Waziri wa Sanaa na Michezo Palamagamba Kabudi kukutana na viongozi wa Simba, Yanga, TFF na Bodi ya Ligi Alhamisi

Waziri wa Sanaa na Michezo Palamagamba Kabudi kukutana na viongozi wa Simba, Yanga, TFF na Bodi ya Ligi Alhamisi

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
473
Reaction score
1,682
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Palamagamba Kabudi amepanga kukutana viongozi wa Shirikisho la Soka la nchini (TFF), Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania (TPLB) na Klabu ya Yanga ili kutatua mgogoro unaoendelea kuhusu kusogezwa mbele kwa mchezo wao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Jumatatu Machi 24, 2025, kikao hicho kitafanyika jijini Dar es Salaam, Alhamisi na maofisa kutoka Yanga, Simba, TFF na Bodi ya Ligi Kuu wamejulishwa na watahudhuria.

"Ni kweli tutakutana na Waziri Kabudi kuhusu masuala mbalimbali, ikiwemo kusogezwa mbele kwa mchezo wetu dhidi ya Simba. Tumepokea barua na tutahudhuria," alisema afisa mmoja wa Yanga aliyeomba kutotajwa kwa jina.

Ofisa mmoja kutoka bodi ya ligi pia alithibitisha kupokea kutoka sekalini kuhusu kikao hicho; "Tumefahamishwa kuhusu kikao hicho na tutahudhuria. Ajenda kuu ni mjadala unaoendelea kuhusu kusogezwa mbele kwa mchezo wa Yanga dhidi ya Simba," alisema ofisa huyo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa alithibitisha kikao hicho kitafanyika jijini Dar es Salaam kikiongozwa na Waziri Kabudi.

Source: Mwananchi
 
Ni upuuzi kuacha mambo mengi ya maana kwenda kushughulikia upuuzi!
Kwa ccm hata upuu!I ni mambo ya maana. Turejee kauli ya makala na barua ya msajili kwa chadema.
Ile tu kuwa mshabiki wa ccm tayar wewe ni mpuuzi. Siyo ajabu pakawa na maandamano ya kumpongeza AMOS MAKALA. Kwa kujua ebola inauzwa wapi?
 
Kikao cha kutafuta suluhu kimepangwa kufanyika alhamisi na Yanga has confirmed to participate the meeting.

Unajua Ubwela
Yanga watake mkutano upate live coverage kutoka AZAM TV ili wasiburuzwe kama wa andaaji wana nia ovuna Yanga.
Wanachama wa Yanga waone na kusikia majadiliano on the spot ili kusiwe na kisingizio oo tulitishwa na bla bla na vile vile WANANCHI wanataka wamuone live KARAI akivuta ule mdomo wake pale atakapo bananishwa na hoja zilizoenda shule.
Ikiwapendeza kama hii ya live coverage itashindikana, basi kwenye deligation yao wasisahau kwenda na wajumbe wa BODI ya udhamini angalau wawili kati ya watatu hawa..
1. Bibi yetu mama yetu mjane wa mzee KARUME(huyu wakimuona watatoa SHKAMOO KUBWA.Kama walikua na uovu uta evaporate.
2. Mzee George Mkuchika
3. Mwigilu Nchemba. Hawa hapatakua na mdogo au mkubwa kwenye mazungumzo. NO KUBURUZANA.
Watu muhimu wengine kwenye hiyo squad ni Mwanasheria, Haji S. Manara na mzee Magoma. Hawa ni watu very important ( sio wanyonge hawa kwe nye majadiliano ya kibishi bishi au kibabe babe).
 
Kwa ccm hata upuu!I ni mambo ya maana. Turejee kauli ya makala na barua ya msajili kwa chadema.
Ile tu kuwa mshabiki wa ccm tayar wewe ni mpuuzi. Siyo ajabu pakawa na maandamano ya kumpongeza AMOS MAKALA. Kwa kujua ebola inauzwa wapi?
Nendeni mkamuulize makala kwa kuwa mnapenda kudandia udaku watu wamejikita kwenye kuboresha daftari la mpiga kura!
 
Back
Top Bottom