Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Mawazo mengine yanaudhi kabisa; yanaumiza, yanachekesha, yanasikitisha na wakati mwingine yanatia huruma - vyote kwa wakati mmoja. Tulizoea sana mtu akipata uteuzi tunasema "kaula". Ukisikia mtu kateuliwa wako watu nyuma wanaanza kushangilia kuwa angalau "mtu wao" kaula kwamba, hivi vyeo vilikuwa na labda vimeendelea kuwa sehemu ya ulaji, siyo utumishi tena.
Niliwahi kuandika huko nyuma kuwa ukishaondoa wazo la "utumishi wa umma" utakuta watu wanaanza "ulaji bila umma". Tukio la jana na labda mengine mengi (kuna jamaa yule wa Morogoro nishamsahau) linatukumbusha tu kuwa kwanza "vyeo ni dhamana" na ukiitwa kwenye nafasi ya serikali (kwa ajira au uteuzi) unaitwa kulitumikia taifa lako.
Huitaji kumuogopa Rais, wala kutetemeka, huitaji kuwa na hofu - kama una uhakika wa weledi wako na uwezo wako. Na uende utumike vizuri, wakati wako ukifika mwisho unaondoka anakuja mwingine. Hakuna mwenye "kiti" chake pale.
Tukilikubali wazo hili, tukaliheshimu basi mtu akiteuliwa au akipata nafasi ni lazima apongezwe lakini pia akumbushwe kuwa ameitwa kutumikia, nchi na wananchi wake. Usifanye sherehe kabla hujaapa, usianze kuaga hadi kuku (kama yule bwana balozi fulani). Tuheshimu hivi vyeo na watu watatuheshimu.
Tusifanye kazi kwa vile tunamwogopa Rais; tufanye kazi kwa sababu tumeanimiwa na Rais, vinginevyo imani ya Rais inaulizwa maana hadi akuteue ujue amekuamini sasa kama wewe mwenyewe hujiamini akikutumbua ndio ameondoa hiyo imani.
Lakini sote tunajua Magufuli huwa anawainua tena hata aliowaangusha, Mwigulu? kama ni Mbunge fanya ubunge wako vizuri na jioneshe kuwa ilikuwa ni siku mbaya tu, huwezi jua.
Nje ya hapo.. tumikieni Watanzania, mjiamini, na kama hamjiamini kateeni hizi teuzi au toeni udhuru, si kuna jamaa mmoja huko nyuma alikataa uteuzi wa Rais ukatenguliwa hata kabla ya kuapishwa? Si lazima uvae hilo joho hata kama halikutoshi au wewe hulitoshiiiii.
Acheni kula, mtaliwa!
MMM
Niliwahi kuandika huko nyuma kuwa ukishaondoa wazo la "utumishi wa umma" utakuta watu wanaanza "ulaji bila umma". Tukio la jana na labda mengine mengi (kuna jamaa yule wa Morogoro nishamsahau) linatukumbusha tu kuwa kwanza "vyeo ni dhamana" na ukiitwa kwenye nafasi ya serikali (kwa ajira au uteuzi) unaitwa kulitumikia taifa lako.
Huitaji kumuogopa Rais, wala kutetemeka, huitaji kuwa na hofu - kama una uhakika wa weledi wako na uwezo wako. Na uende utumike vizuri, wakati wako ukifika mwisho unaondoka anakuja mwingine. Hakuna mwenye "kiti" chake pale.
Tukilikubali wazo hili, tukaliheshimu basi mtu akiteuliwa au akipata nafasi ni lazima apongezwe lakini pia akumbushwe kuwa ameitwa kutumikia, nchi na wananchi wake. Usifanye sherehe kabla hujaapa, usianze kuaga hadi kuku (kama yule bwana balozi fulani). Tuheshimu hivi vyeo na watu watatuheshimu.
Tusifanye kazi kwa vile tunamwogopa Rais; tufanye kazi kwa sababu tumeanimiwa na Rais, vinginevyo imani ya Rais inaulizwa maana hadi akuteue ujue amekuamini sasa kama wewe mwenyewe hujiamini akikutumbua ndio ameondoa hiyo imani.
Lakini sote tunajua Magufuli huwa anawainua tena hata aliowaangusha, Mwigulu? kama ni Mbunge fanya ubunge wako vizuri na jioneshe kuwa ilikuwa ni siku mbaya tu, huwezi jua.
Nje ya hapo.. tumikieni Watanzania, mjiamini, na kama hamjiamini kateeni hizi teuzi au toeni udhuru, si kuna jamaa mmoja huko nyuma alikataa uteuzi wa Rais ukatenguliwa hata kabla ya kuapishwa? Si lazima uvae hilo joho hata kama halikutoshi au wewe hulitoshiiiii.
Acheni kula, mtaliwa!
MMM