Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,929
Waziri wa Habari, Harrison Mwakyembe amesema suala la ving'amuzi lisingefika hapa lilipo kama watu wa sekta binafsi ya habari wangekuwa wanakiri makosa ili kurekebishana
Azam, DSTV na Zuku vilirusha maudhui ya ndani kinyume na leseni zao na pia walifanya hivyo ikiwa mitambo yao haipo nchini
Amesema tulipohama kutoka Analojia kwenda dijitali Serikali ilitenganisha kazi za kutengeneza maudhui na kazi ya kurusha matangazo ili zisifanywe na mtu mmoja
Kazi ya kutengeneza maudhui inafanywa na vituo vyote vya runinga kama ITV, TBC, Clouds TV na vituo vingine huku wanaorusha matangazo wakiwa wa aina mbili; Aina ya kwanza ni wale watakaorusha matangazo ya watanzania ambayo ni bure na pili ni wale wanaorusha matangazo kwa kulipwa(Subscription)
Aidha, leseni zenyewe pia zinatofautiana namna ya kulipia, anayechukua leseni ya kurusha matangazo bure(free to air) analipia dola za kimarekani laki 4 na anayechukua leseni kwa ajili ya kulipwa analipia leseni dola za kimarekani laki 1
Sasa hawa waliingilia leseni za wengine na kukiuka leseni zao na walivyoambiwa walienda Mahakamani, kwa vile wizara, TCRA na mamlaka nyingine zinaheshimu utawala wa sheria ziliwaacha.
Asema "Hivyo kwa miaka kama mitatu hivi tunawaangalia tu ambapo ingekuwa nchi nyingine wangepelekwa mahakamani"
Mahakama iliwaambia kuwa wameenda sehemu sio na kuwataka waende kwenye tribunal of competition kama sheria itakavyo ambapo huko walishindwa kesi. Waliposhindwa kesi hiyo sasa ndipo walipoambiwa waondoe maudhui hayo kama leseni zao zinavyotaka
"Baada ya kuziondoa ndio wanaanza kupia kelele kwamba channel zimeondolewa bila kusema ukweli ulivyo. Ting, Continental, Digitek na Startimes alichukuwa hizi channel na kuzirusha bure ambapo wao walisema kuwa hela yao wataipata kwenye matangazo tu. Ila watu naona wang'angania na kulilia tu Azam, DSTV na Zuku" amesema Mwakyembe
Maudhui ya kitanzania yanatakiwa kuwa bure sio kwa kuwa tumependa yawe bure ila ni kwa mujibu wa kikatiba ambapo mwananchi ana haki ya kupata habari kitu ambacho sio kipya bali ni toka uhuru. Na wanaorusha maudhui ya ndani lazima mitambo yao iwe imesimikwa ndani ya nchi yenyewe na ndio utaratibu duniani kote
Digitek, Ting, Startimes na Continental mitambo yao ipo hapa nchini ila Azam mitambo yao haipo hapa nchini ipo Mauritius lakini sasa hawasemi ukweli. Kwa namna hiyo serikali haina uhuru wa kuambia Azam wabadili chochote kama mambo yakiharibika mpaka wao wasiliane na mamlaka za huko mitambo ilipo ili zikubali au zikatae.....sasa huwezi kuendesha nchi namna hiyo. DSTV wapo Dubai na Zuku wapo Kenya
Waziri Mwakyembe amesema kuwa tamthilia, mpira na vitu kama hivyo wanaweza kuendelea kuonesha kwa kuwa vipo kwenye leseni zao ila kile ambavyo Mtanzania lazima akipate; Taarifa ya Habari na Matukio muhimu mengine ikiwa ni hotuba za viongozi na mengine hatakiwi kulipia
Ameongeza kuwa "Kwa sasa mimi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali tunaangalia ni kiasi gani walipata na sakata hili likiisha lazima warejeshe fedha hizo"
Azam, DSTV na Zuku vilirusha maudhui ya ndani kinyume na leseni zao na pia walifanya hivyo ikiwa mitambo yao haipo nchini
Amesema tulipohama kutoka Analojia kwenda dijitali Serikali ilitenganisha kazi za kutengeneza maudhui na kazi ya kurusha matangazo ili zisifanywe na mtu mmoja
Kazi ya kutengeneza maudhui inafanywa na vituo vyote vya runinga kama ITV, TBC, Clouds TV na vituo vingine huku wanaorusha matangazo wakiwa wa aina mbili; Aina ya kwanza ni wale watakaorusha matangazo ya watanzania ambayo ni bure na pili ni wale wanaorusha matangazo kwa kulipwa(Subscription)
Aidha, leseni zenyewe pia zinatofautiana namna ya kulipia, anayechukua leseni ya kurusha matangazo bure(free to air) analipia dola za kimarekani laki 4 na anayechukua leseni kwa ajili ya kulipwa analipia leseni dola za kimarekani laki 1
Sasa hawa waliingilia leseni za wengine na kukiuka leseni zao na walivyoambiwa walienda Mahakamani, kwa vile wizara, TCRA na mamlaka nyingine zinaheshimu utawala wa sheria ziliwaacha.
Asema "Hivyo kwa miaka kama mitatu hivi tunawaangalia tu ambapo ingekuwa nchi nyingine wangepelekwa mahakamani"
Mahakama iliwaambia kuwa wameenda sehemu sio na kuwataka waende kwenye tribunal of competition kama sheria itakavyo ambapo huko walishindwa kesi. Waliposhindwa kesi hiyo sasa ndipo walipoambiwa waondoe maudhui hayo kama leseni zao zinavyotaka
"Baada ya kuziondoa ndio wanaanza kupia kelele kwamba channel zimeondolewa bila kusema ukweli ulivyo. Ting, Continental, Digitek na Startimes alichukuwa hizi channel na kuzirusha bure ambapo wao walisema kuwa hela yao wataipata kwenye matangazo tu. Ila watu naona wang'angania na kulilia tu Azam, DSTV na Zuku" amesema Mwakyembe
Maudhui ya kitanzania yanatakiwa kuwa bure sio kwa kuwa tumependa yawe bure ila ni kwa mujibu wa kikatiba ambapo mwananchi ana haki ya kupata habari kitu ambacho sio kipya bali ni toka uhuru. Na wanaorusha maudhui ya ndani lazima mitambo yao iwe imesimikwa ndani ya nchi yenyewe na ndio utaratibu duniani kote
Digitek, Ting, Startimes na Continental mitambo yao ipo hapa nchini ila Azam mitambo yao haipo hapa nchini ipo Mauritius lakini sasa hawasemi ukweli. Kwa namna hiyo serikali haina uhuru wa kuambia Azam wabadili chochote kama mambo yakiharibika mpaka wao wasiliane na mamlaka za huko mitambo ilipo ili zikubali au zikatae.....sasa huwezi kuendesha nchi namna hiyo. DSTV wapo Dubai na Zuku wapo Kenya
Waziri Mwakyembe amesema kuwa tamthilia, mpira na vitu kama hivyo wanaweza kuendelea kuonesha kwa kuwa vipo kwenye leseni zao ila kile ambavyo Mtanzania lazima akipate; Taarifa ya Habari na Matukio muhimu mengine ikiwa ni hotuba za viongozi na mengine hatakiwi kulipia
Ameongeza kuwa "Kwa sasa mimi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali tunaangalia ni kiasi gani walipata na sakata hili likiisha lazima warejeshe fedha hizo"