Waziri Simbachawene apendekeza Watumishi wa Umma wasiingie ofisini na simu

Hili pendekezo ni kiki, kwasababu binafsi sijawahi enda ofisi ya umma nikaacha kuhudumiwa eti mtu anachati.

===

View attachment 2577052

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameeleza dhamira yake ya kushirikiana na watumishi wa ofisi yake katika kutekeleza jukumu la kuwasimamia watumishi wa umma nchini kutumia vizuri saa za kazi kuwahudumia wananchi badala ya kufanya mambo ambayo yanakwamisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Simbachawene ameweka wazi dhamira hiyo ya kuwasimamia watumishi wa umma kutekeleza wajibu wao kikamilifu pindi alipowasili ofisini kwake na kuzungumza na watumishi wa ofisi yake waliompokea mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Aprili, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam kuwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora nchini.

Mhe. Simbachawene amesema, rasilimaliwatu ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa lolote, hivyo ni lazima ofisi yake ihakikishe watumishi wa umma wanafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni, Sheria, Taratibu, Miongozo na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo sheria mama ya nchi.

Mhe. Simbachawene ameeleza kuwa, wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma wamekuwa wakilalamika kutopatiwa huduma nzuri na kwa wakati, na kuongeza kuwa, baadhi ya watumishi wa umma wamekuwa wakifanya shughuli zao binafsi mahala pa kazi wakati wananchi wakisubiria kupatiwa huduma.

“Muda ambao mtumishi wa umma anatakiwa kufanya kazi ni saa nane, lakini utakuta mtumishi akiingia kazini anakuwa na pilika nyingine ambazo si za kazi anayopaswa kuifanya, akitoa mfano wa Muuguzi au Mwalimu anaposhindwa kuwajibika, madhara yake ni makubwa na taifa linapata hasara kubwa kwasababu rasilimaliwatu haitumiki ipasavyo,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, mtumishi anaingia kazini na simu ambayo ina makundi mengi, akianza kuwasiliana na makundi matatu tu saa moja ya kazi imeondoka na kwa kuwa ana makundi ya majirani, vikoba na mengineyo hivyo akiendelea kushiriki kinachojadiliwa unakuta matumizi ya simu yanachukua muda mwingi wa kazi

Utumishi
Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, mtumishi anaingia kazini na simu ambayo ina makundi mengi, akianza kuwasiliana na makundi matatu tu saa moja ya kazi imeondoka na kwa kuwa ana makundi ya majirani, vikoba na mengineyo hivyo akiendelea kushiriki kinachojadiliwa unakuta matumizi ya simu yanachukua muda mwingi wa kazi

Utumishi

NDIO MAANA KUNA TOFAUTI YA MTOTO NA MTU MZIMA.....

IKIWA MTU MZIMA ANAPO GEUKA MTOTO LAZIMA TU M TREAT KAMA MTOTO....

MM KAZI NAZO FANYA NINA DEAL NA WATU MUDA MWINGI ILA SIMU HAIJAWAI KUA TATIZO, TATIZO NI WATU WENYEWE TENA WATU WAZIMA WANATAKA WAANZE TRITIWA KAMA WATOTO WA MSINGI AU SECONDARY SCHOOL.....
 
Mawasiliano mfano simu ni sehemu ya kazi kwasasa ndomana walimu wakapewa vishikwambi...
huyu sindio yule mwanae mlevi alisumbua askari eeh? Like father like son!!
Shughulika watumishi wapande madaraja ipasavyo acha kujishughulisha na maujinga.
 
Haya majitu ni majinga sana ,yanaiba huko harafu wanakuja kusumbua Watumishi.
 
Litakuwa linawahusu hao watumishi walioko wizarani maana hawa wengine huku chini sijawahi enda ofisi yoyote nikakosa huduma kisa mtu anabembeleza mchepuko au danga.
Thanks mkuu, maana Kila baya watumishi huwa tunaonekana shida ila Kuna wananchi wasema kweli kama wewe wachache sana. Asante sana mkuu
 
  • Thanks
Reactions: K11
Hili pendekezo ni kiki, kwasababu binafsi sijawahi enda ofisi ya umma nikaacha kuhudumiwa eti mtu anachati.

===

View attachment 2577052

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameeleza dhamira yake ya kushirikiana na watumishi wa ofisi yake katika kutekeleza jukumu la kuwasimamia watumishi wa umma nchini kutumia vizuri saa za kazi kuwahudumia wananchi badala ya kufanya mambo ambayo yanakwamisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Mhe. Simbachawene ameweka wazi dhamira hiyo ya kuwasimamia watumishi wa umma kutekeleza wajibu wao kikamilifu pindi alipowasili ofisini kwake na kuzungumza na watumishi wa ofisi yake waliompokea mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Aprili, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam kuwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora nchini.

Mhe. Simbachawene amesema, rasilimaliwatu ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa lolote, hivyo ni lazima ofisi yake ihakikishe watumishi wa umma wanafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni, Sheria, Taratibu, Miongozo na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo sheria mama ya nchi.

