BoT, toeni matangazo kabla ya taarifa ya habari kuhusu adhabu za kukiuka Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha na kanuni zake ya mwaka 2018

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Muda mfupi uliopita kupitia kipindi cha "Ijue BOT" kinachorushwa na Azam tv, nimemsikia Afisa Mwandamizi wa BOT, Bwana Deogratias Mnyamani akitoa maelezo kuhusu Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 na kanuni zake ya mwaka 2019. Katika maelezo yake akihojwa na Mtangazi wa kipindi hicho, Bwana Mnyamani ameeleza mambo kadhaa ambayo naamini watu wengi hawayajui kuanzia watoa huduma mpaka walaji.

Kwa mfano, Bwana Mnyamani amesema kutoa kadi ya benki kwa mtoa huduma kama dhamana ni kosa kwa mkopeshaji na mkopaji. Swali ni je, watu wangapi wanafahamu hivi? Baadhi ya watoa huduma(Wakopeshaji) wanaweza kuwa wanajua, ila Walaji kwa maana ya Wakopijaji, wanajua kutoa kadi ni kosa kisheria?

Vile vile, Afisa huyu ameeleza adhabu kwa wanaofanya biashara ya kukopesha bila kuwa na leseni ambapo amesema adhabu ni faini kati ya shilingi milioni 20 mpaka milioni 100 au kifungo cha miaka 2 mpaka 5 jela au vyote kwa pamoja. Swali ni je, watu wanaofanya hii biashara kienyeji wanafahamu kuhusu adhabu hizi?

Kwa kifupi, Bwana Deogratias kaongea mengi kuhusu hii sheria na kanuni zake na amesema walikuwa kwenye kipindi cha kutoa elimu kuhusu hii sheria na kanuni zake na sasa wanajipanga kuanza kuisimamia.

Ukweli ni kwamba, watu wengi wanafahamu uwepo wa hii sheria, lakini kama ilivyo kwa sheria zingine, wengi hawajui nini kimo katika hii sheria na kanuni zake na zaidi watu wengi wanaona hii sheria ipo tu lakini serikali haiisimamii na ndio maana inapuuzwa sana humu mitaani kwa watu kufanya hii biashara pasipo kuwa na leseni, huku wenye leseni, wakiifanya kwa kupuuza hii sheria ya mwaka 2018 na kanuni zake za mwaka 2019.

Hivyo, wakati serikali kupitia BOT wakijipanga kuanza kusimamia kwa vitendo utekelezaji wa sheria hii kama alivyosema Afisa huyu wa BOT, nashauri BOT watoe matangaza kabla ya taarifa ya habari kwenye television na redio ili watu watambue kuwa ile "grace period" imepita na sasa utekelezaji unaanza. Mbali na kutoa matangaza kwenye vyombo vya habari, pia watumie mitandao ya kijamii kueleza umma kuhusu hii sheria na kukumbusha umma kuwa sasa usimamizi na utekelezaji wa hii sheria kwa vitendo uko mbiona kuanza.

Pia, kwenye matangazo haya, watamke adhabu anazoweza kupata mtu kwa kuvunja hii sheria na kanuni zake. Hii itasaidia ku-create awareness kwa umma na kufanya watu waone serikali sasa iko serious kuhusu hii sheria na itsaidia sana kupunguza manyanyaso wanayopata wananchi hasa kutoka kwa wale wanaofanya hii biashara pasiokuwa na leseni, na wale wenye leseni kuzingatia mashariti ya leseni walizopewa.
 
Sawa Sawa. Vilevile waangalie ubunifu unaotokana na njia hizi zisizo halali.....Kujengea sheria around hizi biashara za mtaani badala ya kujenga sheria zinazodumaza ubunifu na kukandamiza wazawa au wafanyabiashara wadogo wasio kuwa na mitaji mikubwa kama za mabenki n.k ....wanaweza wakawa wanakusanya viji fee huko na kuongeza pato la pato la ukusanyaji Kodi baadae.


