Waziri Mwakyembe amebadili gia angani?

Waziri Mwakyembe amebadili gia angani?

Nyerere alituasa na kutuhamasisha kwamba 'SIASA NI KILIMO', tena ni azimio la Iringa mwaka 1972. Kwa hiyo yeye Mwakyembe hataki KILIMO na kama ni hivyo Mwakyembe hawataki watanzania kwa asilimia 80%. Maana tunaambiwa 80% ya watanzania ni wakulima.
 
Hivi elimu yote aliyonayo mwakyembe hawezi kuendesha maisha nje ya uwaziri mpaka afikie hatua ya kufanya siasa zenye kumdhalilisha kiasi hiki!!? Hivi kuna faida gani ya kuelimika ikiwa msomi kama huyu anakubali vitu ambavyo hata asiyesoma hakubaliani navyo!!?
 
Lilipoibuka sakata la Ney wa Mitego na wimbo wake wa 'Wapo', Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe alijitokeza na kufanya mambo mawili. Mosi, aliondoa zuio la BASATA la kuzuia wimbo huo kutopigwa redioni na runingani. Pia, alimwalika na kukutana na Ney wa Mitego katika Ofisi za Wizara yake huko Dodoma. Wakafanya na mazungumzo.

Kimantiki, wimbo wa 'Wapo' una mambo ya kisiasa. Unaongelea mambo mbalimbali ya kisiasa katika minajiri ya kukosoa na kadhalika. Ni wimbo huo ndio Waziri Mwakyembe aliufungulia na kufanya mazungumzo na mwimbaji wake. Tena, alitaka wimbo huo uboreshwe na kubeba na maudhui ya wala rushwa, wakwepa kodi na kadhalika.

Jana, alipokuwa akijibu swali na Mbunge wa Mikumi, Mhe. Joseph Haule (Prof. J-CHADEMA), Waziri Mwakyembe amewaasa wanamuziki waache kuimba siasa kwakuwa wanaweza 'kuishia kubaya'. Ndiyo kusema, Waziri Mwakyembe amepiga marufuku wanamuziki wa Tanzania kuimba kuhusu siasa. Anataka waimbe mambo mengineyo.

Kadiri ya uelewa wangu na kwa jinsi ninavyofuatilia muziki, kuna mambo mawili makubwa ya kuyaimbia kwenye muziki. La kwanza, ni siasa. Siasa ni maisha ya watu katika namna mbalimbali. Siasa ni maisha ya kila siku katika uzuri au ubaya wake. Hata Hayati Bob Marley aliyepata umaarufu mkubwa ulimwenguni aliimba siasa pia. Jambo la pili la kuimbia ni mapenzi.

Je, katika mtitiriko wa kauli na matendo ya Waziri Mwakyembe, Waziri amebadili gia angani?
Katumwa aseme hivyo, ili mkuu aje aitengue hiyo kauli kama alivyofanya kipindi kile cha bila vyeti vya kuzaliwa hakuna kufunga ndoa.
 
Lilipoibuka sakata la Ney wa Mitego na wimbo wake wa 'Wapo', Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe alijitokeza na kufanya mambo mawili. Mosi, aliondoa zuio la BASATA la kuzuia wimbo huo kutopigwa redioni na runingani. Pia, alimwalika na kukutana na Ney wa Mitego katika Ofisi za Wizara yake huko Dodoma. Wakafanya na mazungumzo.

Kimantiki, wimbo wa 'Wapo' una mambo ya kisiasa. Unaongelea mambo mbalimbali ya kisiasa katika minajiri ya kukosoa na kadhalika. Ni wimbo huo ndio Waziri Mwakyembe aliufungulia na kufanya mazungumzo na mwimbaji wake. Tena, alitaka wimbo huo uboreshwe na kubeba na maudhui ya wala rushwa, wakwepa kodi na kadhalika.

Jana, alipokuwa akijibu swali na Mbunge wa Mikumi, Mhe. Joseph Haule (Prof. J-CHADEMA), Waziri Mwakyembe amewaasa wanamuziki waache kuimba siasa kwakuwa wanaweza 'kuishia kubaya'. Ndiyo kusema, Waziri Mwakyembe amepiga marufuku wanamuziki wa Tanzania kuimba kuhusu siasa. Anataka waimbe mambo mengineyo.

Kadiri ya uelewa wangu na kwa jinsi ninavyofuatilia muziki, kuna mambo mawili makubwa ya kuyaimbia kwenye muziki. La kwanza, ni siasa. Siasa ni maisha ya watu katika namna mbalimbali. Siasa ni maisha ya kila siku katika uzuri au ubaya wake. Hata Hayati Bob Marley aliyepata umaarufu mkubwa ulimwenguni aliimba siasa pia. Jambo la pili la kuimbia ni mapenzi.

Je, katika mtitiriko wa kauli na matendo ya Waziri Mwakyembe, Waziri amebadili gia angani?

kipindi kile alikuwa anatafuta kikiiiii
 
Huwezi kuwa Waziri ambae juzi ulimsifia Nay na wimbo wake unaozumgumzia siasa halafu after few days unasema ni marufuku kwa wanamuziki kuimba siasa.

Unawatolea mfano Diamond na Ali Kiba kwamba wamefanikiwa kimuziki kwasababu hawaimbi siasa.
Umeshasahau nyie CCM mlivyomwimbisha diamond kwenye kampeni zenu na baadhi ya nyimbo zake akazi badili na kua mwelekeo wa siasa na hata juzi ametunga wimbo wenye mwelekeo wa kisiasa na cover la album kaweka picha ya Mwl Nyerere.

