Wazo la Kuudhi: Hawa wangewafaa wakoloni!

Wazo la Kuudhi: Hawa wangewafaa wakoloni!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,240
Reaction score
44,484
Wazo la Kuudhi: Wapo makamanda wa Polisi (mfano Kamuhanda na Sabas) na Wakuu wa mikoa (mfano Mulungo) ambao kwa kweli wangekuwa wanapendwa sana na wakoloni! Wangeweza hata kupewa nishani kwa "utumishi uliotukuka". Nina uhakika maafisa waliomkamata Nyerere na kumfikisha Mahakamani kwa uchochezi mwaka 1958 walijiona wametumikia vyema "the Crown"...Historia ina tabia mbaya sana... ya kujirudia rudia!
 
MMM,
Nyerere pamaoja na kuwekwa kizuizini. Mwisho wa siku,alikuja kuwa Waziri mkuu wa Tanganyika na kisha kuwa Rais wake...
Yana Mwisho.
 
Mandela alikuwa gaidi na Waziri Mkuu aliyefariki Mage, aliona ANC na Mandela ni Magaidi, lakini historia inatuonesha kuwa mbaya wako atakupa majina yote mabaya kadri atakavyoweza lakini mwisho wake unajulikana. Anayecheka sana mwanzoni mara nyingi hulia sana mwishoni.
 
Ndio maana neno UKOMBOZI lipo ili neno hili litimie yaha lazima yatokee
peoles power
viva CHADEMA
 
Hahahahaa hawa dawa yao nio very simple, wakifa tusiende kuwazika
 
ogopa sana wananchi wanapoamua kusema baasi!
kwa utafiti wangu binafsi hakuna kiongozi asiyekuwa na matatizo ya kiakili.naomba msinihoji sana ni muendelezo tu wa mawazo na fikra za kuudhi
 
Achani haya mambo yatokee, mimi nadhani yanatokea kwa sababu maalumu, hiki ni kifo kwa ccm na kuendelea kukua na kuvuma kwa CHADEMA, maana pamoja na yote haya yanayotokea wananchi wanazidi kuwa wamoja na CHADEMA na kuicha CCM mdomo wazi.

Ukitaka kujua hilo tazama maamuzi ya naibu spika Ndugai, yaliyotiliwa mkazo/kubalikiwa na Anne Makinda (spika) na mtikio/hamasa wa/ya wananchi kwenye mikutano ya wabunge wa CHADEMA kote walikopita, nadhani CCM wenyewe wanajutia uamuzi walioufanya.

Haya maamuzi ya kukurupuka na kutafuta sifa za kijinga yatawagharimu daima, na mimi kwa upande wangu nawaombea waendelee kuyafanya ili kweli itimie ya kwamba majuto ni mjuu huja baada ya kisa.

Big up Mulongo na wenzako katika kuharakisha kifo cha mgojwa wenu CCM, ili tumzike mapema if possible kabla ya 2015.
 
Wazo la Kuudhi: Wapo makamanda wa Polisi (mfano Kamuhanda na Sabas) na Wakuu wa mikoa (mfano Mulungo) ambao kwa kweli wangekuwa wanapendwa sana na wakoloni! Wangeweza hata kupewa nishani kwa "utumishi uliotukuka". Nina uhakika maafisa waliomkamata Nyerere na kumfikisha Mahakamani kwa uchochezi mwaka 1958 walijiona wametumikia vyema "the Crown"...Historia ina tabia mbaya sana... ya kujirudia rudia!

MMM; nina credible sources zinazoniambia RPC wa Arusha analazimishwa kufanya asiyoyataka. Bahati mbaya amri za kijeshi huwa hazipingwi wala kujadiliwa - especially zinazotoka kwa "amiri jeshi mkuu" wa majeshi ya ulinzi na usalama. Ila all in all, arguent yako hapa ni sahihi.
 
Na kwakuwa Kikwete anatuongoza kikoloni koloni, hawa jamaa watarajie kupewa nishani ya utumishi uliotukuka
 
Wazo la Kuudhi: Wapo makamanda wa Polisi (mfano Kamuhanda na Sabas) na Wakuu wa mikoa (mfano Mulungo) ambao kwa kweli wangekuwa wanapendwa sana na wakoloni! Wangeweza hata kupewa nishani kwa "utumishi uliotukuka". Nina uhakika maafisa waliomkamata Nyerere na kumfikisha Mahakamani kwa uchochezi mwaka 1958 walijiona wametumikia vyema "the Crown"...Historia ina tabia mbaya sana... ya kujirudia rudia!

Umemsahau IGP Mwema. Yeye tayari ameshapewa nishani kwa uongozi wa kikoloni uliotukuka.
 
Wazo la Kuudhi: Wapo makamanda wa Polisi (mfano Kamuhanda na Sabas) na Wakuu wa mikoa (mfano Mulungo) ambao kwa kweli wangekuwa wanapendwa sana na wakoloni! Wangeweza hata kupewa nishani kwa "utumishi uliotukuka". Nina uhakika maafisa waliomkamata Nyerere na kumfikisha Mahakamani kwa uchochezi mwaka 1958 walijiona wametumikia vyema "the Crown"...Historia ina tabia mbaya sana... ya kujirudia rudia!

Mkuu pengine umetanguliza na angalizo la kuwa wazo lako ni la kuudhi , kwa kutambua ukweli kuwa liko misplaced.

It seems una wa appease wazee wa CDM baada ya kipindi cha kuwapa vidonge vyao, huwa nafuatilia sna makala zako.
It is interesting kwamba of late makala zako ni reactionary as opposed to being philosophical!

Getting back to the point, hivi ungependa Wakuu wa Mikoa kama wa DSM ambao ni poa tu , "wakiwaomba" wananchi kuhama kufanya biashara mitaani, na "kuwaomba" kwa kuwabembeleza wananchi kuhama mabondeni ili wasije kufa!

Kuna makala nyingi tu ulizoandika juu ya ineffectiveness ya watendaji wa serikali, even under orders!

I do hope unakumbuka villagisation ambapo hapakuwepo kubembelezana, wakati wa Mwalimu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom