Waziri Mpango 'ameteleza', asamehewe

Waziri Mpango 'ameteleza', asamehewe

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Waziri Wa Fedha na Mipango., Dr. Phillip Mpango amelivuruga Bunge. Ni kama amesababisha vurugu zisizo na tija Bungeni. Ni baada ya 'kulitumia' Bunge kupiga kampeni kwa chama chake cha CCM kuelekea Uchaguzi Wa Serikali za Mitaa, Oktoba mwaka huu.

Kiukweli, Waziri Mpango amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali iliyosheheni matumaini makubwa kwa weledi na umakini mkubwa. Ameiwasilisha kwa kuelewekavyema na kwa umahiri mkubwa. Lakini, alipoingiza 'kampeni kwa CCM' aliteleza.

Alianza vyema kutaja sifa zinazofaa kuwepo kwa viongozi wetu na wanaotaka kuwa viongozi wetu. Sifa ya kwanza hadi ya tisa zilikuwa ni sifa za jumla na njema Sana. Ya kumi iliyoleta mtafaruku ilianza vyema kuwa atokane na chama chenye kupigania maslahi ya taifa. Kuitaja CCM ndiyo kuteleza kwenyewe.

Kimsingi, Waziri Mpango hakupaswa kulifanya Bunge kuwa jukwaa LA kampeni kwa CCM. Alisababisha kelele na vurugu zisizo na maana Bungeni. Bunge Si uwanja Wa kampeni Wa chama chochote! Aliteleza na asamehewe.
 
Kwa kitendo cha leo, naamnini Prof Assad alikuwa yupo sahihi kwa kauli yake ile.
Kwa maelezo yake mwenyewe Mpango hajatamka kama huyo mgombea awe ambaye anafuata Katiba ya nchi kwani nafikiri anaona ni kazi sana kwa wale wanaojiona nambari wani
 
Waziri Wa Fedha na Mipango., Dr. Phillip Mpango amelivuruga Bunge. Ni kama amesababisha vurugu zisizo na tija Bungeni. Ni baada ya 'kulitumia' Bunge kupiga kampeni kwa chama chake cha CCM kuelekea Uchaguzi Wa Serikali za Mitaa, Oktoba mwaka huu.

Kiukweli, Waziri Mpango amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali iliyosheheni matumaini makubwa kwa weledi na umakini mkubwa. Ameiwasilisha kwa kuelewekavyema na kwa umahiri mkubwa. Lakini, alipoingiza 'kampeni kwa CCM' aliteleza.

Alianza vyema kutaja sifa zinazofaa kuwepo kwa viongozi wetu na wanaotaka kuwa viongozi wetu. Sifa ya kwanza hadi ya tisa zilikuwa ni sifa za jumla na njema Sana. Ya kumi iliyoleta mtafaruku ilianza vyema kuwa atokane na chama chenye kupigania maslahi ya taifa. Kuitaja CCM ndiyo kuteleza kwenyewe.

Kimsingi, Waziri Mpango hakupaswa kulifanya Bunge kuwa jukwaa LA kampeni kwa CCM. Alisababisha kelele na vurugu zisizo na maana Bungeni. Bunge Si uwanja Wa kampeni Wa chama chochote! Aliteleza na asamehewe.

Ulitegemea asemeje wakati yeye ni mwana CCM? Ikumbukwe kwamba kila mbunge yupo bungeni kwa tiketi ya chama chake cha Siasa.

Isitoshe, katika kipindi cha utawala wa Rais Magufuli, imedhihirika wazi kwamba chama chenye kupigania maslahi ya taifa ni CCM, vingine ni SACCOS, vyama vya mifukoni au vina sura ya udini, ukabila na ukanda.
 
Zaidi ya miaka 40 ya hizi bajeti ni moja tu ya mzee Msuya iliyotanabaisha wazi kuwa 'kila mtu atabeba mzigo wake'. Wengi walimlaani kwa kusema haya lakini ndiye msema kweli pekee aliyewahi kuusema.
Mbali na hapo bujeti zote miaka yote utasikia "bajeti ya wanyonge" na kila mwaka maisha yanaendelea kuwa magumu zaidi ya mwaka unaotangulia. Angelikuwa serious angeeleza jinsi ya kumaliza deni la taifa kwa miaka 10 ijayo!
 
Ulitegemea asemeje wakati yeye ni mwana CCM? Ikumbukwe kwamba kila mbunge yupo bungeni kwa tiketi ya chama chake cha Siasa.

Isitoshe, katika kipindi cha utawala wa Rais Magufuli, imedhihirika wazi kwamba chama chenye kupigania maslahi ya taifa ni CCM, vingine ni SACCOS, vyama vya mifukoni au vina sura ya udini, ukabila na ukanda.
Ccm inapigania maslahi ya Taifa gani? Bora muwe mnakaa kimya!
 
Si kweli. Mpango hayupo bungeni kwa tiketi ya CCM.
Ulitegemea asemeje wakati yeye ni mwana CCM? Ikumbukwe kwamba kila mbunge yupo bungeni kwa tiketi ya chama chake cha Siasa.

Isitoshe, katika kipindi cha utawala wa Rais Magufuli, imedhihirika wazi kwamba chama chenye kupigania maslahi ya taifa ni CCM, vingine ni SACCOS, vyama vya mifukoni au vina sura ya udini, ukabila na ukanda.
 
Nikiwasikilizaga ma Dr na Ma prof wetu waliopewa shavu na jiwe huwa naishia kujisemea kwamba hakuna kitu kibaya duniani kama Njaa. Njaa inaondoa hekima, Njee inakata mshipa wa aibu , njaa inapoteza ufaham njaaa njaaa njaaa.
 
Waziri Wa Fedha na Mipango., Dr. Phillip Mpango amelivuruga Bunge. Ni kama amesababisha vurugu zisizo na tija Bungeni. Ni baada ya 'kulitumia' Bunge kupiga kampeni kwa chama chake cha CCM kuelekea Uchaguzi Wa Serikali za Mitaa, Oktoba mwaka huu.

Kiukweli, Waziri Mpango amewasilisha Bajeti Kuu ya Serikali iliyosheheni matumaini makubwa kwa weledi na umakini mkubwa. Ameiwasilisha kwa kuelewekavyema na kwa umahiri mkubwa. Lakini, alipoingiza 'kampeni kwa CCM' aliteleza.

Alianza vyema kutaja sifa zinazofaa kuwepo kwa viongozi wetu na wanaotaka kuwa viongozi wetu. Sifa ya kwanza hadi ya tisa zilikuwa ni sifa za jumla na njema Sana. Ya kumi iliyoleta mtafaruku ilianza vyema kuwa atokane na chama chenye kupigania maslahi ya taifa. Kuitaja CCM ndiyo kuteleza kwenyewe.

Kimsingi, Waziri Mpango hakupaswa kulifanya Bunge kuwa jukwaa LA kampeni kwa CCM. Alisababisha kelele na vurugu zisizo na maana Bungeni. Bunge Si uwanja Wa kampeni Wa chama chochote! Aliteleza na asamehewe.
Hakuteleza bali sehemu ya mkakati wa CCM kushinda uchaguzi kwa sababu zile Tisa zingine hakuna mwanachama wao yeyote anafit masharti hayo na kushinda.
 
Back
Top Bottom