[Wazo]: Namna ya vijana wa Kitanzania Kuwa Mabilionea

Seneta Wa Mtwiz

JF-Expert Member
Sep 23, 2013
3,601
4,087
WAKUU,

MIONGONI MWA VITU VYENYE TIJA NI KUOMBA USHAURI KWA JAMAA NA MARAFIKI
PINDI UPATAPO IDEA YENYE TIJA NA ENDELEVU.


Nadhani hakuna asiyejua kuwa kuna changamoto Kubwa sana ya ajira nchini,

Hii ni kwa vijana wengi sana bila kujali wana kiwango gani cha elimu.
____
Na huu sio wakati wa vijana kuingojea serikali pasi na Kutafuta mbinu m'badala itakayosaidia kuifikia Tanzania ya viwanda ndani ya muda mfupi sana.

Nadhani mtakubaliana nami kuwa baadhi ya nchi za Magharibi na Asia watu wamewekeza sana Kwenye michezo kiasi cha kuanzia Academy za kufundisha soka na michezo mingine mbalimbali.

Kwa mantiki hiyo basi,

Nime_develop wazo moja matata sana ambalo litanufaisha takribani asilimia kubwa ya vijana,
Na
kuongeza idadi ya vijana wa Kitanzania ambao ni mamilionea.

Kutokana na vijana wengi kujikita katika mchezo wa "kubeti" kwa wingi bila mafanikio
Na
Kuambulia mikeka iliyochanika,

Nime_plan Kutafuta wadau kadhaa wenye utayari ili tuanzishe chuo kitakachoitwa

"COLLEGE OF TECHNICAL BETTING"

ambapo tutafundisha mbinu mbalimbali za kubeti bila kuchana mkeka,

Pia mbinu ya kubeti kwa mia 5 na kuvuna laki 6.

Kwa hatua ya mwanzo tutaanza na
"Basic_Certificate" ya miezi 3,
na
"Advanced_Certificate" ya mwaka mmoja.

Hata hivyo baada ya intakes kadhaa tutaongeza
"Ordinary Diploma in Technical Betting"
na
"Advanced Diploma",

Zitazopelekea baada ya muda tuje na
"Bachelor of Science in Technical Betting"
kabla ya
"Master's" yake.

Hii itatoa ajira si tu kwa wahitimu wa kozi husika,
Bali Hata kwa wakufunzi wake.
____
Hivyo wakuu
hapa nilipo naplan kuiandaa syllabus ili ikiwezekana iambatane na barua ya maombi NACTE,
Kiwango cha ada kwa ngazi zote tutakipanga.

Ambapo Main_Campus natarajia iwe kule Mtwara,
Na constituent 1 itakuwa Dar au Pwani."

Ikumbukwe mafunzo yatakayotolewa chuo Hiki sio ya kubeti kwenye mpira tu,
Bali
Hadi kwenye uteuzi wa viongozi wa kada mbalimbali,
Kauli zitakazotolewa na wawakilishi wetu mjengoni,
Na mengineyo.

Pia kutakuwa na kozi maalumu za kupunguza na kutuliza hasira na machungu pindi ikitokea mkeka umechanika kwa bahati mbaya,
Ili kupunguza matukio ya memba wa kubeti kuwaza kujitundika!
________
KWA YEYOTE MWENYE NIA YA KUWA SHAREHOLDER TUWASILIANE FASTA,

KARIBUNI KWA MICHANGO NA MABORESHO YA HII IDEA WAKUU.

AHSANTENI!
 
Yeye atafundisha kubeti bila kukosa gud idea kuliko kulialia ajira
 
Bado kidogo uwe na akili... kuna business opportunity kubwa sana ya kuwa hata milionea milimita chache sana ya ulichoongea. Ila itaweza kukuchukua hata miaka kutambua naongea nini. Siwezi nikakisema hapa maana wazo lenyewe lipo kwenye mikakati yangu na nimekuwa nalifanyia kazi kwa mwaka mmoja na nusu sasa. Endelea kuwaza sana hiyo idea yako labda baada ya miaka 2 unaweza tambua nina maana gani endapo utakuwa kweli unafikiri nje nje nje ya box ya wazo ulilotoa. Good luck home boy... Ilibaki kidogo upate akili
 
Bado kidogo uwe na akili... kuna business opportunity kubwa sana ya kuwa hata milionea milimita chache sana ya ulichoongea. Ila itaweza kukuchukua hata miaka kutambua naongea nini. Siwezi nikakisema hapa maana wazo lenyewe lipo kwenye mikakati yangu na nimekuwa nalifanyia kazi kwa mwaka mmoja na nusu sasa. Endelea kuwaza sana hiyo idea yako labda baada ya miaka 2 unaweza tambua nina maana gani endapo utakuwa kweli unafikiri nje nje nje ya box ya wazo ulilotoa. Good luck home boy... Ilibaki kidogo upate akili
Miaka 2 imetimia
 
Back
Top Bottom