PreGE2025 Waziri Mkuu Majaliwa: Reforms zimeimarisha hali ya demokrasia nchini

PreGE2025 Waziri Mkuu Majaliwa: Reforms zimeimarisha hali ya demokrasia nchini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema hali ya siasa na utekelezaji wa demokrasia nchini umeendelea kuimarika kutokana na maboresho ya mifumo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatano, Aprili 9, 2025, jijini Dodoma wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Amesema moja ya jitihada hizo ni pamoja na marekebisho ya sheria mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utawala wa kidemokrasia nchini.

“Miongoni mwa sheria hizo ni Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 1 ya Mwaka 2024, Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 2 ya Mwaka 2024, pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258,” amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa Serikali imeshakamilisha utungaji wa Kanuni za Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Aidha, Tume hiyo inaendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kusimamia na kuratibu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura.

 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema hali ya siasa na utekelezaji wa demokrasia nchini umeendelea kuimarika kutokana na maboresho ya mifumo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatano, Aprili 9, 2025, jijini Dodoma wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Amesema moja ya jitihada hizo ni pamoja na marekebisho ya sheria mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utawala wa kidemokrasia nchini.

“Miongoni mwa sheria hizo ni Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 1 ya Mwaka 2024, Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 2 ya Mwaka 2024, pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258,” amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa Serikali imeshakamilisha utungaji wa Kanuni za Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Aidha, Tume hiyo inaendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kusimamia na kuratibu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura.

Hiyo TUME HURU YA UCHAGUZI haipo kabisa kwa sababu watumishi wake ni CCM mojawapo ya vyama vinavyogambania nafasi za uongozi pia ni wateule wa Rais ambaye ni Mwenyekiti wa ccm.
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema hali ya siasa na utekelezaji wa demokrasia nchini umeendelea kuimarika kutokana na maboresho ya mifumo na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali.

Majaliwa ameyasema hayo leo Jumatano, Aprili 9, 2025, jijini Dodoma wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Amesema moja ya jitihada hizo ni pamoja na marekebisho ya sheria mbalimbali kwa lengo la kuimarisha utawala wa kidemokrasia nchini.

“Miongoni mwa sheria hizo ni Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 1 ya Mwaka 2024, Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 2 ya Mwaka 2024, pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa Sura ya 258,” amesema Majaliwa.

Ameongeza kuwa Serikali imeshakamilisha utungaji wa Kanuni za Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Aidha, Tume hiyo inaendelea na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kwa kusimamia na kuratibu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura.

Huyu mzee na Magu ndiyo waliharibu na style zao za kupita bila kupingwa, tutegemee reforms! sidhan😀
 
Aache soga nafasi ya kurudia wadhifa huo ni WA ngamia kwenye tundu la sindano.
 
Kwa umri wangu huu sijawahi kuona Kiongozi mkuu wa Serikali muongo kama huyu jamaa somuamini hata chembe.
 
Wana wa nchi hii tunaonekana wajinga Kwa hakika, eti Sheria ya tume huru ya uchaguzi!
 
Back
Top Bottom