Waziri Ndugulile kajifunze Kenya maana ya digital revolution

chase amante

JF-Expert Member
Feb 24, 2018
5,553
2,073
Nawasalimu kwa jina la jamhuri ya muungano.

Waziri wa Teknolojia na mawasiliano, jana alitangaza kua anawakaribisha watu kuwekeza kwenye mtandao wa 5G nchini Tanzania, na pia mpango wake wa kubadili mfumo wa 2G kwenda 3G unaotumika kwenye simu za tochi.

Pia, akatangaza na mpango wake wa miaka mitano wa wizara yake kuanzia 2021-2022 hadi 2025-2026 wa kuiendeleza sekta hii ya mawasiliano na teknolojia.

Nakiri, hiyo Yote ni mipango mizuri lakini haitoshi kutufikisha kwenye maana halisi ya mapinduzi ya kidigitali.

Mapinduzi ya kidigitali(digital revolution) nchini tanzania yameanza miaka ya 2005,na yalihusisha ujenzi wa mkongo wa taifa na minara ya simu.

mapinduzi haya, yanahusisha uwepo wa CCTV kamera, drones, maroboti na miji ya kisasa(smart cities).yana faida nyingi km kuongeza makusanya ya kodi na kupunguza rushwa, kupunguza uharifu na mengineyo.

Pia yana athari nyingi sana, ambazo zingine tunazioana kupitia wizi wa kwenye mitandao na simu.pia yanaweza kutumika kuchunguza watu, kuiba taarifa za watu bila ridhaa yao.


Kenya na Rwanda ni nchi zilizoendelea sana kwenye mapinduzi ya kigitali na ni majirani zetu. Lkn sisi bado tupo nyuma sana. Kwanza, mkongo wa taifa haujafika maeneo ya vijijini. Hii inawakosesha fulsa wananchi wa kijijini zikiwemo kupata intaneti.

Na kuna uhusiano mkubwa sana kati ya kuwepo kwa 3g coverage na ustawi wa jamii. Kuna utafiti ulifanywa senagal (nimekosa link yake), ulionyesha maeneo yenye coverage 3g, wananchi wake waliongeza matumizi kwa 14% na kupunguza umaskini kwa 10%.

Hata smart cities hapa Tanzania Sidhani kama zipo. Waziri aende kujifunza Kenya, kwani huo ndo ujirani mwema.


Sisemi kwamba tukurupukie tu hizi teknolojia, bali tutumie muda kujifunza faida zake , na hasara zake kisha tuamue zipi nzuri na zipi mbaya.
 
Nilimshangaa sana waziri!

Anataka kuleta mapinguzi ya kidigitali wakati anatoza kodi kwenye youtube channel na blogs?

Hajui, ni wabunifu wangapi wamekwama kuendeleza vipaji vyao, baada ya kufunga blogs na youtube channels baada ya kukosa hela za kulipia kodi?

Yeye anahisi waliokuwa na blogs na youtube channels, walikuwa ni wanaharakati tu wa kuipinga serikali? Hajui watu wengine walikuwa wanapost ubunifu mbalimbali tofauti na siasa?
 
Huyu waziri ni mpumbavu zaidi ya yule mfu wa Chato aliyemuweka hapo,anashindwa hata kuzungumzia namna ya kuiruhusu mifumo ya malipo ya mtandaoni kama vile PayPal nk.

Yeye anawaza maminara tu ya simu & tozo
 
Nilimshangaa sana waziri!

Anataka kuleta mapinguzi ya kidigitali wakati anatoza kodi kwenye youtube channel na blogs?

Hajui, ni wabunifu wangapi wamekwama kuendeleza vipaji vyao, baada ya kufunga blogs na youtube channels baada ya kukosa hela za kulipia kodi?

Yeye anahisi waliokuwa na blogs na youtube channels, walikuwa ni wanaharakati tu wa kuipinga serikali? Hajui watu wengine walikuwa wanapost ubunifu mbalimbali tofauti na siasa?
Nakisura chake domo lilivopinda vile muda wote anadhani kilamtu nimakonda
 
Huyu waziri ni mpumbavu zaidi ya yule mfu wa Chato aliyemuweka hapo,anashindwa hata kuzungumzia namna ya kuiruhusu mifumo ya malipo ya mtandaoni kama vile PayPal nk.

Yeye anawaza maminara tu ya simu & tozo
Mtanzania ili kufaidi paypal instant deposit na withdrawals inabidii upate the better option- safaricom baba lao.
 
Nakumbuka huyu waziri alipoteuliwa tu na JPM, kati ya matamko yake ya kwanza ilikuwa kudhibiti matumizi ya WhatsApp. Ushauri wako ni mzuri lakini nina mashaka na uwezo wa waziri kuleta mapinduzi uliyo yataja.
 
Back
Top Bottom