Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,930
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemuagiza Kamishna wa Uhamiaji kutotoa kibali kwa Mtanzania yeyote kuondoka nchini kwa madai ya kupata kazi nje ya nchi bila kujiridhisha kuwa anayo mikataba ya sehemu anayokwenda kufanya kazi
Ametaka pia Kamishna wa Uhamiajia ajiridhishe kwa kufanya mawasiliano na Balozi husika katika nchi ambayo mtanzania huyo atadai anaenda kufanya kazi
Kauli hiyo ameitoa wakati wa shughuli ya maadhimisho ya kupinga usafirishaji haramu wa binadamu nchini jana Julai 30 katika viwanja vya Mnazi Mmoja
Pia amesisitiza kuwa Serikali haikatazi Watanzania kwenda kufanya kazi nje ya nchi bali kinachotakiwa ni kufuata utaratibu kutokana na nchi kuendelea kuathirika na watu kusafirishwa kiharamu na kwenda kuteswa
Aidha katika maadhimisho hayo, Waziri Lugola amemfuta kazi Mjumbe wa Sekretarieti ya kupinga usafirishaji Haramu wa binadamu kwa kushindwa kujua idadi ya vyombo vinavyotakiwa kutaifishwa
Ifahamike kuwa, Tanzania imefanya maadhimisho ya kupinga usafirishaji hafamu kwa binadamu kwa mara ya kwanza yakiwa yamebeba kauli mbiu ya "Tokomeza usafirishaji haramu kwa watoto na vijana kufanikisha uchumi wa Viwanda"
Ametaka pia Kamishna wa Uhamiajia ajiridhishe kwa kufanya mawasiliano na Balozi husika katika nchi ambayo mtanzania huyo atadai anaenda kufanya kazi
Kauli hiyo ameitoa wakati wa shughuli ya maadhimisho ya kupinga usafirishaji haramu wa binadamu nchini jana Julai 30 katika viwanja vya Mnazi Mmoja
Pia amesisitiza kuwa Serikali haikatazi Watanzania kwenda kufanya kazi nje ya nchi bali kinachotakiwa ni kufuata utaratibu kutokana na nchi kuendelea kuathirika na watu kusafirishwa kiharamu na kwenda kuteswa
Aidha katika maadhimisho hayo, Waziri Lugola amemfuta kazi Mjumbe wa Sekretarieti ya kupinga usafirishaji Haramu wa binadamu kwa kushindwa kujua idadi ya vyombo vinavyotakiwa kutaifishwa
Ifahamike kuwa, Tanzania imefanya maadhimisho ya kupinga usafirishaji hafamu kwa binadamu kwa mara ya kwanza yakiwa yamebeba kauli mbiu ya "Tokomeza usafirishaji haramu kwa watoto na vijana kufanikisha uchumi wa Viwanda"