Waziri Ummy Mwalimu kwa hili la Bima Ya Afya umeniangusha, machozi yananitoka

Countrywide

JF-Expert Member
Mar 2, 2015
18,200
27,248
Waziri Ummy hili la Bima ya Afya Umeniangusha sana, hapa nilipo nina masikitiko makubwa sana ya maelezo unayoyatoa na kinachoendelea.

Ni wazi kabisa tumeanza kukwama kwenye hili ya bima ya afya.

Waziri umesema watu ambao sio watumishi ndio pia wamechangia mfuko kuelemewa na kuufanya udhoofike. Kimsingi kabisa kila mtu anapaswa kuwa na bima ya afya, wengi wamejiunga na NHIF sababu gharama za kujiunga na kulipia kwa mwaka ni ndogo kulinganisha na bima zingine. Vipato vya watanzania vinajulikana.

Afya ndio uti wa mgongo wa taifa lolote, ambae hana elimu Iia ana afya njema ataweza kuzalisha, Ila ambae hana vyote atawezaje kuzalisha? Taifa litakua la aina gani?

Tabia ya wengi huwa hawapendi kwenda hospitali hata kama ana bima, ukimuona mtanzania anaenda sana hospitali basi kweli huyo mtu ana shida kubwa. Hivyo hakuna ambae anafanya makusudi kwenda mara kwa mara hospital.

Sasa hivi pamoja na yote hayo bado Kuna mamia ya watu ambao kila siku huku mitandaoni wanaomba msaada wa matibabu. Na wewe waziri umekua mmoja wa watu wanaochangia na kusaidia hawa watu huku mitandaoni. Vipi bima ikienda kupunguza na kuweka masharti magumu zaidi, Hali itakuaje?

Ni hadi lini tutaendelea kuchangishana mitandaoni kuwasaidia walioshindwa gharama za matibabu??

Waziri ninakuomba tuwekeze zaidi kwenye afya, tubane mwingine. Kama kifaa flani cha mil 10 kinanunuliwa kwa mil. 50, basi tubane kuanzia hapo. Bado naamini pesa ipo ni kuweka tu mipango vizuri.

#kazi inaendelea#





Screenshot_20220902-113724_1.jpg
 
Yaani bima ya afya kuhudumia na raia wa kawaida waziri yeye inamuuma, anataka walipa Kodi wafe kwa kukosa pesa za matibabu ,hii si sawa kabisa,

Nimesikia pia anasema kifurushi cha bima ya watoto Cha Tsh. 50400 kipandishwe Bei,
 
Yaani bima ya afya kuhudumia na raia wa kawaida waziri yeye inamuuma, anataka walipa Kodi wafe kwa kukosa pesa za matibabu ,hii si sawa kabisa
Kabisa, Hilo waziri Ummy ameniangusha. Ni Bora mtu akose elimu Ila awe na afya njema. Afya ndio kila kitu.

Ni mara mia usijenge flyover Ila wape watu afya wataijenga flyover wao wenyewe.
 
Mawaziri wote wako hoi tu sasa hivi. Hakuna anae fanya kazi kwa makini.

Wengi wao ndio hao walamba asali na wahuni.
 
Sasa hivi wanataka kulazimisha kila mtanzania awe na bima wakati huduma hazijaboreshwa.
Tatizo sio kama anavyolisema Ummy Mwalimu Bali ni matumizi mabaya ya mfuko ikiwemo serikali kuchota pesa kila inavyojisikia
 
Wenye Akili tunajua fika KUWA MAREKANI by December itaacha kutoka fedha za afya KWA shirika la afya Duniani WHO HIVYO nchi zetu zitaathirika na ukosefu wa vifaa na madawa !

Tunaandaliwa kisaikolojia mapema KUWA Vifo kwa kukopa Dawa ni Hali yetu watz!!

Tuimbe KWA PAMOJA wimbo huu

"Rasimu ya Warioba irudi mezani Sasa iwe Katiba mpya"!
 
Waziri Ummy hili la Bima ya Afya Umeniangusha sana, hapa nilipo nina masikitiko makubwa sana ya maelezo unayoyatoa na kinachoendelea.

Ni wazi kabisa tumeanza kukwama kwenye hili ya bima ya afya.

Waziri umesema watu ambao sio watumishi ndio pia wamechangia mfuko kuelemewa na kuufanya udhoofike. Kimsingi kabisa kila mtu anapaswa kuwa na bima ya afya, wengi wamejiunga na NHIF sababu gharama za kujiunga na kulipia kwa mwaka ni ndogo kulinganisha na bima zingine. Vipato vya watanzania vinajulikana.