Waziri Hasara.
uzee unamsumbua,wenzake washastaafu na heshima zao lakin yeye ulafi wa madaraka ndio chachu ya yeye kuwepo hadi leo
 
wasanii wasipoingia kwenye siasa, Nchi itakuwa imepiga maendeleo sana.Ila wanatumika pote tu ingawa hata US tuliwaona wasanii wako upande wa mama Hilary ila kwetu wamezidi
Kila mmoja afanye kazi zake.
kazi zao ni kuimba, waimbe nini tuwaachie wao. Upande unaoongoza kuwatumia wanamuziki ni serikali na CCM. Tatizo wao wakiwatumia wanamuziki 30 sio tatizo ila upande fulani ukiwatumia wawili tu ni tatizo. Huku ni kutojiamini kwa kiwango cha PhD.
 
kama wanamuziki wakikatazwa kuimba nyimbo za maudhui ya siasa, CCM na serikali ndio itakayoathirika zaidi. Tunaona kwenye sherehe za serikali na mikutano ya kampeni ya CCM, bila kujaza wanamuziki haifani so katazo hili ni hasara kwao kuliko faida
 
wasanii wasipoingia kwenye siasa, Nchi itakuwa imepiga maendeleo sana.Ila wanatumika pote tu ingawa hata US tuliwaona wasanii wako upande wa mama Hilary ila kwetu wamezidi
Kila mmoja afanye kazi zake.

Wewe una akili halisi ama ya kugushi, kazi ya mwanamuziki ni kuimba anachoona kina maslahi kwake! Tatizo ni kwamba watu hawapendi kusikia jinsi upande wa pili unavyowatathmini!!! Shame on you
 
Mimi ninafikiri tatizo halianzii kwa huyu ndugu Mwakinembe, bali ni upotoshwaji na ukengeushi tena wa makusudi wa dhana nzima ya SIASA ambao umeasisiwa na mkuu wa kaya. Kuna haja ya wanazuoni na wananchi wa Tanzania kuwa na mjadala uliomakinika kuhusu dhana ya SIASA na tukubaliane 'SIASA' ni nini? Mkuu wa kaya amepiga marufuku vyama vya siasa kufanya 'siasa' hadi 2020 lakini tunaona Chama cha Mapinduzi na yeye pia kwa kofia ya Rais na Mwenyekiti wanafanya 'siasa' kama kawa! Sasa na ndugu Mwakiembe naye anakuja na fikira hizo hizo kuwa wanasanii wasiimbe 'siasa' (pengine naye anamaanisha hadi 2020!).
 
Lilipoibuka sakata la Ney wa Mitego na wimbo wake wa 'Wapo', Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dr. Harrison Mwakyembe alijitokeza na kufanya mambo mawili. Mosi, aliondoa zuio la BASATA la kuzuia wimbo huo kutopigwa redioni na runingani. Pia, alimwalika na kukutana na Ney wa Mitego katika Ofisi za Wizara yake huko Dodoma. Wakafanya na mazungumzo.

Kimantiki, wimbo wa 'Wapo' una mambo ya kisiasa. Unaongelea mambo mbalimbali ya kisiasa katika minajiri ya kukosoa na kadhalika. Ni wimbo huo ndio Waziri Mwakyembe aliufungulia na kufanya mazungumzo na mwimbaji wake. Tena, alitaka wimbo huo uboreshwe na kubeba na maudhui ya wala rushwa, wakwepa kodi na kadhalika.

Jana, alipokuwa akijibu swali na Mbunge wa Mikumi, Mhe. Joseph Haule (Prof. J-CHADEMA), Waziri Mwakyembe amewaasa wanamuziki waache kuimba siasa kwakuwa wanaweza 'kuishia kubaya'. Ndiyo kusema, Waziri Mwakyembe amepiga marufuku wanamuziki wa Tanzania kuimba kuhusu siasa. Anataka waimbe mambo mengineyo.

Kadiri ya uelewa wangu na kwa jinsi ninavyofuatilia muziki, kuna mambo mawili makubwa ya kuyaimbia kwenye muziki. La kwanza, ni siasa. Siasa ni maisha ya watu katika namna mbalimbali. Siasa ni maisha ya kila siku katika uzuri au ubaya wake. Hata Hayati Bob Marley aliyepata umaarufu mkubwa ulimwenguni aliimba siasa pia. Jambo la pili la kuimbia ni mapenzi.

Je, katika mtitiriko wa kauli na matendo ya Waziri Mwakyembe, Waziri amebadili gia angani?
Maana nzima ya kile anachokisema Mh Mwakyembe unakipata kupitia mifano yake ya wanamuziki aliowataja. Nyimbo za kisiasa alizozikataza ni zile zenye kuibua mgogoro kati ya serikali na mwanamuziki. Hapa alitoa mfano wa Fela Ramson Anikulapo Kuti wa Nigeria kuimba nyimbo za kushambulia wanasiasa zilimfanya afe kama chokolaa.
Kwa yeyote mwenye akili, sijui hapa nikikujumisha nitakuwa nimekosea,anafahamu kuwa Mh Mwakyembe hajazuia Mwanamuziki kuimba nyimbo za kuumpa shime,kumuasa na kumkumbusha mwanasiasa,chama na wananchi juu ya mambo mbalimbali yanayoendelea katika jamii bila nia ya kutweza.
 
Back
Top Bottom