Waziri; TANESCO imeshindwa.....

Waziri; TANESCO imeshindwa.....

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,946
Reaction score
38,657
Ukurasa wa Nne wa Gazeti la Nipashe la leo Umeandikwa hivi; TANESCO IMESHINDWA...

Waziri wa Nishati akiri kushindwa kwa Tanesco kuzalisha umeme, kwa hiyo sasa Shirika hilo litabakia kama wasambazaji tu, wa huduma hiyo! Uzalishaji utafanywa na makampuni ya nje na ndani ya Nchi.


NB
nilishaweka humu taarifa kutoka kwa mtonyaji wa kutoka shirikani kuhusu mpango wa kuligawa shirika hili kwa maharamia ili kupunguza mapato ya serikali.

Wamehakikisha wamelidhoofisha shirika lisiweze kufanya kazi ili kutimiza AZMA yao.

WITO
Bunge liunde kamati maalumu kufuatilia undani wa kulifikisha shirika ktk kushindwa kuhudumia kama litakiwavyo. Na pia kuichunguza kauli ya Waziri kuona kama kuna uingiliwaji kisiasa kwenye utendaji wa shirika. Tuna haki ya kujua ili kuliboresha.

ENRON case
 
Ukurasa wa Nne wa Gazeti la Nipashe la leo Umeandikwa hivi; TANESCO IMESHINDWA...

Waziri wa Nishati akiri kushindwa kwa Tanesco kuzalisha umeme, kwa hiyo sasa Shirika hilo litabakia kama wasambazaji tu, wa huduma hiyo! Uzalishaji utafanywa na makampuni ya nje na ndani ya Nchi.


NB
nilishaweka humu taarifa kutoka kwa mtonyaji wa kutoka shirikani kuhusu mpango wa kuligawa shirika hili kwa maharamia ili kupunguza mapato ya serikali.

Wamehakikisha wamelidhoofisha shirika lisiweze kufanya kazi ili kutimiza AZMA yao.

WITO
Bunge liunde kamati maalumu kufuatilia undani wa kulifikisha shirika ktk kushindwa kuhudumia kama litakiwavyo. Na pia kuichunguza kauli ya Waziri kuona kama kuna uingiliwaji kisiasa kwenye utendaji wa shirika. Tuna haki ya kujua ili kuliboresha.

ENRON case
Kama imeshindwa kuzalisha, kusambaza ndio haiwezi kabisa. Mzalishaji huwa hana kazi ngumu kama msambazaji, maana msambazaji ndie anaepambana na vishoka. hiki ni kitendawili tega.
 
Ni jambo la kusikitisha na kutia simanzi kwa viongozi wetu kila mara kujaribu kubuni mambo mapya ambayo hayajafanyiwa utafiti na kuanza kuyafanyia kazi!

Ni kweli kuwa TANESCO kuna matatizo ambayo baadhi yamesababishwa na utendaji mbovu ndani yake lakini pia kuna matatizo yamesababishwa na serikali!!

Hivyo kinachotakiwa ni kuyarekebisha na siyo kulifumua shirika! Serikali inapaswa kuiacha TANESCO huru ili iweze kukabili na kutatua matatizo yake na siyo kupeleka siasa!
 
Kama imeshindwa kuzalisha, kusambaza ndio haiwezi kabisa. Mzalishaji huwa hana kazi ngumu kama msambazaji, maana msambazaji ndie anaepambana na vishoka. hiki ni kitendawili tega.
Hapana mkuu.

Kama shirika lisingeingiliwa na wanasiasa kimaamuzi linaweza kuzalisha umeme hadi wa kuuza nje. Kinachotokea hapa ni kugawa mapato ya serikali ili kuwezesha vilembwe wa mabwanyenye kunyonya zaidi.