Mhe. Simbachawene ameeleza kuwa, wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma wamekuwa wakilalamika kutopatiwa huduma nzuri na kwa wakati, na kuongeza kuwa, baadhi ya watumishi wa umma wamekuwa wakifanya shughuli zao binafsi mahala pa kazi wakati wananchi wakisubiria kupatiwa huduma.

“Muda ambao mtumishi wa umma anatakiwa kufanya kazi ni saa nane, lakini utakuta mtumishi akiingia kazini anakuwa na pilika nyingine ambazo si za kazi anayopaswa kuifanya, akitoa mfano wa Muuguzi au Mwalimu anaposhindwa kuwajibika, madhara yake ni makubwa na taifa linapata hasara kubwa kwasababu rasilimaliwatu haitumiki ipasavyo,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.

Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, mtumishi anaingia kazini na simu ambayo ina makundi mengi, akianza kuwasiliana na makundi matatu tu saa moja ya kazi imeondoka na kwa kuwa ana makundi ya majirani, vikoba na mengineyo hivyo akiendelea kushiriki kinachojadiliwa unakuta matumizi ya simu yanachukua muda mwingi wa kazi

Utumishi
Ujinga ndio unaanziaga hapa.Akitaka kwenda kutembea ofisi fulani atawatafuta kwa mguu
 
Simu ni sehemu ya kisaidizi cha mtumishi, waziri apambane na matatizo makubwa ya kiutumishi kama uchelewashaji wa mishahara, madaraja, uonevu wa kingono, etc etc, mimi mwenyewe ninashuhudia sana customs officials wetu wakitumia simu kupata informations nyingi za product's zinazoingia nchini, aachane na Kiki mfu
Utumishi katika nchi ina matatizo mengi na makubwa kuliko hilo dogo analobainisha huyo Chawene .Walimu na manesi aliowatolea mfano ni watumishi wenye matatizo lukuki yakiwemo ya maslahi madogo na kutolipwa malimbikizo ya mishahara yao kwa wengine tangu 2017 hayo magroup wataingia kwa saa nzima data ataweka yeye
 
Halafu sio vizuri kuwafanya wafumishi wenzio kama sio binadamu wasio na haki,yapo mazuri mengi wanafanya kwa taifa lao licha ya changamoto nyingi walizo nazo.
Tujifunze kuwakosoa kwa hekima na pale inapobidi pia tuwapongeze isionekane wote hawana jema.
Kuna miaka kulikuwa na nidhamu public service kwani husikii wenzio wakisema?Simu hazikuwepo?
Fanya utafiti wako vizuri,njoo na suluhu lenye afya kwa kuzingatia mizania sawa hautapigwa mawe.
Kwa hili umeteleza pakubwa.
 
Mawazo,,fikra,,maono,, ya viongozi wetu wakati mwingine yanashangaza sana,,,kuna mambo mengi sana yakufanyia kazi kwa wafanyakazi wa serikali,,Uache kuzungumzia uboreshaji wa mazingira yao ya kazi,maslahi kwa wafanyakazi,,,promesheni za motisha kwa wafanyakazi ili kuongeza chachu katika utendaji,,,kubuni na kuunda mifumo bora ambayo itakuwa bora na italeta angalua ahueni kwa hao wafanyakazi nk,,,,Simu kweli ndio inakuwa ajenda ya maana na kuzungumzwa??Na makamera juu kwa ishu ambayo haina maana kabisa,,,na wala sidhani kama ni tija kwa sasa kwa hao wafanyakazi,,,,Ajenda nzuri,,kanuni na sheria bora wanajitungiaga wao kwa maslahi yao,,,wengine wasiwe na simu kwa ulimwengu huu wa sasa wa teknolojia simu haikwepeki,,popote pale!!!Akajipange aje na hoja za maana!!!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Wow 🤣🤣🤣🤣🤣

Kweli tumebalikiwa na ujinga tele. I mean what the fuc*k is wrong with viongozi hawa??

Keep recycling and reusing the same people and hoping for a different outcome!

WOW!
 
Badala ya kuongelea namna atakavyoshughulikia maslahi ya watumishi ikiwemo kulipa mishahara stahiki na allowances za nyumba, usafiri, maji, umeme, chakula kazini na kufuta kikokotoo cha kinyonyaji anaanza na porojo? hii ni kiashiria kwamba watumishi safari hii watakutana na surprise ileile ya mwaka jana, nyongeza ya asilimia 23 kuishia kuwa buku mbili...​
Ningemuona ana akili kama angekuja na mpango wa kuhakikisha kila mtumishi wa umma madai yake yaliyohakikiwa yanalipwa ndani ya miezi miwili na yale yaliyobado kuhakikishiwa yanalipwa ndani ya miezi minne ili hao watumishi wasifanye kazi kwa kinyongo na kuongeza ufanisi wa kuwahudumia watanzania.Tutamuona huyo jamaa atakavyoperform naona anajaribu kudeal na vitu minor sana hakuna Mtumishi atajizuia kutumia simu kwa masaa 8 simply ameagiza huyo Simbachawene
 
Back
Top Bottom