Sumasuma
JF-Expert Member
- Jun 23, 2011
- 342
- 110
SIKU chache baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), kumtolea uvivu Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, akidai ana elemu ya kuunga unga, sakata hilo limeendelea kuibua mambo mapya.
Mbilinyi maarufu kama Sugu, alidai kuwa Mulugo hawezi kumbabaisha kwa vile ameunga elimu akiwa amesoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyeitwa Amim.
Alisema kuwa anamfahamu sana naibu waziri huyo kwa vile alisoma naye sekondari ya Mbeya Day akiwa anamtangulia madarasa mawili, lakini wakati huo alikuwa akijulikana kama Amim si Philipo Mulugo.
Wakati Mulugo akiwa amejitetea kwa madai kuwa mwenye shaka na wasiwasi wa elimu yake aende akatazame rekodi zake Chuo Kikuu Huria, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), naye ameibua tuhuma mpya dhidi yake.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara juzi mjini Mbeya eneo la Sido Mwanjelwa, Msigwa alisema kuwa si jambo la kushangaza kwa Mulugo kushindwa kuelewa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulitokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Alisema kuwa Mulugo aliwahi pia kuchemka bungeni na kuwekwa kwenye kumbukumbu za Bunge mambo ya ajabu.
"Jamani katika mfumo wa elimu kuna vitu vinaitwa ‘K' tatu ambazo ni Kusoma, Kuandika na Kuhesabu, lakini yeye alitueleza kuwa ‘K' hizi zinatafsiriwa kwa lugha ya Kiingereza kwa ‘R' tatu yaani Reading, Writing and Arthematic, kitu ambacho si kweli," alisema.
Mchungaji Msigwa aliongeza kuwa Mulugo alipewa unaibu waziri kwa fadhila na kwamba ni bora akanyamaza kabisa na kuamua kufanya kazi ya kuwatetea wananchi jimboni kwake Songwe juu ya mikataba mibovu wanayoingia ya madini.
Madai ya Sugu na Msigwa juu ya Mulugo yameibuliwa baada ya naibu waziri huyo kusema kuwa CCM itayakomboa majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani humo likiwemo pia la Mbeya Mjini.
Awali akizungumza katika mkutano huo, Sugu alisema hana sababu ya kuendelea kumjibu Mulugo kwa kuwa tayari wananchi wa Mbeya wamekwishakumjibu kwa kujitokeza kwa wingi kumsikiliza mbunge wao tofauti na ilivyokuwa katika mkutano wa CCM aliohutubia naibu huyo.
"Hivi tu mlivyojitokeza wengi mnanipa faraja kuwa tayari Mulugo ujumbe umemfikia sina sababu ya kuendelea kusema kitu, nawashukuru sana Wanambeya wenzangu kwa kuniunga mkono.
source: Tanzaniadaima