Bajeti inayopangiwa haipelekwi hata nusu yake, kisha serikali na idara zake ndo wanatumia umeme bila kulipia.....
kuna factors ambazo zikirekebishwa shirika linaweza kurudi kwenye tija
 
Akili za kuambiwa jaribuni kuchanganya na zenu, mie nimemsikia waziri wakati anazungumzia jambo hilo alikuwa very positive isipokuwa tunapenda kutafasiri tunavyotaka na si kama ilivyokusudiwa, na mnukuu ni lazima katika kipindi kifupi kijacho tuwe na umeme wa kutosha na uhakika sasa kusubiri tanesco wajenge uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia tech ya upepo kisha jua kisha makaa ya mawe na mbeleni madini urani nikuota ndoto za mchana akaendelea uchumi wa kisasa ni kuweza kuvutia mitaji ya watu kuja kwenu na sasa ndio kinachofanyika ilikukuza uchumi kwa haraka zaidi, jamani huo ndio ukweli tukikaa kusubiri kauli za viongozi kila wakati in a negative attitude hatutatoka hapa tulipo, tusijenge taifa la majungu kila wakati na mambo ya vyama yasitufanye kuwa watumwa wa kufikiri

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Akili za kuambiwa jaribuni kuchanganya na zenu, mie nimemsikia waziri wakati anazungumzia jambo hilo alikuwa very positive....
Mkuu unakumbuka hata Karamagi, Msabaha na Lowassa walikuwa very positive kuhusu issue ya kuinginza mkenge serikali kupitia mkataba wa RICHMOND?

Unajua kwamba how positive viongozi wetu walivyokuwa wakati wa kubinafsisha TRL, ATCL, TTCL na kadhalika?

Hapa tunachokiona ni mkanda wa matukio kujirudia chini ya mchezeshaji mwingine.
 
Acha tu na makampuni mengine yaingie ubia nakumbuka enzi za TTCL jinsi gharama za kupiga simu zilivyokuwa juu kina vodacom wametusaidia huenda bei ya umeme itashuka.
 
Ni jambo la kusikitisha na kutia simanzi kwa viongozi wetu kila mara kujaribu kubuni mambo mapya ambayo hayajafanyiwa utafiti na kuanza kuyafanyia kazi!

Ni kweli kuwa TANESCO kuna matatizo ambayo baadhi yamesababishwa na utendaji mbovu ndani yake lakini pia kuna matatizo yamesababishwa na serikali!!

Hivyo kinachotakiwa ni kuyarekebisha na siyo kulifumua shirika! Serikali inapaswa kuiacha TANESCO huru ili iweze kukabili na kutatua matatizo yake na siyo kupeleka siasa!




Hapa kila mtu anataka apate chake, viongozi wa serikali pammoja na hao wa tanesco.
Cha muhimu ni kwamba haya masuala ya umeme yawe private tu, kama huku ulaya kulivyo. Kuna makampuni tofauti yanayo zalisha umeme, na kuna wasambazaji wa umeme tofauti. kila mtu ana bei yake kwa hiyo ni wewe mteja kuamua uchague msambazaji gani. Hata hao wasabazaji pia inabidi uangalie, kuna hao wa bei ya chini sana lakini ujue hutapata huduma kamilifu lakini uko huru kubadilisha msambazaji wakati wowote
 
Acha tu na makampuni mengine yaingie ubia nakumbuka enzi za TTCL jinsi gharama za kupiga simu zilivyokuwa juu kina vodacom wametusaidia huenda bei ya umeme itashuka.
Lakini upungufu wa bei za simu za mkononi na wingi wa wateja kwa makampuni hayo kunawiana na ukusanyaji mapato kutoka kampuni hizo?
 
ukurasa wa nne wa gazeti la nipashe la leo umeandikwa hivi; tanesco imeshindwa...

Waziri wa nishati akiri kushindwa kwa tanesco kuzalisha umeme, kwa hiyo sasa shirika hilo litabakia kama wasambazaji tu, wa huduma hiyo! Uzalishaji utafanywa na makampuni ya nje na ndani ya nchi.


nb
nilishaweka humu taarifa kutoka kwa mtonyaji wa kutoka shirikani kuhusu mpango wa kuligawa shirika hili kwa maharamia ili kupunguza mapato ya serikali.

Wamehakikisha wamelidhoofisha shirika lisiweze kufanya kazi ili kutimiza azma yao.

wito
bunge liunde kamati maalumu kufuatilia undani wa kulifikisha shirika ktk kushindwa kuhudumia kama litakiwavyo. Na pia kuichunguza kauli ya waziri kuona kama kuna uingiliwaji kisiasa kwenye utendaji wa shirika. Tuna haki ya kujua ili kuliboresha.

