elivina shambuni
JF-Expert Member
- May 31, 2018
- 461
- 295
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Russian Railways, Alexander Misharin na kumweleza kuwa Tanzania inahitaji kuimarisha usafi ri wa ndani wa reli hasa katika majiji ya Dar es salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya na Tanga.
Amesema kampuni hiyo yenye uwezo mkubwa wa kujenga reli mpya, kukarabati, kutengeneza injini za treni na mabehewa na ukarabati wake inahitajika nchini ili kufanikisha mpango wa serikali wa kuimarisha reli za zamani za Tazara, ya Kati na kufungua ya Kaskazini inayounganisha mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Kilimanjaro na Arusha.
Waziri Mkuu alizungumza na mkurugenzi huo juzi mjini Sochi nchini Urusi, ambako alitumia fursa hiyo kuikaribisha Russian Railways kuwekeza nchini hususani katika sekta ya ujenzi, ufundi na mafunzo ikishirikiana na kampuni za Watanzania. Waziri Mkuu yuko nchini Urusi kuhudhuria mkutano baina ya Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka Mataifa ya Afrika na Urusi, uliotarajiwa kuanza jana jijini Sochi, akimwakilisha Rais John Magufuli.
“Katika kipindi hiki ambacho Tanzania inajenga reli ya kiwango cha kimataifa ya SGR pamoja na kufufua reli ya Kaskazini, inaikaribisha Kampuni ya Russian Railways kwa mikono miwili ije ifanye mazungumzo rasmi na Wizara husika. Pia Serikali inao mkakati wa kujenga reli mpya katika ukanda wa Kusini kutoka Mtwara hadi Ruvuma ili kuiunganisha bandari ya Mtwara na mikoa ya Kusini pamoja na nchi jirani za Malawi na Zambia,” alisema.
Alisema Tanzania kwa sasa inahitaji kuimarisha usafiri wa ndani wa reli hasa katika majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya na Tanga hivyo endapo mazungumzo kati ya wizara husika na kampuni hiyo yataonekana kuwa na tija na yana maslahi kwa Watanzania, kampuni hiyo itapewa fursa ya kuwekeza nchini.
Amesema kampuni hiyo yenye uwezo mkubwa wa kujenga reli mpya, kukarabati, kutengeneza injini za treni na mabehewa na ukarabati wake inahitajika nchini ili kufanikisha mpango wa serikali wa kuimarisha reli za zamani za Tazara, ya Kati na kufungua ya Kaskazini inayounganisha mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Kilimanjaro na Arusha.
Waziri Mkuu alizungumza na mkurugenzi huo juzi mjini Sochi nchini Urusi, ambako alitumia fursa hiyo kuikaribisha Russian Railways kuwekeza nchini hususani katika sekta ya ujenzi, ufundi na mafunzo ikishirikiana na kampuni za Watanzania. Waziri Mkuu yuko nchini Urusi kuhudhuria mkutano baina ya Wakuu wa Nchi na Serikali kutoka Mataifa ya Afrika na Urusi, uliotarajiwa kuanza jana jijini Sochi, akimwakilisha Rais John Magufuli.
“Katika kipindi hiki ambacho Tanzania inajenga reli ya kiwango cha kimataifa ya SGR pamoja na kufufua reli ya Kaskazini, inaikaribisha Kampuni ya Russian Railways kwa mikono miwili ije ifanye mazungumzo rasmi na Wizara husika. Pia Serikali inao mkakati wa kujenga reli mpya katika ukanda wa Kusini kutoka Mtwara hadi Ruvuma ili kuiunganisha bandari ya Mtwara na mikoa ya Kusini pamoja na nchi jirani za Malawi na Zambia,” alisema.
Alisema Tanzania kwa sasa inahitaji kuimarisha usafiri wa ndani wa reli hasa katika majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya na Tanga hivyo endapo mazungumzo kati ya wizara husika na kampuni hiyo yataonekana kuwa na tija na yana maslahi kwa Watanzania, kampuni hiyo itapewa fursa ya kuwekeza nchini.