Waziri Mulugo azidi kuandamwa

Waziri Mulugo azidi kuandamwa

mhesimiwa kanusha kwa kuweka vyeti vyako

Hawezi kukanusha kwa kuweka vyeti kwani cha kidato cha nne anaitwa Amim Augustino lakini cha Open University anaitwa Philipo Mulugo, mbona hata hakanushi anakimbilia kueleza habari za OUT sisi tunataka tuone trend yake tangu Primary
 
Hamim Augustino ana kazi!

Kweli kazi ipo kutoka Amim Agustino hadi Philipo Mulugo, naye baba Riz hata hatengui basi tumombe Brother K wa Futuhi atengue Alhamisi hii ni aibu kwa Rais na washauri wake Hisani hizi zitztumaliza hivi hakuna vetting kwa viongozi wakubwa kama hawa kabla ya kuteuliwa au ndo alichowahi kusema Lukuvi kuwa ikimpendeza Rais kuteua ni yeyote? Hakika tunalishwa sumu ya mamba
 
Nawaomba ndg zake na Mulugo aliyekufa wajitokeze au WALIKULA MULUNGULA?
 
Hawezi kukanusha kwa kuweka vyeti kwani cha kidato cha nne anaitwa Amim Augustino lakini cha Open University anaitwa Philipo Mulugo, mbona hata hakanushi anakimbilia kueleza habari za OUT sisi tunataka tuone trend yake tangu Primary

Mwenye Cv yake ebu aiteremshe apa...
 
......na nimesikia anaweza kuwa mgeni mwalikwa kwenye ''This Week in Perspective'' ya Simbei TBC, yatawashuka mnaodhani waziri hawezi tema yai tupu
 
He! Kumbe Naibu Waziri wa kuporomoka kwa Elimu na yeye ni chakachua. Hapo unategemea nini? Kumbe hawa watu ambao huwa wanapenda publicity na media covarage wana mengi waliyoyaficha. Ajabu mtu ulimi unateleza badala ya kusema Zanzibar unasema Zimbabwe, utashindwa kugundua kama umekosea na kuwaomba radhi hadhira? Hapana Mulugo ana tatizo kubwa zaidi ya tunavohisi au hata anavojifahamu mwenyewe. Halafu speech unayokwenda present kimataifa haiwezekani ikasomwa au kueditiwa na mtu mmoja au mara moja tu. Kitu kinachoandaliwa kimataifa kinapaswa kuwa na hadhi ya kimataifa, kama Obama anaweza kufanya rehearse ya kitu atakacho present, sembuse Amim Augustino?
 
............Mwingine atakayeumbuka muda si mrefu ni Sospeter Muhongo, jamaa anajidai much know vibaya sana ila hakuna la maana analoongea.

..... Kama unamuunga mkono unanipa sababu za kukuhofia na wewe pia.

..wewe tutakuweka kwenye kundi la Mulugo......muda si mrefu....ukiendelea na hiyo nadharia yako kuhusu Prof
 
Anaeleza kuwa tatizo la Tanzania sio uzalishaji (kilimo cha mazao ya chakula) bali tatizo ni masoko. Ni nchi gani iliyowahi kuzalisha ikakosa masoko katika dunia ya leo?.[/QUOTE]
Hapa na mimi sijakuelewa? Umewahi kufika Rukwa na Mpanda ukaona mazao yanaoza? Serikali ilinunua mahindi kule ikayakimbia! Soko halipo kule na la mbali unalifikiaje bila barabara? Na pia usimguse Sospeter Muhongo, ana vyeti na ameelimika waulize Germany tena ilikoanza shule walimpa PhD. Google kazi zake za jiolojia worldwide utaamua mwenyewe. Muhongo ni tofauti na vilaza wengi wa CCM
 
Siku zake zinahesabika atatuambia tu siku moja kama kweli kuna mgao wa umeme au hapana, atapewa options 2 tu? je kuna umeme au hapana?
sio kama anajifanya anajua..ni anajua na kichwa ile mbaya..mbona zitto anamkimbia?!?
 
Anaeleza kuwa tatizo la Tanzania sio uzalishaji (kilimo cha mazao ya chakula) bali tatizo ni masoko. Ni nchi gani iliyowahi kuzalisha ikakosa masoko katika dunia ya leo?.
Hapa na mimi sijakuelewa? Umewahi kufika Rukwa na Mpanda ukaona mazao yanaoza? Serikali ilinunua mahindi kule ikayakimbia! Soko halipo kule na la mbali unalifikiaje bila barabara? Na pia usimguse Sospeter Muhongo, ana vyeti na ameelimika waulize Germany tena ilikoanza shule walimpa PhD. Google kazi zake za jiolojia worldwide utaamua mwenyewe. Muhongo ni tofauti na vilaza wengi wa CCM[/QUOTE]

 
Hivi upo Tz hii au hapana? Hivi unaona vizuri mazao kuoza huko Rukwa au sehemu ingine ya muungano? wakati mahindi hayo hayo yapo Sirari, Mtukura na Namanga yanaoza yamezuiwa yasiende kuuzwa nchi jirani?
Hivi usomi wa Muhongo unatusaidia nini sisi, au ni sawa na jirani yako wa hapo kijijini kwenu ana gari halafu unajisifia kuwa hata sisi kijijini kwetu tuna gari, nikuulize:hivi asilimia ya mapato yetu kwenye madini imeongezeka? hivi wachimbaji wetu wa madini wana facility za kuwasaidia wawekeze?hivi ni kwa nini umeme unakatikakatika hovyo? [/SIZE][/FONT]

