Waziri Mulugo azidi kuandamwa

Waziri Mulugo azidi kuandamwa

Jamani WanaJF.....what is the way foward juu ya hili?
mbona tunaendeleza mijadala bila kuchukua hatua? Jamani walio karibu na Raisi Kikwete...... this is urgent please amweleze watu wa aina hii waondoke kwenye system
 
Mbona wewe tayari upo katika kundi hilo la Mulugo?

......dogo huu mwaka mpya 2013 tuuanze vyema.......acha matusi.......Ukiwa hujui halafu hujijui kuwa hujui matokeo yake ndio kama unavyofanya hivi sasa.........
 
Hii ni kazi ya waziri wa elimu kivuli kuweka wazi mafisadi wa elimu hasa waliojipachika elimu wasiyostahili na kupata vyeo ambavyo hawana uwezo navyo hivyo kuwanyima nafasi wasomi halisi.

Lissu kaanza na majaji feki, Zitto kakomaa kwenya madini, Mdee kakomaa kwenye ardhi sasa tunataka waziri kivuli wa elimu nae ahoji elimu ya mawaziri wa elimu kwani ndiko kwenye uozo wote.

Watoto wanafeli na wengine kutojua kusoma na kuandika kabisa tunaambiwa ufaulu umeongezeka baada ya kushusha alama na wanachaguliwa kuingia kidato cha kwanza! Eti sasa walimu wa sekondari ndio waanze kuwafundisha watoto wa kidato cha kwanza kusoma, kuhesabu na kuandika.

Kuna haja pia ya kuwachunguza viongozi wote wenye digrii za Open University kwani wengi wanakitumia chuo hicho kuficha vibaya na kujinyakulia digrii wasizostahili. Wengi ukiwasikiliza ndio utagundua hata mwanafunzi wa kidato cha pili ana nafuu!
 
Ngoja tamtumia Wambura Mtani wa RFA ailushe Habari hii ktk pindi la JEE HUO NI UUNGWANA?
 
......dogo huu mwaka mpya 2013 tuuanze vyema.......acha matusi.......Ukiwa hujui halafu hujijui kuwa hujui matokeo yake ndio kama unavyofanya hivi sasa.........

Hustahili kuendelea kujibiwa!!
 
Anaeleza kuwa tatizo la Tanzania sio uzalishaji (kilimo cha mazao ya chakula) bali tatizo ni masoko. Ni nchi gani iliyowahi kuzalisha ikakosa masoko katika dunia ya leo?
.
Hapa na mimi sijakuelewa? Umewahi kufika Rukwa na Mpanda ukaona mazao yanaoza? Serikali ilinunua mahindi kule ikayakimbia! Soko halipo kule na la mbali unalifikiaje bila barabara? Na pia usimguse Sospeter Muhongo, ana vyeti na ameelimika waulize Germany tena ilikoanza shule walimpa PhD. Google kazi zake za jiolojia worldwide utaamua mwenyewe. Muhongo ni tofauti na vilaza wengi wa CCM[/QUOTE]

Tatizo siyo vyeti, tatizo ni ccm kwani ukishakuwa ccm bac vyeti vyako vyote unaficha tumboni na unaanza kufikiria na kufanya mambo kwa kutumia masaburi. So huenda Prof. naye (ambaye namkubali sana ki-academic yuko vema) ameanza kuficha vyeti vyake na kufikiria kimasaburimasburi.
 
Tuanzie na kaburi la marehemu Philip Mulugo kama kweli lipo ndio tutarejea mezani kujadili maana ndugu zake watakuwa wanaumia wakisikia jina la ndugu yao likitamba kwenye media ilhali wakijua ndugu yao alishatangulia mbele za haki zamani hizo!!

Aisee, this issue is now getting very very serious.

 

na Angelica Sullusi, Mbeya

SIKU chache baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kumtolea uvivu Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, akidai ana elemu ya kuunga unga, sakata hilo limeendelea kuibua mambo mapya.

Mbilinyi maarufu kama Sugu, alidai kuwa Mulugo hawezi kumbabaisha kwa vile ameunga elimu akiwa amesoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyeitwa Amim.

