Waziri wa Mkapa amshukia Kikwete ataka CCM imtose 2010

Ni matumaini yangu sauti kama hizi za kumtosa Kikwete ili asigombee tena 2010 zinaongezeka zaidi ndani ya CCM na pia nchini kote. Hakuna hata moja ambalo Kikwete alilolifanya tangu aingie madarakani linalostahili kumpa tena awamu nyingine.

Ni Rais muoga sana labda kutokana na yeye mwenyewe kuwa na madhambi yake au kuwa karibu mno na mafisadi ambao walimchangia mabilioni ya kampeni zake 2005 ili aibuke kama mgombea wa CCM.

Bado kuna muda wa kutosha tu wa kuongeza hizi kampeni dhidi ya Kikwete. Tanzania inahitaji Kiongozi shujaa asiyemuogopa yoyote yule, hajawekwa mifukoni mwa mafisadi na atakayekuwa tayari kufanya maamuzi mazito hasa katika kipindi hiki kigumu ambapo nchi imegubikwa na ufisadi na utendaji mbovu vya kutisha.

Kumrudisha tena Kikwete madarakani ni kuangalia zaidi maslahi ya Kikwete na mafisadi badala yale ya nchi na sidhani kabisa kumrudisha Kikwete itakuwa ni maslahi kwa CCM pia.
 
Mimi sadhani hapo kama kuna hoja ya wamefulia au anaesema hiyo kauli ni nani, cha muhimu ni kupima uzito wa hiyo kauli,

kama angeisema Zitto nadhani ndio ungejua kuwa ni kauli kuntu

Kauli haina uzito.Ni siasa za kuelekea uchaguzi mkuu tu.Nyerere foundation inajiingiza katika siasa hasa baada ya mtu wao Salim kufunikwa na Jk.
 
Hizi ni kauli nzito sana kutolewa hadharani na watu waheshimiwa na waliowahi kushika nyadhifa kubwa sana. Imenitia moyo kuona kwamba jinsi hapa JF tunavyoghadhabika na udhaifu wa JK hata makada wa chama chake yameshawakifu.

Inaonekana mwanzoni walikua wanaogopa raisi anaweza kuwashughulikia wakiropoka lakini taratibu wamegundua kuwa JK ni dhaifu kiasi kwamba hata ukimkejeli hadharani hana uwezo wa kukufanya kitu. Kazi kwake.

Kama watakua na ujasiri wa kuyasema haya ndani ya vikao vya ccm, basi usishangae JK akapata wakati mgumu sana kutetea kuteuliwa 2010.
 
2005 wanamtandao walimsurubu Fredrick Sumaye kwamba ni Mr. Zero! Sasa kibao kinageuzwa kwao. Waingereza usema "The chicken has come home to roost"
 
"Alisema hoja ya msingi ni mwenyekiti wa CCM ambaye pia ni rais kujiandaa kufanya maamuzi magumu kwani hiyo itamuweka katika nafasi nzuri, lakini vinginevyo ashauriwe mwakani apumzike kwa kuwa miaka mitano aliyoongoza inamtosha. "


Maumivu ya joto la uchaguzi wa 2010 linaanza pooole pole
 
Wamtose ASAP;

Sio tu kwa kushindwa kufanya maamuzi mazito, bali pia kwa kukosa mwelekeo na kutokujua majukumu yake.

Acha unafiki wewe,

Unadhani unamdaganya nani hapa kwa kujifanya unamtosa Kikwete wakati wewe ni mtandao bwana. Nyie ndio mnaharibu chama chetu.
 
Ni matumaini yangu sauti kama hizi za kumtosa Kikwete ili asigombee tena 2010 zinaongezeka zaidi ndani ya CCM na pia nchini kote. Hakuna hata moja ambalo Kikwete alilolifanya tangu aingie madarakani linalostahili kumpa tena awamu nyingine.

Mkuu BAK,
Umeongea vizuri sana.

Kama tunaipenda nchi yetu ukweli lazima tuuseme. Kikwete has to go.