Afya ndio uti wa mgongo wa taifa lolote, ambae hana elimu Iia ana afya njema ataweza kuzalisha, Ila ambae hana vyote atawezaje kuzalisha? Taifa litakua la aina gani?

Tabia ya wengi huwa hawapendi kwenda hospitali hata kama ana bima, ukimuona mtanzania anaenda sana hospitali basi kweli huyo mtu ana shida kubwa. Hivyo hakuna ambae anafanya makusudi kwenda mara kwa mara hospital.

Sasa hivi pamoja na yote hayo bado Kuna mamia ya watu ambao kila siku huku mitandaoni wanaomba msaada wa matibabu. Na wewe waziri umekua mmoja wa watu wanaochangia na kusaidia hawa watu huku mitandaoni. Vipi bima ikienda kupunguza na kuweka masharti magumu zaidi, Hali itakuaje?

Ni hadi lini tutaendelea kuchangishana mitandaoni kuwasaidia walioshindwa gharama za matibabu??

Waziri ninakuomba tuwekeze zaidi kwenye afya, tubane mwingine. Kama kifaa flani cha mil 10 kinanunuliwa kwa mil. 50, basi tubane kuanzia hapo. Bado naamini pesa ipo ni kuweka tu mipango vizuri.

#kazi inaendelea#





View attachment 2343042
Taifa kubwa na tajiri kama Marekani halina bima ya afya kwa kila mwananchi- Tanzania inastahili pongezi kwa kujaribu. Shida kubwa ni upigaji wa hela za mfuko wa bima ya afya. Hospitali na zahanati nyingi zinanafanya udanganyifu wa makusudi wa kuzidisha gharama za matibabu wakijua fedha hazina mwenyewe. Ni hospitali na zahanati chache zinazojaza fomu kwa wakati ili mgonjwa analiyetibiwa aone gharama halisi ya matibabu wakati anasaini fomu. Wagonjwa wanabambikiwa madawa na matibabu feki. Hospitali zimegeuza mfuko wa bima kama njia pekee ya kujinufahisha. Ili mfuko uweze kuhimili kishindo cha kutofilisika ni lazima wadau wote wawe waaminifu- kitu ambacho si rahisi kwa nyakati hizi. Wote wanao uibia mfuko wafungwe gerezani bila huruma- kwani wanahatarisha maisha ya Watanzania wengi wasio na hatia. Waziri anasema kweli ili kuunusuru mfuko- vile vile wezi wasakwe.
 
Suala la Bima ya Afya ni changamoto kubwa sana Bado anajitahidi
 
Waziri Ummy hili la Bima ya Afya Umeniangusha sana, hapa nilipo nina masikitiko makubwa sana ya maelezo unayoyatoa na kinachoendelea.

Ni wazi kabisa tumeanza kukwama kwenye hili ya bima ya afya.

Waziri umesema watu ambao sio watumishi ndio pia wamechangia mfuko kuelemewa na kuufanya udhoofike. Kimsingi kabisa kila mtu anapaswa kuwa na bima ya afya, wengi wamejiunga na NHIF sababu gharama za kujiunga na kulipia kwa mwaka ni ndogo kulinganisha na bima zingine. Vipato vya watanzania vinajulikana.

Afya ndio uti wa mgongo wa taifa lolote, ambae hana elimu Iia ana afya njema ataweza kuzalisha, Ila ambae hana vyote atawezaje kuzalisha? Taifa litakua la aina gani?

Tabia ya wengi huwa hawapendi kwenda hospitali hata kama ana bima, ukimuona mtanzania anaenda sana hospitali basi kweli huyo mtu ana shida kubwa. Hivyo hakuna ambae anafanya makusudi kwenda mara kwa mara hospital.

Sasa hivi pamoja na yote hayo bado Kuna mamia ya watu ambao kila siku huku mitandaoni wanaomba msaada wa matibabu. Na wewe waziri umekua mmoja wa watu wanaochangia na kusaidia hawa watu huku mitandaoni. Vipi bima ikienda kupunguza na kuweka masharti magumu zaidi, Hali itakuaje?

Ni hadi lini tutaendelea kuchangishana mitandaoni kuwasaidia walioshindwa gharama za matibabu??

Waziri ninakuomba tuwekeze zaidi kwenye afya, tubane mwingine. Kama kifaa flani cha mil 10 kinanunuliwa kwa mil. 50, basi tubane kuanzia hapo. Bado naamini pesa ipo ni kuweka tu mipango vizuri.

#kazi inaendelea#





View attachment 2343042
Tatizo umelishwa .. ungekula mwenyewe ungejua tamu au chungu. Jiongeze
 
Back
Top Bottom