Waziri Mkuu Majaliwa: Atakeyeonea waandishi wa habari kukiona

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,049
4,904
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, amesema yoyote atakaye waonea waandishi wa habari wakati wakitimiza majukumu yao watakiona, kwani serikali inawatambua na kuwathamini na isingependa kuona hata siku moja mwandishi anapata tatizo anapotimiza wajibu wake.

===

SERIKALI: HATUTAKUBALI KUONA MWANDISHI WA HABARI ANAONEWA

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali haitakubali kuona Mwandishi anapata uonevu popote kutokana na thamani ya mchango wanaotoa katika kuufahamisha Umma, Ameeleza hayo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Mkoani Morogoro.

Amesema, "Sio Sera ya Serikali kuonea Waandishi wa Habari. Serikali haitomvumilia mtu yeyote atakayemkwaza Mwandishi wa Habari akiwa katika kazi, na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Vilevile, amesema hatua kadhaa zinaendelea ili kuyafungulia Magazeti ya Mawio, Mseto, Tanzania Daima na Mwanahalisi akifafanua yalifungiwa Kisheria na Sheria hizo hizo zitafuata taratibu.
 
Hii ni kweli kweli. Mbona Kipindi cha Uongozi wa mwendazake Wanahabari walionja joto la jiwe bila hata mtu kutamka lolote.

However, kama Ndugai nae vimemrudia na anasema Watu wasionewe basi tunamwomba atende haki maana COVID - 19 Kuna dhuruma (Awatendee haki CHADEMA maana Majina ya COVID-19 ni Project yake na Mwendazake.

Ni Short Viongozi wote Serikalini Hawaamini bali wanacheza tu Ngoma ya Mama SSH. Mama ni Mpole mtu wa Haki na wataicheza Sana tu.
 
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali haitakubali kuona Mwandishi anapata uonevu popote kutokana na thamani ya mchango wanaotoa katika kuufahamisha Umma.

Ameeleza hayo wakati wa Ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Mkoani Morogoro.

Amesema, "Sio Sera ya Serikali kuonea Waandishi wa Habari. Serikali haitomvumilia mtu yeyote atakayemkwaza Mwandishi wa Habari akiwa katika kazi, na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

Vilevile, amesema hatua kadhaa zinaendelea ili kuyafungulia Magazeti ya Mawio, Mseto, Tanzania Daima na Mwanahalisi akifafanua yalifungiwa Kisheria na Sheria hizo hizo zitafuata taratibu.
 
Hahaha Mama kawanyoosha....na bado Waumini wa Udikta chalii mbende mbende
Hii ni kweli kweli....Mbona Kipindi cha Uongozi wa mwendazake Wanahabari walionja joto la jiwe bila hata mtu kutamka lolote. However, kama Ndugai nae vimemrudia na anasema Watu wasionewe basi tunamwomba atende haki maana COVID - 19 Kuna dhuruma ( Awatendee haki CHADEMA maana Majina ya COVID-19 ni Project yake na Mwendazake . Ni Short Viongozi wote Serikalini Hawaamini bali wanacheza tu Ngoma ya Mama SSH. Mama ni Mpole mtu wa Haki na wataicheza Sana tu...
Naomba anaye amini maneno ya huyu Mheshimiwa PM anyooshe kidole tafadhali! 🤭

Hivi amefufuka kutoka wapi huyu PM! Au ameshushwa tu kutoka mbinguni ndani ya hii miezi miwili iliyopita!
Kwa hiyo mlitaka aende against na boss wake 😃 et kisa analinda regacy ya mtu ambaye ni mfu na Hana uhai na helpless, aiseee ni mwehu Tu anayeweza kufanya mlichokuwa mnatarajia!
 
Vilevile, amesema hatua kadhaa zinaendelea ili kuyafungulia Magazeti ya Mawio, Mseto, Tanzania Daima na Mwanahalisi akifafanua yalifungiwa Kisheria na Sheria hizo hizo zitafuata taratibu
Aisee!!
 
RIP yule Mwandishi aliyelipuliwa mabomu pale Nyololo Mufindi na Kamanda akapandishwa cheo.
 
Back
Top Bottom