ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 82,489
- 88,633
Alikuwa akijibu maswali katika Program ya Mjadala ya Club House ya Msemaji wa Serikali.
========
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema, takribani nusu ya miradi ya kimkakati iliyoainishwa na serikali ipo kwenye sekta ya nishati.
January amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuwaamini na kuwapa Jukumu hilo na akasema hata utamaduni wa kazi katika wizara hiyo umebadilika. Alisema hayo baada ya kujibu maswali katika programu ya mjadala katika Club House ya Msemaji wa Serikali.
"Sisi tunachoomba ni muda na subira, kwasababu kazi hizi matokeo yake yanachukua muda kupatikana na hukumu ya kazi tunayoifanya sasa tungeomba itolewe mbele kidogo na sio sasa," alisema.
January alisema miaka ya nyuma wizara hiyo ilikuwa na sifa mbaya ya rushwa, mikataba mibaya lakini sasa wizara hiyo na taasisi zake wana mipango mahususi kuhakikisha wanazingatia maadili.
Alisema takribani kila siku kuna zabuni inatolewa katika wizara hiyo na takribani watu 30 wanazikosa zabuni hizo kila siku hivyo wanaokosa wanakuwa na hisia kwamba waliopata hawakupata kihalali.
Habari Leo
========
Waziri wa Nishati, January Makamba amesema, takribani nusu ya miradi ya kimkakati iliyoainishwa na serikali ipo kwenye sekta ya nishati.
January amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassani kwa kuwaamini na kuwapa Jukumu hilo na akasema hata utamaduni wa kazi katika wizara hiyo umebadilika. Alisema hayo baada ya kujibu maswali katika programu ya mjadala katika Club House ya Msemaji wa Serikali.
"Sisi tunachoomba ni muda na subira, kwasababu kazi hizi matokeo yake yanachukua muda kupatikana na hukumu ya kazi tunayoifanya sasa tungeomba itolewe mbele kidogo na sio sasa," alisema.
January alisema miaka ya nyuma wizara hiyo ilikuwa na sifa mbaya ya rushwa, mikataba mibaya lakini sasa wizara hiyo na taasisi zake wana mipango mahususi kuhakikisha wanazingatia maadili.
Alisema takribani kila siku kuna zabuni inatolewa katika wizara hiyo na takribani watu 30 wanazikosa zabuni hizo kila siku hivyo wanaokosa wanakuwa na hisia kwamba waliopata hawakupata kihalali.
Habari Leo