ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,115
- 49,840
Hili pendekezo ni kiki, kwasababu binafsi sijawahi enda ofisi ya umma nikaacha kuhudumiwa eti mtu anachati.
===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameeleza dhamira yake ya kushirikiana na watumishi wa ofisi yake katika kutekeleza jukumu la kuwasimamia watumishi wa umma nchini kutumia vizuri saa za kazi kuwahudumia wananchi badala ya kufanya mambo ambayo yanakwamisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Mhe. Simbachawene ameweka wazi dhamira hiyo ya kuwasimamia watumishi wa umma kutekeleza wajibu wao kikamilifu pindi alipowasili ofisini kwake na kuzungumza na watumishi wa ofisi yake waliompokea mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Aprili, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam kuwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora nchini.
Mhe. Simbachawene amesema, rasilimaliwatu ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa lolote, hivyo ni lazima ofisi yake ihakikishe watumishi wa umma wanafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni, Sheria, Taratibu, Miongozo na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo sheria mama ya nchi.
Mhe. Simbachawene ameeleza kuwa, wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma wamekuwa wakilalamika kutopatiwa huduma nzuri na kwa wakati, na kuongeza kuwa, baadhi ya watumishi wa umma wamekuwa wakifanya shughuli zao binafsi mahala pa kazi wakati wananchi wakisubiria kupatiwa huduma.
“Muda ambao mtumishi wa umma anatakiwa kufanya kazi ni saa nane, lakini utakuta mtumishi akiingia kazini anakuwa na pilika nyingine ambazo si za kazi anayopaswa kuifanya, akitoa mfano wa Muuguzi au Mwalimu anaposhindwa kuwajibika, madhara yake ni makubwa na taifa linapata hasara kubwa kwasababu rasilimaliwatu haitumiki ipasavyo,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.
Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, mtumishi anaingia kazini na simu ambayo ina makundi mengi, akianza kuwasiliana na makundi matatu tu saa moja ya kazi imeondoka na kwa kuwa ana makundi ya majirani, vikoba na mengineyo hivyo akiendelea kushiriki kinachojadiliwa unakuta matumizi ya simu yanachukua muda mwingi wa kazi
Utumishi
===
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ameeleza dhamira yake ya kushirikiana na watumishi wa ofisi yake katika kutekeleza jukumu la kuwasimamia watumishi wa umma nchini kutumia vizuri saa za kazi kuwahudumia wananchi badala ya kufanya mambo ambayo yanakwamisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Mhe. Simbachawene ameweka wazi dhamira hiyo ya kuwasimamia watumishi wa umma kutekeleza wajibu wao kikamilifu pindi alipowasili ofisini kwake na kuzungumza na watumishi wa ofisi yake waliompokea mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 02 Aprili, 2023 Ikulu Jijini Dar es Salaam kuwa waziri mwenye dhamana ya kusimamia Utumishi wa Umma na Utawala Bora nchini.
Mhe. Simbachawene amesema, rasilimaliwatu ni muhimu sana katika maendeleo ya taifa lolote, hivyo ni lazima ofisi yake ihakikishe watumishi wa umma wanafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni, Sheria, Taratibu, Miongozo na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ndiyo sheria mama ya nchi.
Mhe. Simbachawene ameeleza kuwa, wateja wanaofuata huduma katika taasisi za umma wamekuwa wakilalamika kutopatiwa huduma nzuri na kwa wakati, na kuongeza kuwa, baadhi ya watumishi wa umma wamekuwa wakifanya shughuli zao binafsi mahala pa kazi wakati wananchi wakisubiria kupatiwa huduma.
“Muda ambao mtumishi wa umma anatakiwa kufanya kazi ni saa nane, lakini utakuta mtumishi akiingia kazini anakuwa na pilika nyingine ambazo si za kazi anayopaswa kuifanya, akitoa mfano wa Muuguzi au Mwalimu anaposhindwa kuwajibika, madhara yake ni makubwa na taifa linapata hasara kubwa kwasababu rasilimaliwatu haitumiki ipasavyo,” Mhe. Simbachawene amesisitiza.
Mhe. Simbachawene ameongeza kuwa, mtumishi anaingia kazini na simu ambayo ina makundi mengi, akianza kuwasiliana na makundi matatu tu saa moja ya kazi imeondoka na kwa kuwa ana makundi ya majirani, vikoba na mengineyo hivyo akiendelea kushiriki kinachojadiliwa unakuta matumizi ya simu yanachukua muda mwingi wa kazi
Utumishi