billion 122.9,Larry mwanzilishi mwenza wa google ana utajiri
wa Billion 100.2 dola za kimarekani

Kivipi wanaingiza pesa wakati tovuti na App zao ni bure nitalijibu mwisho kwa maelezo mepesi zaidi,ila kina nani wananufaika kupitia MB zetu nalijibu hapa

Internet ina furahisha,wengi tunai-take for granted(tunaichukulia juu juu),lakini kuna organizations zinazofanya kazi usiku na machana kuhakikisha Internet ipo na inapatikana kwa
watu wote
Japo kuwa hakuna anayemiliki Internet,(waanzilishi wake walitupa for free) lakini organizations hizi kwa namna fulani inabidi zilipwe kwa kazi zinazofanya

Moja kati ya Organizations hizo ni ISP ( Internet Service Providers),
ISP kazi yake kubwa ni kukupa uwezo wa wewe kama mtu wa kawaida ambaye huna miundombinu yoyote inayotakiwa kukuunganisha wewe na Internet kupata internet
So ISP wanakupa access ya internet kupitia vifurushi,kama UNIT za LUKU zinazoisha kulingana na matumizi yako

Tofauti kwenye vifurushi vya internet,hatutumii UNIT kama kipimo,tunatumia Bit
Bit ni kiasi kidogo cha data/taarifa ambacho kinaweza kuhifadhiwa na Computer yako (Laptop,Desktop,Smartphone zote ni computer)
Taarifa inaweza kuwa chochote,kwanzia herefu,neno,maneno,picha,video,sauti,namba hata nukta pia inachukua kiasi cha bit kwenye computer

8 bits =1 Byte(B)
I Mega Byte(MB) = 1,000,000 Bytes(B)

Kwakua ISP(Mfano Halotel, Vodacom, Tigo etc) wana miundombinu inayohitaji gharama kui manage,ndipo tunapopaswa kuwalipa kwa kununua vifurushi vyao
ISP ndio wanufaika halisi wa MB zako

So ISP anapokupa 500 MB kwa mfano,maana yake unaweza kupakua/download taarifa zenye ukubwa wa bits billions 4,
Taarifa unazo pakua zikizidi hiko kiasi,ndio pale unapowaona Halotel wezi


Turudi kwenye swali letu la pili,tovuti na apps kama Facebook zinaingiza vipi pesa?
Sio pesa tu,Ma-Trillions ya pesa?

Kupitia Matangazo,tuseme wewe ni mpenzi wa viatu,pia ni mwanaume kwenye account yako ya Facebook au Instagram unapenda ku like content au picha zinazo husiana na viatu
Unaperuzi tovuti zinazohusiana na viatu,at the same time upo logged in Facebook

Katika huo mtiririko wote huo,Facebook wanataarifa muhimu kuhusu mapenzi yako kwa viatu

Kilometa kadhaa kutoka ulipo,kuna muuzaji wa viatu vya kiume,anataka wateja zaidi
So anaamua kutangaza bidhaa zake Facebook,Facebook wanachohitaji kutoka kwake ni aina ya bidhaa anazouza
Kazi ya kutangaza bidhaa zake anaiachia Facebook kwa kuilipa kiasi kadhaa cha pesa

Kwa kua Facebook tayari inawafahamu watumiaji wake kama wewe,inachofanya ni ku onyesha hio Post kwako,kama Sponsored Post
Kwa kua tayari una interest na viatu,kuna chance kubwa uta click hio post...na hapo Facebook ndio inapoingiza Cash


Kwa ushauri kuhusu Tech,Website,Apps, na digital marketing nicheki 0748333586

By the way unaweza vipi kuongea kwa kujiamini mbele ya hizo Camera bila ku sound kama Robot?
 
Kwa hiyo wewe ulikuwa hujui hili ndugu😳😳😳😳🤣🤣🤣🤣
Tafuta mada nyingine ya maana Ila hii labda wafaid form 4
 
Na wakina diamond wanaingizaje pesa kutoka YouTube fafanua tafadhali
Matangazo tu
Youtube wana advertisement program kama ya Facebook
kwa kutumia data nyingi walizo na wanazo kusanya kuhusu wewe wana uwezo wa kuku target wewe na matangazo ambayo wanahisi upo interested nayo

Hayo matangazo wanayaweka mwanzoni au katikati ya video ya YouTuber aliyekidhi vigezo vya monetization na kuamua ku monetize channel yake

uki click hizo ads Youtube wanamplipa Youtuber huyo kiasi kadhaa....

Youtube pia wanalipwa pesa na advertisers walioweka ads zao pale

Youtubers wenye subscriptions nyingi ndiyo wanao nufaika zaidi kama hawa wasanii
 
Upo sahihi kwa kiasi fulani, ila kusema hakuna website inayoingiza hela kwa mb si sahihi.

Website inaweza ingia mkataba na kampuni ya simu kikaekwa kifurushi maalum cha website husika.

Mfano kipindi cha nyuma kulikua na vifurushi vya Dstv vodacom na kwese pia waliwahi kuwa na vifurushi vyao, Airtel pia waliwahi ku test zali na kifurushi chao cha laki 2 cha Netflix.

Vifurushi vya namna hii ukijiunga Unapata bure service ya Kulipia, then Mtandao wa simu unawalipa kampuni husika, vinakuwa ghali lakini inakuwa tu rahisi kwa mtumiaji kulipia Mara moja na kuondoa headache za ku manage bundle.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom