Wazee wana usemi "chini kunakwenda watu"

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,854
30,198
WAZEE WANA USEMI "CHINI KUNAKWENDA WATU"

Picha hizo mbili hapo chini hazihitaji maelezo mengi ni picha za Abdul Sykes na Julius Nyerere na wake zao.

Picha ya Abdul Sykes imepigwa Government House katika Garden Party ya Gavana Edward Twining na mkewe Mrs. Twining miaka ya 1950 wakati akiwa kiongozi wa TAA.

Picha ya Nyerere imepigwa miaka ya mwanzo ya uhuru 1960s.

Wazalendo hawa wawili hakuna aliyefungua kinywa chake kueleza kuhusu urafiki wao wala kueleza historia ya kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Lakini kwa bahati historia za wazalendo hawa wawili zote zimeandikwa na kwa hakika ndiyo historia ya harakati ya kupambana na ukoloni wa Mwingereza kupitia chama cha TANU.

Wake zao Bi. Mwamvua na Maria Nyerere wameshuhudia yote kwa macho yao na wamesikia mengi kutoka kwa waume zao katika yale ambayo yalifanyika wakati ule.

Baada ya karibu miaka 20 kupita Bi. Mwamvua maarufu kwa jina la Mama Daisy alikutana na Mama Maria Ukumbi wa Diamond siku Mwalimu alipokuwa na mkutano wa kuwaaga Wazee wa Dar es Salaam mwaka wa 1984.

Mama Maria Nyerere alikutana na wanawake wa Dar es Salaam baada ya Mwalimu kumaliza hotuba yake ya kuaga.

Siku ile ndiyo kwa mara ya kwanza Mwalimu alimtaja Abdul Sykes hadharani.

Mama Maria alipomuona Mama Daisy katika kundi lile la akina mama, Maria Nyerere aliwaambia wale wanawake waliokutanika kumuaga, ''Huyu Mama Daisy na mumewe ndiyo waliotupokea mimi na mume wangu hapa Dar es Salaam.''

Maneno haya kanieleza Mama Daisy.

Ilikuwa miaka mingi imepita mashoga hawa wawili hawajaonana.

Prof. Shivji na jopo la waandishi wa historia ya Julius Nyerere, Prof. Saida Yahya-Othman na Dr. Ng'wanzi Kamata walipokuja nyumbani kwangu kunihoji kuhusu maisha ya Julius Nyerere alipofika Dar es Salaam niliwaomba wafanye juhudi wazungumze na Mama Maria kuhusu siku za mwanzo za TANU khasa ile mikutano iliyokuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa Stanley na Mama Maria na Mama Daisy wakiwapo pale.

Sijui kilichotokea lakini kitabu kilipotoka imeelezwa kuwa Mwalimu aliishi nyumbani kwa Ally Sykes kwa miezi mitatu na imeelezwa kuwa chanzo cha taarifa ile ni Abbas Sykes.

Ukweli ni kuwa Mwalimu hakupata kuishi nyumbani kwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab Mtaa wa Kipata bali aliishi na Abdul Sykes na mkewe Bi. Mwamvua Mtaa wa Stanley.

Kidogo nilisikitika kwani kwa kosa hili mengi yamewapita yaliyofanyika nyumbani kwa Mama Daisy.

Wakati ule hakuna aliyefikiria hata kwa mbali kuwa Julius Nyerere atakuja kuwa kiongozi mkubwa sana ulimwenguni na jina lake litafahamika kote duniani.

Laiti Mama Maria angezungumza...

Screenshot_20210812-072306_Facebook.jpg


Screenshot_20210812-075408_Photos.jpg
 
WAZEE WANA USEMI "CHINI KUNAKWENDA WATU"

Picha hizo mbili hapo chini hazihitaji maelezo mengi mengi ni picha za Abdul Sykes na Julius Nyerere na wake zao.

Picha ya Abdul Sykes imepigwa Government House katika Garden Party ya Gavana Edward Twining na mkewe Mrs. Twining miaka ya 1950 wakati akiwa kiongozi wa TAA.

Picha ya Nyerere imepigwa miaka ya mwanzo ya uhuru 1960s.

Wazalendo hawa wawili hakuna aliyefungua kinywa chake kueleza kuhusu urafiki wao wala kueleza historia ya kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Lakini kwa bahati historia za wazalendo hawa wawili zote zimeandikwa na kwa hakika ndiyo historia ya harakati ya kupambana na ukoloni wa Mwingereza kupitia chama cha TANU.

Wake zao Bi. Mwamvua na Maria Nyerere wameshuhudia yote kwa macho yao na wamesikia mengi kutoka kwa waume zao katika yale ambayo yalifanyika wakati ule.

Baada ya karibu miaka 20 kupita Bi. Mwamvua maarufu kwa jina la Mama Daisy alikutana na Mama Maria Ukumbi wa Diamond siku Mwalimu alipokuwa na mkutano wa kuwaaga Wazee wa Dar es Salaam mwaka wa 1984.

Mama Maria Nyerere alikutana na wanawake wa Dar es Salaam baada ya Mwalimu kumaliza hotuba yake ya kuaga.

Siku ile ndiyo kwa mara ya kwanza Mwalimu alimtaja Abdul Sykes hadharani.

Mama Maria alipomuona Mama Daisy katika kundi lile la akina mama, Maria Nyerere aliwaambia wale wanawake waliokutanika kumuaga, ''Huyu Mama Daisy na mumewe ndiyo waliotupokea mimi na mume wangu hapa Dar es Salaam.''

Maneno haya kanieleza Mama Daisy.

Ilikuwa miaka mingi imepita mashoga hawa wawili hawajaonana.

Prof. Shivji na jopo la waandishi wa historia ya Julius Nyerere, Prof. Saida Yahya-Othman na Dr. Ng'wanzi Kamata walipokuja nyumbani kwangu kunihoji kuhusu maisha ya Julius Nyerere alipofika Dar es Salaam niliwaomba wafanye juhudi wazungumze na Mama Maria kuhusu siku za mwanzo za TANU khasa ile mikutano iliyokuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa Stanley na Mama Maria na Mama Daisy wakiwapo pale.

Sijui kilichotokea lakini kitabu kilipotoka imeelezwa kuwa Mwalimu aliishi nyumbani kwa Ally Sykes kwa miezi mitatu na imeelezwa kuwa chanzo cha taarifa ile ni Abbas Sykes.

Ukweli ni kuwa Mwalimu hakupata kuishi nyumbani kwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab Mtaa wa Kipata bali aliishi na Abdul Sykes na mkewe Bi. Mwamvua Mtaa wa Stanley.

Kidogo nilisikitika kwani kwa kosa hili mengi yamewapita yaliyofanyika nyumbani kwa Mama Daisy.

Wakati ule hakuna aliyefikiria hata kwa mbali kuwa Julius Nyerere atakuja kuwa kiongozi mkubwa sana ulimwenguni na jina lake litafahamika kote duniani.

Laiti Mama Maria angezungumza...

View attachment 1889176

View attachment 1889200
Upo vzr
 
Kwa hili la Mwalimu kuishi miezi mitatu kwa Abdul Sykes miaka Miezi mitatu, ama Abbas kadanganya au akina Mzee Shivji wamedanganya.

Hawa akina Shivji hawakujua kuwa mwenye kujua historia ya kweli juu Uhuru ni mmoja tu naye ni Mohammed Said!
 
Kwa hili la Mwalimu kuishi miezi mitatu kwa Abdul Sykes miaka Miezi mitatu, ama Abbas kadanganya au akina Mzee Shivji wamedanganya.

Hawa akina Shivji hawakujua kuwa mwenye kujua historia ya kweli juu Uhuru ni mmoja tu naye ni Mohammed Said!
Platozoom,
Hapana kwa sisi tuliozaliwa Gerezani miaka ile ya 1950 wazee wetu wote walikuwa wanachama wa TANU na sote kwa ajili hii tukiijua vyema historia ya uhuru na tumemuona Nyerere katikati ya wazee wetu katika mitaa yetu.

Si kweli kuwa mimi peke yangu ndiyo naijua historia hii.

Mjukuu wa Bi. Chiku bint Said Kisusa yeye ndiye aliyemvisha Nyerere shada la maua alipotoka UNO safari ya kwanza 1955 yu hai na bibi yake huyo alimsindikiza Nyerere uwanja wa ndege na picha yao nimeiweka hapa barzani mara nyingi.

Nyumba ya Bi. Chiku ilikuwa Mtaa wa Mchikichi jirani sana na duka la mufuta ya taa la Mama Maria Nyerere lililokuwa Mtaa wa Mchikichi na Livingstone.

Sote tuliokulia mitaa hii tulikuja kujua mengi katika historia hii ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Siko peke yangu.

Nilichokifanya mimi labda cha zaidi ni kuandika kitabu.

Tuje kwenye suala la Abbas Sykes na timu ya Issa Shivji kuhusu nyumba gani Nyerere aliishi baada ya kuacha kazi ya ualimu.

Tuanze na Abbas.

Abdul Sykes alimuhamisha kwenye chumba chake alichokuwa akikaa ili ampishe Nyerere.

Sasa inawezekana vipi yeye alieleze jopo la uandishi wa kitabu cha Nyerere lililokuwa likiongozwa na Prof. Shivji kuwa Mwalimu Nyerere alikwenda kukaa Kipata kwa Ally Sykes?

Tuje kwa jopo la uandishi wa maisha ya Mwalimu Nyerere.