Bahati mbaya, kama Kikwete ni wa kuondolewa madarakani, itabidi aondolewe na wana CCM wenzake maana nje ya CCM hakuna atakayemuweza licha ya ufisadi uliozunguka serikali yake.

Tuombe na kusisitiza hizi kelele za kumuondoa zizidi maana ndio njia pekee ya kuwafanya walio na uwezo ndani ya CCM kujitokeza kupambana naye.

Cha kushangaza ni kuwa magazeti yetu, ukiachilia Mwananchi, hawakuona hayo aliyosema Qares kuwa ni muhimu na maendeleo makubwa ya kisiasa nchini.

Magazeti yetu mko wapi? Onyesheni wazi ubweteka wa Kikwete ili wengine waweze kumvaa.

P'se, p'se, do it for the sake of our Nation.
 
Mkuu BAK,
Umeongea vizuri sana.

Kama tunaipenda nchi yetu ukweli lazima tuuseme. Kikwete has to go.

Bahati mbaya, kama Kikwete ni wa kuondolewa madarakani, itabidi aondolewe na wana CCM wenzake maana nje ya CCM hakuna atakayemuweza licha ya ufisadi uliozunguka serikali yake.

Tuombe na kusisitiza hizi kelele za kumuondoa zizidi maana ndio njia pekee ya kuwafanya walio na uwezo ndani ya CCM kujitokeza kupambana naye.

Cha kushangaza ni kuwa magazeti yetu, ukiachilia Mwananchi, hawakuona hayo aliyosema Qares kuwa ni muhimu na maendeleo makubwa ya kisiasa nchini.

Magazeti yetu mko wapi? Onyesheni wazi ubweteka wa Kikwete ili wengine waweze kumvaa.

P'se, p'se, do it for the sake of our Nation.

Bwa ha ha ha ha,

Wanamtandao bwana bado wanafikiri hii ni 2005. Sasa unajaribu kumdaganya nani hapa. Eti mnakaa kwenye vikao na kuamua kuwa leo spinning itakuwa ni kujionesha kuwa hata nyie hamtaki Kikwete aendelee na kisha mtaanza na kusema kuwa lakini tukimtoa Kikwete, nani atapewa nchi?

Kisha mnatoa macho makali kuwa, kwa vile hakuna mtu mwingine anayefaa kwa sasa (maana wengine wote mmeshawachafua) basi ngoja tu Kikwete amalizie miaka yake mitano.

Kadanganye watoto wa chekechea na sio wana JF lakini mkae mtambue kuwa mnatuharibia chama chetu cha wakulima na wafanyakazi.

Down with mtandao
 
Nakubaliana na wewe kabisa, huu ni wito kwa CCM ku-revolt dhidi ya kilaza JK.


Nani Kilaza?????

JK au Wana Mtandao ???? si ndio walio mweka JK agombee Uraisi!!

Si ndio hao wanamtandao wasio jua kujipanga kuliongoza Taifa walijua jinsi ya Kuingia IKULU ila Hawakujua jinsi ya kuliongoza Taifa na hawakujua ni nini wakakifanye IKULU.

Walimsaliti Dr. SAS 2005 Chimwaga sasa matokeo yake ndio haya mnayaona sasa. DR. SAS was right president for this Country. ila kwa majungu na fitina za wana CCM wengine walipotezea ingawa waliju anawafaaaa.


 
Kwa mtazamo wangu sasa hivi ndo wameanza kuguza kiini tete chenyewe, samani walikuwa wanapiga blabla tu kwamba raisi wetu anania njema na nchi hii. ni ukweli haupingiki kabisa kwamba matatizo yote yanayoikumba CCM, kikwete na mtandao wake ndo wanahuka nambari wani. CCM itawaondoaje? sisi hatujui, na elfu 2015 mwanamtandao mwingine Bernard Membe anaukwaa urais. Maumivu mbele ya maumivu
 
Bwa ha ha ha ha,

Wanamtandao bwana bado wanafikiri hii ni 2005. Sasa unajaribu kumdaganya nani hapa. Eti mnakaa kwenye vikao na kuamua kuwa leo spinning itakuwa ni kujionesha kuwa hata nyie hamtaki Kikwete aendelee na kisha mtaanza na kusema kuwa lakini tukimtoa Kikwete, nani atapewa nchi?