Anaeleza kuwa tatizo la Tanzania sio uzalishaji (kilimo cha mazao ya chakula) bali tatizo ni masoko. Ni nchi gani iliyowahi kuzalisha ikakosa masoko katika dunia ya leo?.
Hapa na mimi sijakuelewa? Umewahi kufika Rukwa na Mpanda ukaona mazao yanaoza? Serikali ilinunua mahindi kule ikayakimbia! Soko halipo kule na la mbali unalifikiaje bila barabara? Na pia usimguse Sospeter Muhongo, ana vyeti na ameelimika waulize Germany tena ilikoanza shule walimpa PhD. Google kazi zake za jiolojia worldwide utaamua mwenyewe. Muhongo ni tofauti na vilaza wengi wa CCM[/QUOTE]
 
Amim tafadhali usikubali kudhalilishwa hivyo. Jitokeze jamvini ujisafishe kwa kuelezea ukweli wa tuhuma wanazokubambikia. Kitendo cha wewe kuaminiwa na kuteuliwa na J.K. kinatosha. Chezea Mulugo wee. Karibu jamvini ufanye mavitu yako.:target:
 
Tuanzie na kaburi la marehemu Philip Mulugo kama kweli lipo ndio tutarejea mezani kujadili maana ndugu zake watakuwa wanaumia wakisikia jina la ndugu yao likitamba kwenye media ilhali wakijua ndugu yao alishatangulia mbele za haki zamani hizo!!

Inabidi kuwe na msiba mpya tena wa kuzika upya jina hilo ili lisije likafufuka tena;na wenye tabia kama hiyo wote watafutwe na Kuadhibiwa ili isirudiwe tena.
 
hahahahahaha na Lowasa afuatiliwe Jamani, mi nawasiwasi nae sana.

Mawaziri kadhaa, makamanda wa polisi wastaafu ndiyo wafanyabiashara wakubwa wa maunga.
Ni hapo TZ itakapokuwa na rais muuza unga. Usishangae mgombea kupitia ccm ni zungu kamili la unga.
 
Waziri Kihiyo anaongoza wizara ya elimu? tutegemee matunda mabovu
 
SIKU chache baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kumtolea uvivu Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, akidai ana elemu ya kuunga unga, sakata hilo limeendelea kuibua mambo mapya.
Mbilinyi maarufu kama Sugu, alidai kuwa Mulugo hawezi kumbabaisha kwa vile ameunga elimu akiwa amesoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyeitwa Amim.
Alisema kuwa anamfahamu sana naibu waziri huyo kwa vile alisoma naye sekondari ya Mbeya Day akiwa anamtangulia madarasa mawili, lakini wakati huo alikuwa akijulikana kama Amim si Philipo Mulugo.
Wakati Mulugo akiwa amejitetea kwa madai kuwa mwenye shaka na wasiwasi wa elimu yake aende akatazame rekodi zake Chuo Kikuu Huria, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), naye ameibua tuhuma mpya dhidi yake.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara juzi mjini Mbeya eneo la Sido Mwanjelwa, Msigwa alisema kuwa si jambo la kushangaza kwa Mulugo kushindwa kuelewa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulitokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Alisema kuwa Mulugo aliwahi pia kuchemka bungeni na kuwekwa kwenye kumbukumbu za Bunge mambo ya ajabu.
“Jamani katika mfumo wa elimu kuna vitu vinaitwa ‘K’ tatu ambazo ni Kusoma, Kuandika na Kuhesabu, lakini yeye alitueleza kuwa ‘K’ hizi zinatafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza kwa ‘R’ tatu yaani Reading, Writing and Arthematic, kitu ambacho si kweli,” alisema.
Mchungaji Msigwa aliongeza kuwa Mulugo alipewa unaibu waziri kwa fadhila na kwamba ni bora akanyamaza kabisa na kuamua kufanya kazi ya kuwatetea wananchi jimboni kwake Songwe juu ya mikataba mibovu wanayoingia ya madini.
Madai ya Sugu na Msigwa juu ya Mulugo yameibuliwa baada ya naibu waziri huyo kusema kuwa CCM itayakomboa majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani humo likiwemo pia la Mbeya Mjini.
Awali akizungumza katika mkutano huo, Sugu alisema hana sababu ya kuendelea kumjibu Mulugo kwa kuwa tayari wananchi wa Mbeya wamekwishakumjibu kwa kujitokeza kwa wingi kumsikiliza mbunge wao tofauti na ilivyokuwa katika mkutano wa CCM aliohutubia naibu huyo.
“Hivi tu mlivyojitokeza wengi mnanipa faraja kuwa tayari Mulugo ujumbe umemfikia sina sababu ya kuendelea kusema kitu, nawashukuru sana Wanambeya wenzangu kwa kuniunga mkono.



[TD="bgcolor: #ffffff"]
na Angelica Sullusi, Mbeya


[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"]
amka2.gif

[/TD]
source: Tanzaniadaima

Sasa nimeelewa tatizo liko wapi. Kuna mtu amesema baadhi ya mawaziri ni waziba nafasi. kwa staili hii kweli nafasi zimezibwa.
 
Ingekua ni enzi za Mwalimu Amim angechapwa viboko na kutimuliwa km mbwa. Angekua ni waziri wa nchi km china akaaibisha nchi yake kwa kile kiswanglish broken vile ukiacha hata hayo ya muungano wake na zimbabwe ANGEPOTEZWA kimyakimya coz China hawataki uzembe hasa na jina la nchi yao...Aombe mungu tu dhaifu dhaifu na nchi yetu ndo maana hata hakuandika risala kuomba msamaha na kujiuzulu!! Binafsi ningekua rais angeanza kunieleza alisoma wap?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
MULUGO, Philipo Hamimu Augustino
 
Do na hii chama bwana... Wanateseka kweli ukificha maovu yao unaongwa cheo basi waangalie na elimu ya anayeongwa hana uwezo????
 
Back
Top Bottom