GE2025 Waziri wa Maji, Jumaa Aweso awaonya wakandarasi Mradi Miji 28 muda wa utekelezaji kutoongezwa

GE2025 Waziri wa Maji, Jumaa Aweso awaonya wakandarasi Mradi Miji 28 muda wa utekelezaji kutoongezwa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Waziri wa Maji, Jumaa Hamidu Aweso , Waziri wa Maji, Jumaa Hamidu Awesowote wanaoshiriki katika utekelezaji wa Mradi wa Maji kwa Miji 28, akisisitiza kuwa hakutakuwa na nafasi ya kuongezewa muda kwa wakandarasi watakaoshindwa kukamilisha kazi kwa wakati

Ametoa kauli hiyo jijini Dodoma wakati wa kikao na wakandarasi pamoja na washauri wa mradi huo, ambao katika baadhi ya maeneo umefikia hatua ya asilimia 60 ya utekelezaji. Hata hivyo, alionesha kutoridhishwa na kasi ndogo katika baadhi ya maeneo yaliyosalia nyuma

"Nimechoka kusikia hoja za kuomba muda wa nyongeza. Mara hii hatutajadili suala hilo. Tumekubaliana kazi imalizike kwa wakati na lazima hilo litekelezwe," alisema kwa msisitizo Waziri Aweso

Ametaja baadhi ya miji inayotakiwa kuwa imemaliza kazi kufikia Septemba hadi Oktoba 2025 kuwa ni Handeni, Korogwe, Muheza, Pangani, Kilwa Masoko, Manyoni na Geita, huku miji ya Ifakara, Njombe, Makambako, Sikonge, Kasulu na Mpanda ikipaswa kukamilika kufikia Desemba 2025

Aidha, Waziri Aweso alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza juhudi za kuimarisha huduma ya maji nchini, pamoja na kuishukuru Serikali ya India kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha katika kufanikisha mradi huu. Pia alitoa pongezi kwa jamii na mamlaka za serikali za mitaa kwa uvumilivu wao wakati mradi ukiendelea kutekelezwa

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mhandisi Mwajuma Waziri, alisisitiza kuwa ushirikiano wa karibu kati ya pande zote zinazohusika ni muhimu ili kuhakikisha kuwa utekelezaji wa mradi huu haukwami katika hatua yoyote

Mradi huu unalenga kuboresha huduma ya maji safi na salama kwa Watanzania zaidi ya milioni 6.9, kwa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa asilimia 5 maeneo ya mijini na asilimia 3 vijijini

Thamani ya mradi ni zaidi ya shilingi trilioni 1.58, ambapo miji 24 inatekelezwa kwa msaada wa kifedha kutoka Serikali ya India (Sh. trilioni 1.167), na miji mingine minne inatekelezwa kwa kutumia fedha za ndani zenye thamani ya Sh. bilioni 413

jumaa.png

Chanzo: ITV
 
Back
Top Bottom