Waziri Nape,tunasubiri utekelezaji wa kauli yako Clouds pamoja na ripoti ya uchunguzi kuhusu uvamizi

Mdakuzi mkuu

JF-Expert Member
Dec 27, 2016
212
720
Nape ,Nape kulikoni?Umesimamia upande gani?Ukakasi huu..

Suala la mtu fulani kuvamia kituo cha Clouds lilileta sintofahamu mpaka ukaamua kuwatembelea na kusema mawili matatu, ikiwemo kuchukua hatua baada ya ripoti ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza swala hili,ambayo wewe mwenyewe ulisema ingekamilika na kukabidhiwa ndani ya masaa 24 (juzi jumatatu, March 20,2017).

Lakini katikati kamati ikiwa kwenye uchunguzi,Mh Rais alisema "Makonda chapa kazi, nasema chapa kazi". Ilikuwa katika kukoleza kwamba,Makonda alikuwa na yupo sahihi kwenye tukio la uvamizi Clouds Media.

Sasa wewe Nape, kauli yako ya kwamba mtatoa maamuzi na mtachukua hatua kali imekaaje hii?Maana bado tunasubiri.

Kama imezimwa na kwamba huwezi tena, tengua kauli yako na si kukaa kimya tu. Kama vipi hamia CHADEMA kama mwenzako Msukuma wa Geita.

Asubuhi njema.
 
Mkuu ina maana wewe huwajui hao CCM??hao ni sawasawa na panya wanauma huku wanapuliza hapo ni maigizo lla hakuna jipya
 
Nape ,Nape kulikoni?Umesimamia upande gani?Ukakasi huu..

Suala la mtu fulani kuvamia kituo cha Clouds lilileta sintofahamu mpaka ukaamua kuwatembelea na kusema mawili matatu, ikiwemo kuchukua hatua baada ya ripoti ya kamati iliyoteuliwa kuchunguza swala hili,ambayo wewe mwenyewe ulisema ingekamilika na kukabidhiwa ndani ya masaa 24 (juzi jumatatu, March 20,2017).

Lakini katikati kamati ikiwa kwenye uchunguzi,Mh Rais alisema "Makonda chapa kazi, nasema chapa kazi". Ilikuwa katika kukoleza kwamba,Makonda alikuwa na yupo sahihi kwenye tukio la uvamizi Clouds Media.

Sasa wewe Nape, kauli yako ya kwamba mtatoa maamuzi na mtachukua hatua kali imekaaje hii?Maana bado tunasubiri.

Kama imezimwa na kwamba huwezi tena, tengua kauli yako na si kukaa kimya tu. Kama vipi hamia CHADEMA kama mwenzako Msukuma wa Geita.

Asubuhi njema.
Hili bandiko naona kama limeandikwa na mtu aishiye Honolulu!!
 
Back
Top Bottom