Jopo limesoma kitabu cha Abdul Sykes na nimeeleza kuwa Nyerere aliishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley.

Naamini nimeeleweka.
Yako mengi.
 
WAZEE WANA USEMI "CHINI KUNAKWENDA WATU"

Picha hizo mbili hapo chini hazihitaji maelezo mengi mengi ni picha za Abdul Sykes na Julius Nyerere na wake zao.

Picha ya Abdul Sykes imepigwa Government House katika Garden Party ya Gavana Edward Twining na mkewe Mrs. Twining miaka ya 1950 wakati akiwa kiongozi wa TAA.

Picha ya Nyerere imepigwa miaka ya mwanzo ya uhuru 1960s.

Wazalendo hawa wawili hakuna aliyefungua kinywa chake kueleza kuhusu urafiki wao wala kueleza historia ya kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Lakini kwa bahati historia za wazalendo hawa wawili zote zimeandikwa na kwa hakika ndiyo historia ya harakati ya kupambana na ukoloni wa Mwingereza kupitia chama cha TANU.

Wake zao Bi. Mwamvua na Maria Nyerere wameshuhudia yote kwa macho yao na wamesikia mengi kutoka kwa waume zao katika yale ambayo yalifanyika wakati ule.

Baada ya karibu miaka 20 kupita Bi. Mwamvua maarufu kwa jina la Mama Daisy alikutana na Mama Maria Ukumbi wa Diamond siku Mwalimu alipokuwa na mkutano wa kuwaaga Wazee wa Dar es Salaam mwaka wa 1984.

Mama Maria Nyerere alikutana na wanawake wa Dar es Salaam baada ya Mwalimu kumaliza hotuba yake ya kuaga.

Siku ile ndiyo kwa mara ya kwanza Mwalimu alimtaja Abdul Sykes hadharani.

Mama Maria alipomuona Mama Daisy katika kundi lile la akina mama, Maria Nyerere aliwaambia wale wanawake waliokutanika kumuaga, ''Huyu Mama Daisy na mumewe ndiyo waliotupokea mimi na mume wangu hapa Dar es Salaam.''

Maneno haya kanieleza Mama Daisy.

Ilikuwa miaka mingi imepita mashoga hawa wawili hawajaonana.

Prof. Shivji na jopo la waandishi wa historia ya Julius Nyerere, Prof. Saida Yahya-Othman na Dr. Ng'wanzi Kamata walipokuja nyumbani kwangu kunihoji kuhusu maisha ya Julius Nyerere alipofika Dar es Salaam niliwaomba wafanye juhudi wazungumze na Mama Maria kuhusu siku za mwanzo za TANU khasa ile mikutano iliyokuwa ikifanyika nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa Stanley na Mama Maria na Mama Daisy wakiwapo pale.

Sijui kilichotokea lakini kitabu kilipotoka imeelezwa kuwa Mwalimu aliishi nyumbani kwa Ally Sykes kwa miezi mitatu na imeelezwa kuwa chanzo cha taarifa ile ni Abbas Sykes.

Ukweli ni kuwa Mwalimu hakupata kuishi nyumbani kwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab Mtaa wa Kipata bali aliishi na Abdul Sykes na mkewe Bi. Mwamvua Mtaa wa Stanley.

Kidogo nilisikitika kwani kwa kosa hili mengi yamewapita yaliyofanyika nyumbani kwa Mama Daisy.

Wakati ule hakuna aliyefikiria hata kwa mbali kuwa Julius Nyerere atakuja kuwa kiongozi mkubwa sana ulimwenguni na jina lake litafahamika kote duniani.

Laiti Mama Maria angezungumza...

View attachment 1889176

View attachment 1889200
We babu haya ma historia yanamsaidia nini mwanao katika kupambana na teknolojia?
 
We babu haya ma historia yanamsaidia nini mwanao katika kupambana na teknolojia?
Telegram,
Si adabu kumwita mtu, "we," khàsa ikiwa ni babu yaani mzee.

Mila zetu za Kiafrika zinajali sana umri.

Inaelekea umeghadhibishwa na hayo uliyosoma kwa mimi kusahihisha makosa katika historia ya uhuru wa Tanganyika.

Haya ni katika mambo ya kustaajabisha sana katika historia hii.

Wengi wamechomwa roho na kalamu yangu nilipoinyanyua kuandika historia ya wazee wangu katika kuunda TANU na kupigania uhuru waTanganyika.

Historia niliyoandika mimi si wengi walikuwa wanaijua kama hivi wewe ulivyokuwa huijui.

Kwa ajili hii iliwaumiza sana.

Wako walionitukana na wengine kunitisha.

Kwangu haya sasa ni mambo ya kawaida na nimeyazoea.
 
Back
Top Bottom