Waziri wa nchi, ofisi ya Rais-Tamisemi anavunja sheria za nchi mchana kweupe

msovero

JF-Expert Member
Jun 30, 2019
839
1,472
Mawaziri wote kwenye viapo vyao huwa wanaapa kuhifadhi, kuitetea na kuilinda katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kiapo hicho ni sheria na hupaswa kufuatwa kwa mtu yeyote anayepewa dhamana ya uwaziri kwani anakuwa anafanya kazi kwa niaba ya Rais wa nchi.

Jambo la kushangaza badala ya kuilinda katiba, waziri wa Tamisemi mhe. Ummy mwalimu amekuwa kinara wa kuvunja katiba na sheria za nchi kwa matamko yake ambayo amekuwa akiyatoa.

Tamko la kwanza ni kuhusu kupiga marufuku uhamisho kwa walimu
kama tunavyofahamu 'uhamisho' ni haki ya msingi ya kila mtumishi na hakuna anayeweza kuzuia haki hii kwakuwa ipo kwa mujibu wa sheria.

Lakini katika hali isiyotarajiwa, waziri ummy amepiga marufuku walimu wa vijijini kuhamia mjini kwa madai kwamba bado kuna upungufu mkubwa wa walimu katika shule za vijijini.

Ofcourse anaweza kuwa sahihi na dhamira njema lakini suluhisho ni kuajiri walimu wapya na kuwapeleka vijijini kuondoa huo uhaba lakini sio kuzuia uhamisho kwa walimu kwa sababu ni haki yao ya msingi ambayo ipo kwa mujibu wa sheria.

Au kama kuajiri haiwezekani, waziri apeleke muswada bungeni ili itungwe sheria inayoweka zuio kwa walimu wa vijijini kuhamia mjini lakini kwa sasa sheria haimpi mamlaka ya kuzuia 'uhamisho' kwahivyo tunamwomba waziri azingatie sheria za nchi.

Kuhusu walimu kuajiriwa na tume ya walimu 'TSC' badala ya wizara
Waziri ummy ametamka kwamba sasa walimu wataajiriwa na tume ya utumishi wa walimu badala ya wizara

Kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma, tamko hili lina kinzana na sheria kwa sababu tume ya utumishi wa walimu ilianzishwa chini ya kifungu cha 15 cha sheria ya utumishi wa umma. Sheria namba 8 ya mwaka 2002 ambapo kinataja majukumu ya tume kuwa ni kusimamia masuala ya kinidhamu kwa walimu, kusimamia maadili ya walimu, kusajili walimu, kuwapandisha vyeo walimu nakadhalika lakini sio kuajiri walimu

Na kwenye kifungu hicho sheria imeweka wazi kwamba tume ya utumishi wa walimu sio mwajiri wa walimu bali ni mamlaka ya ajira ikiwa na maana kwamba tume ni idara inayotakiwa kusimamia ajira rasmi katika utumishi wa umma na sio kuajiri kwa sababu hilo ni jukumu la wizara.

Vifungu vyote vinavyo eleza haya na msingi wa kuundwa kwa tume ya walimu vyote vipo kwenye sheria za utumishi wa umma kwahiyo ni vyema waziri akavifanyia marejeo ili asiendelee kutoa matamko yanayo kinzana na sheria.
 
Mawaziri wote kwenye viapo vyao huwa wanaapa kuhifadhi, kuitetea na kuilinda katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kiapo hicho ni sheria na hupaswa kufuatwa kwa mtu yeyote anayepewa dhamana ya uwaziri kwani anakuwa anafanya kazi kwa niaba ya Rais wa nchi.

Jambo la kushangaza badala ya kuilinda katiba, waziri wa Tamisemi mhe. Ummy mwalimu amekuwa kinara wa kuvunja katiba na sheria za nchi kwa matamko yake ambayo amekuwa akiyatoa.

Tamko la kwanza ni kuhusu kupiga marufuku uhamisho kwa walimu

kama tunavyofahamu 'uhamisho' ni haki ya msingi ya kila mtumishi na hakuna anayeweza kuzuia haki hii kwakuwa ipo kwa mujibu wa sheria.