Alisema kuwa anamfahamu sana naibu waziri huyo kwa vile alisoma naye sekondari ya Mbeya Day akiwa anamtangulia madarasa mawili, lakini wakati huo alikuwa akijulikana kama Amim si Philipo Mulugo.

Wakati Mulugo akiwa amejitetea kwa madai kuwa mwenye shaka na wasiwasi wa elimu yake aende akatazame rekodi zake Chuo Kikuu Huria, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), naye ameibua tuhuma mpya dhidi yake.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara juzi mjini Mbeya eneo la Sido Mwanjelwa, Msigwa alisema kuwa si jambo la kushangaza kwa Mulugo kushindwa kuelewa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulitokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alisema kuwa Mulugo aliwahi pia kuchemka bungeni na kuwekwa kwenye kumbukumbu za Bunge mambo ya ajabu.
“Jamani katika mfumo wa elimu kuna vitu vinaitwa ‘K’ tatu ambazo ni
Kusoma, Kuandika na Kuhesabu, lakini yeye alitueleza kuwa ‘K’ hizi zinatafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza kwa ‘R’ tatu yaani Reading, Writing and Arthematic, kitu ambacho si kweli,” alisema.
Mchungaji Msigwa aliongeza kuwa Mulugo alipewa unaibu waziri kwa fadhila na kwamba ni bora akanyamaza kabisa na kuamua kufanya kazi ya kuwatetea wananchi jimboni kwake Songwe juu ya mikataba mibovu wanayoingia ya madini.



Madai ya Sugu na Msigwa juu ya Mulugo yameibuliwa baada ya naibu waziri huyo kusema kuwa CCM itayakomboa majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani humo likiwemo pia la Mbeya Mjini.

Awali akizungumza katika mkutano huo, Sugu alisema hana sababu ya kuendelea kumjibu Mulugo kwa kuwa tayari wananchi wa Mbeya wamekwishakumjibu kwa kujitokeza kwa wingi kumsikiliza mbunge wao tofauti na ilivyokuwa katika mkutano wa CCM aliohutubia naibu huyo.

“Hivi tu mlivyojitokeza wengi mnanipa faraja kuwa tayari Mulugo ujumbe umemfikia sina sababu ya kuendelea kusema kitu, nawashukuru sana Wanambeya wenzangu kwa kuniunga mkono.

source: Tanzaniadaima

Hapo kwenye red naomba kumtetea. Tafsiri iko hivyo na mimi sijaona kosa lake hapa. Mwalimu yeyote pia angesema hivi. Labda hawa waheshimiwa wanaosema Mulugo watupe tafsiri yao.


 
Mulugo anaumbuka kwa sababu ya kiherehere chake. Ninafahamu wapo mawaziri wengi sana ambao hawana kitu kichwani ila tofauti yao na Mulugo ni kuwa wao wanaficha ujinga wao kwa kukaa kimya. Mfano ni Shukuru kawambwa ambaye ni bosi wa Mulugo. Mwingine atakayeumbuka muda si mrefu ni Sospeter Muhongo, jamaa anajidai much know vibaya sana ila hakuna la maana analoongea.

Ha ha huyu Sosy umemuona mweupe sana anatumia nguvu kuhalallisha ujinga hii wizara lazima itampiga chini.
 

na Angelica Sullusi, Mbeya

SIKU chache baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kumtolea uvivu Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, akidai ana elemu ya kuunga unga, sakata hilo limeendelea kuibua mambo mapya.

Mbilinyi maarufu kama Sugu, alidai kuwa Mulugo hawezi kumbabaisha kwa vile ameunga elimu akiwa amesoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyeitwa Amim.

Alisema kuwa anamfahamu sana naibu waziri huyo kwa vile alisoma naye sekondari ya Mbeya Day akiwa anamtangulia madarasa mawili, lakini wakati huo alikuwa akijulikana kama Amim si Philipo Mulugo.