"Chupi Mkononi" Vs Sheria Kitabuni.
 
Sawa Sawa. Vilevile waangalie ubunifu unaotokana na njia hizi zisizo halali.....Kujengea sheria around hizi biashara za mtaani badala ya kujenga sheria zinazodumaza ubunifu na kukandamiza wazawa au wafanyabiashara wadogo wasio kuwa na mitaji mikubwa kama za mabenki n.k ....wanaweza wakawa wanakusanya viji fee huko na kuongeza pato la pato la ukusanyaji Kodi baadae.


"Chupi Mkononi" Vs Sheria Kitabuni.
Ila sio kutoza watu masikini au wanaopambana na ugumu wa maisha riba ya asilimia 30, 40 mpaka 50. Mfano, umekopa shilingi 1,000,000/= ndani ya mwezi mmoja unarudisha riba ya shilingi 300,000/=. Je, hii ni sawa?

Niambie biashara gani ya mtaji wa shilingi 1,000,000/= inaweza kukupa faida ya shilingi 300,000 tu ndani ya siku 30?

Inawezekana zipo ila hii riba ni kufanya watu hasa wajasiliamali huku mitaani kuwa masikini, hivyo BOT wanapaswa kutazama riba hizi za kinyonyaji.

Shida na matatizo ya watu haviwezi kugeuzwa mtaji wa kutokea kimaisha.Hata vitabu vya dini vinakataza riba.
 
Ila sio kutoza watu masikini au wanaopambana na ugumu wa maisha kwa kutoza riba ya asilimia 30, 40 mpaka 50. Mfano, umekopa 1000,000/= ndani ya mwezi mmoja unarudisha riba ya shilingi 300,00o/=. Je, hii ni sawa?

Niambie biashara gani ya mtaji wa shilingi 1000,000/= inaweza kukupa faida ya shilingi 300,000 tu ndani ya siku 30?

Inawezekana zipo ila hii riba ni kufanya watu hasa wajasiliamali huku mitaani kuwa masikini, hivyo BOT wanapaswa kutazama riba hizi za kinyonyaji

.

Shida na matatizo ya watu haviwezi kugeuzwa mtaji wa kutokea kimaisha.Hata vitabu vya dini vinakataza riba.
Kiunagaubaga, hii hoja, imenikumbusha Mh. Daktari Raisi Amri Jeshi Mkuu Chief Mama alipouliza, (rhetorically)'mbona tunavaa suti kutoka nje?' kwa mlolongo huo mbona tunaegemea kufanya biashara za Kibepari halafu tukatae madhara yake? Manake kuvaa Suti tayari tumeshajivua maadili yetu, vivyohivyo kuwekea tozo au riba na vyote vinavyofanana na hiyo ni kujivua 'Utu' ambayo naona ndio tafsiri sahihi kwangu ya ulichokisema""
Shida na matatizo ya watu haviwezi kugeuzwa mtaj
moja ya mbinu za kibepari za Biashara ni lazima, yaani ni lazima uondoe 'utu' kwenye mahesabu yako ili ufanikiwe kama mfanyabiashara, uwe mkubwa au mdogo.

Hizi ni Sheria zilizojengwa na kuasisiwa na watu wasio kuwa na mitazamo wala fikra ya Muafrika au niseme hapa Sheria zilizojengwa kwa kupuuza Watu wenye matatizo na shida. Yaani madai yao ni kuwa watu hawa ni high risk(wasiokuwa na uwezo wa kurudisha mikopo) na hivyo umuhimu wa kuweka riba juu...haya na mengine ni kwasababu ya maadili, fikra na tamaduni walizokuwa nazo watunga wa sheria hizo kukosa 'utu' ndani ya mioyo yao,
ambazo, sisi tuna copy na kupaste
 
Back
Top Bottom