Enron case
bora watanzania tuutue mzigo huo
 
naona ile trailer ndio muvi yake inaanza tena.
 
Nchi hii sijui inakwenda wapi jamani. a moment nilipomuona balozi wa Marekani pale wizarani eti alikwenda kumpongeza waziri kwa kuteuliwa kwake nilijua tumekwisha...Hillary Clinton alikuja Tanzania eti kwa issue ya Symbio Power!
Hatufanyi tafiti? wote wamenunuliwa? hakuna wazalendo waliobaki nchi hii jamani... Kwa mujibu wa kile kitabu cha comfesion of Economic Hit Men... Marekani huwa wanatemper na power production and transmission katika nchi mbali mbali...Kupitia mpango huwa nchi nyingi zimejikuta tegemezi kutokana na madeni makubwa ambayo huingiwa kwa kujua ama kutokujua...
TANESCO wanazilipa AGRECO, IPTL, SYMBION, SONGAS kiasi gani kwa siku? Pamoja na malipo hayo kuwa makubwa kiasi hicho bado Umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji ni 75%... Kwanin hakufanyiki uwekezaji zaidi kwenye hydroelectric power?...Huu mpango wa prof Muhongo unalenga kuizika TANESCO na kuwasababishia wananchi mzigo mkubwa wa maisha. Mpango huu unamaanisha uharibifu wa mazingira zaidi kwa siku za usoni kwani kuni na mkaa vitandelea kuwa source of energy kwa wengi... Gesi haishikiki kwakuwa wamiliki ni wale wale wenye kutuletea hapa nchini! ...
TISS hamyaoni haya? mnawashauri lakini?...
 
Watawala wetu wameweka kipaumbele cha kwanza KUWAPENDEZESHA nchi wahisani. Kisha wananchi ndo tunafuati tena kwa shingo upande.

Tunachoweza sasa ni kusimamisha mpango huu kupitia vyombo vya sheria kama hatua ya awali
 
Huyu Waziri wa Nishati wa sasa hivi ndio hana jipya kuweza kuwapiku wenzie waliotangulia mbele yake . Tatizo ya Siasa kuingiza kwenye fani ndizo kikwaza kwa hii Tanzania yetu . Pia mengi ya Mashirika yetu hapa nchini yamefunga shughuli zake kwa sababu tu ya Wanasiasa kuingiza mikono yao ya kifisadi ndani yake . Tanesco iache ijisimamie yenyewe katika masuala ya Maamuzi na Utendaji na Serikali pia kupitia mashirika na Taasisi zilizo chini yake zilipe matumizi yake kwa wakati na bila kikwazo tuone kama Tanesco itashindwa kazi iliyopewa ya kuzalisha Umeme na kusambaza kwa faida . Muhongo ndiye kashindwa kuongoza Wizara hiyo na sio Tanesco
 
muhongo is doing very fine kuhakikisha umeme unapatikana na tangu achukue wizara hii mgawo haupo tena
 
Ukurasa wa Nne wa Gazeti la Nipashe la leo Umeandikwa hivi; TANESCO IMESHINDWA...

Waziri wa Nishati akiri kushindwa kwa Tanesco kuzalisha umeme, kwa hiyo sasa Shirika hilo litabakia kama wasambazaji tu, wa huduma hiyo! Uzalishaji utafanywa na makampuni ya nje na ndani ya Nchi.


NB
nilishaweka humu taarifa kutoka kwa mtonyaji wa kutoka shirikani kuhusu mpango wa kuligawa shirika hili kwa maharamia ili kupunguza mapato ya serikali.

Wamehakikisha wamelidhoofisha shirika lisiweze kufanya kazi ili kutimiza AZMA yao.

WITO
Bunge liunde kamati maalumu kufuatilia undani wa kulifikisha shirika ktk kushindwa kuhudumia kama litakiwavyo. Na pia kuichunguza kauli ya Waziri kuona kama kuna uingiliwaji kisiasa kwenye utendaji wa shirika. Tuna haki ya kujua ili kuliboresha.

ENRON case

peleka usanii wako huko, kwanini usiweke taarifa kamili hapa watu wasome wenyewe, unatuwekea maoni yako...look at you!!!
 
Back
Top Bottom