Kisha mnatoa macho makali kuwa, kwa vile hakuna mtu mwingine anayefaa kwa sasa (maana wengine wote mmeshawachafua) basi ngoja tu Kikwete amalizie miaka yake mitano.

Kadanganye watoto wa chekechea na sio wana JF lakini mkae mtambue kuwa mnatuharibia chama chetu cha wakulima na wafanyakazi.

Down with mtandao


Nakasirika sana ninapokutana na maoni ya aina hii. Hapa sio suala la wanamtandao wala kundi lolote. Tunazungumzia nchi na mustakabali wake. Nani anawajua hao wahuni wanaojiita wanamtandao? Hicho ni kikundi kidogo sana mbele ya umati wa Watanzania wanaozidi milioni 40 ambao wanaangalia nchi yao ikiteketezwa na wageni wanaouvaa uraia wa Tanzania na kuthubutu kutamba eti wameiweka serikali yetu mikononi. Tunahitaji radical change ili kuwang'oa madarakani watu wasio na faida kwa maendeleo ya nchi yetu. Ebo!
 
Hakuna jipya. Tulishayasema yote humu JF.Tatizo liko palepale; wote tunabweka tu, nani wakutuongoza tuchukue hatua zinazostahili? Wapi Kinjeketile wa kututia ujasiri kuwa risasi ni maji tu? Wapi shujaa kama Mirambo, wapi shujaa kama mkwawa?nk. Tunatishiwa nyau tunarudi nyuma, Mikataba ya sasa ni mibovu kuliko enzi za karl peters - wazee wetu walipigana kwa nguvu kuondoa mikataba hiyo, sisi tunaiingia tukijua ubaya wake, lakini hatuchukui hatua stahili!!
Tuache woga - mimi sudhani kama kwa sanduku la kura mabadiliko yatakuja maana kura zitaibiwa au tukizidhibiti, watajitanganzia ushindi kwa ubabe. Mbona wameshajaza askari kila mahali - angalia wakuu wa mikoa, wilaya nk.
 
Kwa mtazamo wangu sasa hivi ndo wameanza kuguza kiini tete chenyewe, samani walikuwa wanapiga blabla tu kwamba raisi wetu anania njema na nchi hii. ni ukweli haupingiki kabisa kwamba matatizo yote yanayoikumba CCM, kikwete na mtandao wake ndo wanahuka nambari wani. CCM itawaondoaje? sisi hatujui, na elfu 2015 mwanamtandao mwingine Bernard Membe anaukwaa urais. Maumivu mbele ya maumivu

Hahahahaha,

Mi nilisema kuhusu hii syndrome ya "rais wetu mzuri ila ana washauri wabovu"

Sasa naona vidingi vimechoka.
 
hawa wote walikuwa serikalini na mambo bado yalikuwa mabaya na rushwa ilikuwa kubwa,ni kwa sababu wamenyang'anywa tonge mdomoni sasa wanatapatapa,pia hawa walikuwa against kikwete na hata salim mwenyewe yuko against kikwete kwa namna moja au nyingine ni lazima watamponda kikwete,mbona wao walipokuwa madarakani walikuwa hawataki kukosolewa na wamefanya nini cha maana kwa watanzania?
 
..Mateo Qares namkubali kama mtu asiyekuwa na uoga kutetea lile analoliamini.

..alikuwepo hata kwenye lile kundi maarufu la G-55.

..wananchi wa Mbeya wanakumbuka kama mtu asiyependa majungu ktk kazi.
 
Binafsi naona maoni kama maoni sio mabaya. Jamii itaendelea kuwa katika hali ya hatari kama wahalifu wataendelea na umoja wao, sisi kama wananchi tunaomba wagombane ili kama ni genge la wezi watajane wenyewe polisi. Umoja wao ni hatari kwa jamii salama.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom