Ni kawaida ya mtu asiyejiamini au mwenye mashaka na anachokiongelea kutafuta audience ambayo ameizidi uelewa au ya washikaji wake ili pasiwepo wa kumuuliza maswali mazito.
Kwenye hiyo hotuba aliyoiwakilisha kwao amesema awewaita kuongea nao ili wamsaidie kufikisha ujumbe kwa watanzania. hawa wazee wataufikisha vipi huo ujumbe kwa watanzani!!!. Hotuba nzima ni kama anaongelea CDM na katiba. Mi nadhani ni kutaka kuonyesha ubabe tu. Mi nafikiri kama kweli nia ni njema na Raisi wetu ana busara Ni kwanini asikubali tu huo muswada usome kwa mara ya kwanza!!. Hii inaonyesha kuna dhamira inayotarajiwa kufanywa na CCM. Kwa mtazamo hiyo katiba itakuwa ni ya CCM na wanachama wake, sio ya watanzania wote, Kwasababu haina baraka na wananchi wa aina zote Tanzania. Hata viongozi wa dini hawakubaliani. KIKWETE shauri watu wako, tumia busara, kubali yaishe, ubabe hautatufikisha popote.
Anajua wana akili km yake na watamsapoti. Rejea hotuba yake aliyohu2bia wafanyakazi walivyotaka kugoma walimshangilia na kutoa maneno ya kashfa kumuunga ujinga wake aliokua akiuropoka.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.