Wakati Mulugo akiwa amejitetea kwa madai kuwa mwenye shaka na wasiwasi wa elimu yake aende akatazame rekodi zake Chuo Kikuu Huria, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), naye ameibua tuhuma mpya dhidi yake.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara juzi mjini Mbeya eneo la Sido Mwanjelwa, Msigwa alisema kuwa si jambo la kushangaza kwa Mulugo kushindwa kuelewa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulitokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Alisema kuwa Mulugo aliwahi pia kuchemka bungeni na kuwekwa kwenye kumbukumbu za Bunge mambo ya ajabu.
“Jamani katika mfumo wa elimu kuna vitu vinaitwa ‘K’ tatu ambazo ni Kusoma, Kuandika na Kuhesabu, lakini yeye alitueleza kuwa ‘K’ hizi zinatafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza kwa ‘R’ tatu yaani Reading, Writing and Arthematic, kitu ambacho si kweli,” alisema.
Mchungaji Msigwa aliongeza kuwa Mulugo alipewa unaibu waziri kwa fadhila na kwamba ni bora akanyamaza kabisa na kuamua kufanya kazi ya kuwatetea wananchi jimboni kwake Songwe juu ya mikataba mibovu wanayoingia ya madini.

Madai ya Sugu na Msigwa juu ya Mulugo yameibuliwa baada ya naibu waziri huyo kusema kuwa CCM itayakomboa majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani humo likiwemo pia la Mbeya Mjini.

Awali akizungumza katika mkutano huo, Sugu alisema hana sababu ya kuendelea kumjibu Mulugo kwa kuwa tayari wananchi wa Mbeya wamekwishakumjibu kwa kujitokeza kwa wingi kumsikiliza mbunge wao tofauti na ilivyokuwa katika mkutano wa CCM aliohutubia naibu huyo.

“Hivi tu mlivyojitokeza wengi mnanipa faraja kuwa tayari Mulugo ujumbe umemfikia sina sababu ya kuendelea kusema kitu, nawashukuru sana Wanambeya wenzangu kwa kuniunga mkono.

source: Tanzaniadaima

Ni raha sana kuwaona wanasiasa wawili au zaidi wakilumbana, hofu yangu isije ikawa ni janja yao ya kutaka kutuondoa katika focus ya maendeleo ili tusifanye appraisal ya kazi zao. Lakini pia unachokisikia kutoka kwao sio kweli kwamba siku zote kinawakilisha picha halisi. Sijajua kama ni makosa ya mwandishi au gazeti ama imetoka kwa wanasiasa kama ilivyo, ila kuna mambo yasiyo sahihi katika taarifa.
1. Si kweli kwamba sugu alikuwa mbele madarasa mawili kwa Mulugo. Mulugo alipokuwa kidato cha kwanza sugu alikuwa kidato cha pili.

2. Hawa watu hawajasoma pamoja kwa miaka yote,wamesoma pamoja kwa kipindi kisichozidi mwaka kwa kuwa Sugu alifukuzwa shule kwa kuwanyanyasa wanafunzi wa hostel wa kidato cha kwanza.

Ningekuwa na uwezo wa kukutana nao wote wawili ningewashauri wayaache malumbano yatawadestroy wote wawili. Kwa kuwa kwa wote wawili changes katika maisha yao zote hazina mizengwe na wote wawili wanaujua ukweli. Mfano; Mulugo alikuwa muislam kwa jina la Hamimu, akabadili kuwa Philipo. Sugu kwakuwa kosa alilofukuziwa halikuthibitishwa beyond doubt akapata uhamisho kwenda shule nyingine (hakukuwa na favour yeyote katika uhamisho wake). na wote wawili wanatumia fact hizi kulumbana.

Malumbano yao yanachelewesha maendeleo ya majimbo yao, hayatufaidishi sisi hata kidogo zaidi ya kutupotezea muda
 
Asante kwa kutuhabarisha ila huyu mulugo anakihelehele sana alafu kama kilaza fulani hivi!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Si Mulugo tu
issue uchaguzi waja kunajamaa baba wa Mafisadi Lowasa ataliangamiza taifa bora hata huyo Mulugo. Si mtetei lakini Lowasa ni Hatari kuliko Umeme
 
Back
Top Bottom