Lakini katika hali isiyotarajiwa, waziri ummy amepiga marufuku walimu wa vijijini kuhamia mjini kwa madai kwamba bado kuna upungufu mkubwa wa walimu katika shule za vijijini.

Ofcourse anaweza kuwa sahihi na dhamira njema lakini suluhisho ni kuajiri walimu wapya na kuwapeleka vijijini kuondoa huo uhaba lakini sio kuzuia uhamisho kwa walimu kwa sababu ni haki yao ya msingi ambayo ipo kwa mujibu wa sheria.

Au kama kuajiri haiwezekani, waziri apeleke muswada bungeni ili itungwe sheria inayoweka zuio kwa walimu wa vijijini kuhamia mjini lakini kwa sasa sheria haimpi mamlaka ya kuzuia 'uhamisho' kwahivyo tunamwomba waziri azingatie sheria za nchi.

Kuhusu walimu kuajiriwa na tume ya walimu 'TSC' badala ya wizara.

Waziri ummy ametamka kwamba sasa walimu wataajiriwa na tume ya utumishi wa walimu badala ya wizara

Kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma, tamko hili lina kinzana na sheria kwa sababu tume ya utumishi wa walimu ilianzishwa chini ya kifungu cha 15 cha sheria ya utumishi wa umma. Sheria namba 8 ya mwaka 2002 ambapo kinataja majukumu ya tume kuwa ni kusimamia masuala ya kinidhamu kwa walimu, kusimamia maadili ya walimu, kusajili walimu, kuwapandisha vyeo walimu nakadhalika lakini sio kuajiri walimu

Na kwenye kifungu hicho sheria imeweka wazi kwamba tume ya utumishi wa walimu sio mwajiri wa walimu bali ni mamlaka ya ajira ikiwa na maana kwamba tume ni idara inayotakiwa kusimamia ajira rasmi katika utumishi wa umma na sio kuajiri kwa sababu hilo ni jukumu la wizara.

Vifungu vyote vinavyo eleza haya na msingi wa kuundwa kwa tume ya walimu vyote vipo kwenye sheria za utumishi wa umma kwahiyo ni vyema waziri akavifanyia marejeo ili asiendelee kutoa matamko yanayo kinzana na sheria.
Mlizoea kujitengenezea fursa za uhamisho kwa kurundikana mjini na kukimbia vituo halali mlivyopangiwa hasa vijijini au miji iliyopoa sasa mnadhibitiwa unasema sheria inakiukwa?

Sheria zipo, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma zipo kwahiyo hakuna sehemu yoyote amekiuka ila inaonesha una 'inda' na waziri Ummy Mwalimu kwa sababu binafsi
 
walimu fungueni kesi ya kikatiba kupitia wawakilishi wenu.
Walimu wanaogopa kufungua kesi kwa kuhofia kufukuzwa kazi lakini mioyoni wanaumia kwa kunyimwa 'uhamisho' ambao ni haki yao kisheria ndio maana hata ufanisi wa ufundishaji mashuleni umepungua kwa sababu walimu wanatekeleza majukumu yao wakiwa na kinyongo moyoni
 
Kwa hiyo
Mlizoea kujitengenezea fursa za uhamisho kwa kurundikana mjini na kukimbia vituo halali mlivyopangiwa hasa vijijini au miji iliyopoa sasa mnadhibitiwa unasema sheria inakiukwa?

Sheria zipo, kanuni na miongozo ya utumishi wa umma zipo kwahiyo hakuna sehemu yoyote amekiuka ila inaonesha una 'inda' na waziri Ummy Mwalimu kwa sababu binafsi
mwalimu wa mjini yeye aishi mjini miaka yake yote ?
 
Labda umemtafsiri vibaya Mama wa watu ila yeye alichosisitiza ni kwamba hakuna ulazima wa kuhama kwa mwalimu ikiwa shule haijapata mwalimu mwingine mbadala yake na kuwaacha watoto wanakosa baadhi ya masomo mashuleni kwao. Kwa hiyo akawataka maafisa elimu ikiwa hamna sababu maalum ya kuhama basi hakuna ulazima wa kuhama kwa haraka hadi apatikane mwalimu wa kujaza hiyo nafasi iliyowazi.
 
