Waziri wa Biashara, Innocent Bashungwa ahaha mahindi yafike DRC

Boniphace Kichonge

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
1,606
1,956
Picha

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa amesema endapo Zambia haitaondoa vikwazo visivyo vya kisheria vya kuzuia mahindi, yanayotoka nchini kwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(DRC) kupita katika nchi yao, nao watawawekea vikwazo hivyo wasipitishe mizigo yao kuelekea Rwanda.

Alisema hayo jana katika mkutano, ulioandaliwa na Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) wa kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na mifugo kwa maendeleo ya viwanda. Mkutano huo ulishirikisha mawaziri kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Biashara na Viwanda na wadau mbalimbali wa kilimo. Alisema ipo changamoto kwa mahindi kutoka Tanzania kwenda soko la DRC kupitia Zambia, kwani nchi hiyo imekuwa ikiweka vikwazo visivyo vya kisheria.

Alisema kutokana na hali hiyo, amewasiliana na waziri wa viwanda na biashara wa Zambia na kumwomba watumie njia za kidiplomasia ili kuondoa vizuizi hivyo. Alisema hilo linashangaza, kwa sababu Zambia ikipeleka bidhaa zake Rwanda hupitia Tanzania, ambapo wao hawajawekewa vikwazo hivyo.

“Kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki tumeiandikia serikali ya Zambia kuwa wanachokifanya sio sawa, kwani sisi na wao ni sehemu ya SADC (Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika) na tumekubaliana ndani ya SADC kuweka uwanja wa sawa soko la pamoja.

Kwa hiyo wanachokifanya hatua ya kwanza kuifanya ni kupitia majadiliano ya kidiplomasia, lakini wakiendelea kutokutoa kibali na sisi upande wetu tutazuia bidhaa zao zisipite nchini kwenda Zambia,” alisema.
 
NAWATAFUNA Mi sijaona ubabe hapo, maana kama hatua zimechukuliwa pamoja na kuiandikia barua wizara inayojihusisha na diplomasia huko Zambia, hakuna namna kama mizigo yetu wanaiwekea vikwazo isife tunakokutaka kwann nawao tusiwawekee watakapotaka kupitisha mizigo yao kwenda Rwanda?

USA alipandisha ushuru kwa bidhaa toka china na China akajibu hvo kwa bidhaa toka USA, USA alitishia kupandisha kodi kwa bidhaa za EU na wao walimsubiria apandishe nao wapandishe zake! No way out my brother wakijitia ngangali aheri nao wawekewe vikwazo tu.
 
Watanzania ni wanafiki kiwango cha SGR, hicho walichofanya serikali ya Zambia ingeanza kufanya serikali ya Tanzania basi watanzania wangeilaumu serikali yao kuwa haiina mahusiano mazuri na majiran zake, mara ooh huyu jiwe ye anaharibu kila kitu! Lakin ata hvo wameanza wao lakin tunailalamikia serikali yetu.
 
Jana watu walikurupuka hapa kumlaumu waziri bila kujua Nini tatizo na Wala hawakujua Nini sababu ilikuwa ni mwendo wa kukurupuka mara serikali mara ccm mpaka aibu leo kimya chadema wanakurupuka sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania ni wanafiki kiwango cha SGR, hicho walichofanya serikali ya Zambia ingeanza kufanya serikali ya Tanzania basi watanzania wangeilaumu serikali yao kuwa haiina mahusiano mazuri na majiran zake, mara ooh huyu jiwe ye anaharibu kila kitu! Lakin ata hvo wameanza wao lakin tunailalamikia serikali yetu.
Jana si uliona walivyokurupuka kuisema serikali Leo kimya chadema kwa kukurupuka hawajambo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom