Wizara ya Afya Tanzania
Official Account
- Oct 1, 2020
- 58
- 124
HATUFUTI POLYCLINIC, TUNAWEKA VIGEZO VYA KUSAJILIWA NA NHIF - WAZIRI UMMY MWALIMU
Serikali imesema haikusudii kufuta Kliniki za Kibingwa (Polyclinics) zilizopo nchini bali inapitia vigezo vya kuwa na Polyclinics ambazo hivi karibuni zimeibuka kliniki nyingi ambazo zimekuwa ni vichochoro vya udanganyifu dhidi ya Mfuko wa Taifa wa NHIF.
.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu leo alipokutana na Watoa Huduma za Afya wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya wa Mkoa wa Dar Es Salaam.
"Hatufuti wala hatukusudii kufuta Polyclinics, lakini tunafanya mapitio ya vigezo vya Polyclinics kwasababu ndio kichochoro kingine cha udanganyifu dhidi ya NHIF na ndio maana kuna wingi wa Kliniki za Kibingwa zinazoanzishwa amabzo hazina vigezo kwa sababu ya kufanya udanganyifu” amesema Waziri Ummy Mwalimu.