Kwa hiyo

mwalimu wa mjini yeye aishi mjini miaka yake yote ?
Uhamisho uwiano ndio dira ya uhamishaji maarifa kwa usahihi. Tatizo likuja wimbi kubwa kwa mfano walimu wa kike huomba kuhamia shule za mijini kuwafuata wale wanaodai ni waume zao hivyo kusababisha shule ya mjini kuwa na walimu waliozidi kiwango wakati huko kijijini wanabaki chukulia wawili au watatu kwenye shule ya wanafunzi 600-1,200 kwa ulinganifu ni kuwatesa na kuwapa mzigo mzito walimu wanaobaki. Hakuna mtumishi wa serikali au umma aliyeajiriwa kufanya kazi pekee mjini au katika baadhi ya miji iliyochangamka hivyo kusababisha ombwe mahala fulani.
 
Hivi kwa nn mtu asiombe kazi directly kwenye kituo anachokipenda? itapubguza sana hizi stress za kuhamahama.

Watoto wa maskini wako tayar kupiga kazi kokote ila hawapati kazi na wanaopata wanahama aftera year tu.

Sio fair kabisa
 
Kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma, tamko hili lina kinzana na sheria kwa sababu tume ya utumishi wa walimu ilianzishwa chini ya kifungu cha 15 cha sheria ya utumishi wa umma. Sheria namba 8 ya mwaka 2002 ambapo kinataja majukumu ya tume kuwa ni kusimamia masuala ya kinidhamu kwa walimu, kusimamia maadili ya walimu, kusajili walimu, kuwapandisha vyeo walimu nakadhalika lakini sio kuajiri
Kuna mtu amesema mawaziri wanatengeneza mazingira ya kula bata, huu ni ushahidi
 
Hivi kwa nn mtu asiombe kazi directly kwenye kituo anachokipenda? itapubguza sana hizi stress za kuhamahama.

Watoto wa maskini wako tayar kupiga kazi kokote ila hawapati kazi na wanaopata wanahama aftera year tu.

Sio fair kabisa
Kwa sasa mfumo wa ajira unaruhusu watu kuomba kazi kwenye vituo wanavyo vipenda moja kwa moja lakini hata hivyo suala la uhamisho linachagizwa na mambo mengi ambayo yanafanya watu wahame mfano kuugua, kuuguliwa, matatizo ya kifamilia, na imani za kishirikina.

Kwahiyo hata kuomba kwenye kituo cha kazi directly bado sio mwarobaini wa tatizo. Atleast serikali iboreshe mazingira ya vijijini au kutoa motisha kwa walimu wanaopangiwa vijijini itasaidia kupunguza tatizo kwa kiasi fulani
 
Labda umemtafsiri vibaya Mama wa watu ila yeye alichosisitiza ni kwamba hakuna ulazima wa kuhama kwa mwalimu ikiwa shule haijapata mwalimu mwingine mbadala yake na kuwaacha watoto wanakosa baadhi ya masomo mashuleni kwao. Kwa hiyo akawataka maafisa elimu ikiwa hamna sababu maalum ya kuhama basi hakuna ulazima wa kuhama kwa haraka hadi apatikane mwalimu wa kujaza hiyo nafasi iliyowazi.
Mkuu kwanza unatakiwa utambue kuwa hakuna mwalimu anayehama bila sababu maalum ndio maana ikionekana huna sababu za msingi zinazokufanya uhame serikali inazuia uhamisho wako.

Halafu kusema mwalimu asihame hadi atakapopatikana mbadala wake bado ni mwendelezo wa ukandamizaji wa haki za kiutumishi za walimu kwa sababu hilo ni jukumu la serikali kuhakikisha inafanya replacement baada ya mwalimu kuhama
 
Hii wizara bado haijapata mawaziri. Rudisheni Jafo au Simbachawene. Hiki kinachofanyika sicho kabisa.
Hapana, jaffo aendelee kubaki muungano na mazingira, ummy arudishwe wizara ya afya, dorothy abakie na ubunge wake wa kuteuliwa, simbachawene abakie mambo ya ndani halafu mchengerwa ndio aje Tamisemi
 
Back
Top Bottom