Wazee wa CCM tunawaomba radhi Watanzania, vijana wetu wa CCM wametudhalilisha na kutuangusha

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Ngoma ya kitoto huwa haikeshi. Vijana ndani ya CCM walijichora kama ndio wenye chama na wafiachama kuliko sisi wazee waliotukuta chamani. Tuliwapokea na kuwalea lakini wakatupoka chama na kutuweka kando kama simu simu isiyo na bando. Wakakiteka na kukitesa chama. Filamu zote za kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni matunda ya hayo niliyoyasema.

Ushindi si kama kupanda mahindi. Ushindi, wakati wetu chamani, ulitokana na kuachia uwanja wa siasa na kupumbaza kuwa kulikuwa na usawa. Halafu, kura zilitubeba. Tulijitahidi kuonesha kwa mtazamaji yeyote kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki ingawa tulikuwa na maandalizi yetu ya kichama na kidola kuhakikisha kuwa kura hazituangushi.

Wabobezi wa kisiasa chamani tulikuwa tukiulizwa cha kufanya na tulishauri bila kiburi. Tulishauri kuwa demokrasia, hata kama haipo, lazima iwepo. Lazima ioneshwe kwa watazamaji kuwa ipo. Wakati wa kuhesabu kura na kutangaza matokeo, hatukuwa na msalia mtume. Hata mabomu yasiyo na hamu yalitumika ili matokeo kueleweka. Tukapambana hadi mahakamani.

Kwa uchafuzi na filamu inayoendelea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sisi Wazee na Makada Waandamizi wa CCM tunawaomba radhi ya wazi. Waandalizi na wasimamizi wa uchaguzi huu wamekuwa vichekesho. Hata wao kwasasa wanajuta kufanya walivyofanya na hawajui watokaje kwenye mkwamo huu. Wamebaki kujiongelesha, kujikasirisha na kujichekesha.

Sisi Wazee wa CCM tunajua kuwa viongozi wetu Vijana wa CCM ndiyo walioishauri vibaya Serikali kuhusu chama chetu kupata ushindi wa kihistoria. Kuhusu kupata ushindi wa kishindo kama nyundo. Waliendeshwa na mihemko ya kutaka kutufunika kwa mafanikio ya kiuchaguzi. Sisi Wazee tupo kimya, tunawachora tu. Najua tutaitwa kuulizwa suluhisho. Tutawakatalia hadi tuone wanalia.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Songea, Ruvuma)
 
kweli wamelikoroga na watalinywa tu hamna namna. Kwani mzee rumumba ulihamishwa au ruvuma upo kikazi zaidi
 
Wapinzani wameishiwa hoja kabisa.

Walikimbia Uchaguzi, Jaffo kawarudisha Ahah

Wasubiri aibu ya kukataliwa na wananchi.
 
Umesema uko Songea? Kuna shida ya maji huko, uwe makini. Habari za miaka mingi Mzee Mwenzangu
Screenshot_20191110-180753.jpeg
 
Wapinzani wameishiwa hoja kabisa

Walikimbia Uchaguzi,Jafo kawarudisha Ahah

Wasubiri aibu ya kukataliwa na Wananchi

Mumshukuru sana Magufuli kutumia madaraka yake kudhibiti vyombo vya habari, ili viwe vinaandika propaganda zake tu. Leo hii mgekuwa mnanuka, pamoja na udhibiti huo, bado wananchi wamepuuza huu ushenzi wenu kwenye uchaguzi.
 
Wapinzani wameishiwa hoja kabisa

Walikimbia Uchaguzi,Jafo kawarudisha Ahah

Wasubiri aibu ya kukataliwa na Wananchi
We jamaa inabid posho yako ipande kidogo kutoka buku saba unajidhailisha sana kwaajili ya chama ambacho kinawenyewe na wewe sio mmojawapo ujafikia levels za overgrown green baboon bado upo kweye ngaz ya pimbi wa kijani ila komaa anything for money brethren
 
Ngoma ya kitoto huwa haikeshi. Vijana ndani ya CCM walijichora kama ndio wenye chama na wafiachama kuliko sisi wazee waliotukuta chamani. Tuliwapokea na kuwalea lakini wakatupoka chama na kutuweka kando kama simu simu isiyo na bando. Wakakiteka na kukitesa chama. Filamu zote za kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni matunda ya hayo niliyoyasema.

Ushindi si kama kupanda mahindi. Ushindi, wakati wetu chamani, ulitokana na kuachia uwanja wa siasa na kupumbaza kuwa kulikuwa na usawa. Halafu, kura zilitubeba. Tulijitahidi kuonesha kwa mtazamaji yeyote kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wa haki ingawa tulikuwa na maandalizi yetu ya kichama na kidola kuhakikisha kuwa kura hazituangushi.

Wabobezi wa kisiasa chamani tulikuwa tukiulizwa cha kufanya na tulishauri bila kiburi. Tulishauri kuwa demokrasia, hata kama haipo, lazima iwepo. Lazima ioneshwe kwa watazamaji kuwa ipo. Wakati wa kuhesabu kura na kutangaza matokeo, hatukuwa na msalia mtume. Hata mabomu yasiyo na hamu yalitumika ili matokeo kueleweka. Tukapambana hadi mahakamani.

Kwa uchafuzi na filamu inayoendelea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, sisi Wazee na Makada Waandamizi wa CCM tunawaomba radhi ya wazi. Waandalizi na wasimamizi wa uchaguzi huu wamekuwa vichekesho. Hata wao kwasasa wanajuta kufanya walivyofanya na hawajui watokaje kwenye mkwamo huu. Wamebaki kujiongelesha, kujikasirisha na kujichekesha.

Sisi Wazee wa CCM tunajua kuwa viongozi wetu Vijana wa CCM ndiyo walioishauri vibaya Serikali kuhusu chama chetu kupata ushindi wa kihistoria. Kuhusu kupata ushindi wa kishindo kama nyundo. Waliendeshwa na mihemko ya kutaka kutufunika kwa mafanikio ya kiuchaguzi. Sisi Wazee tupo kimya, tunawachora tu. Najua tutaitwa kuulizwa suluhisho. Tutawakatalia hadi tuone wanalia.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Songea, Ruvuma)
Selemaaniiii..........!!!!
 
Ati wazee, hamuwezi kupata msamaa maana nyie ndio mliosababisha matatizo yote kwa kuwaandaa vijana kinyume na matakwa ya nchi na sasa ynatukuta sote!
 
Acha kujificha katika kivuli cha uanachama wa CCM wewe ni Chadema damu.
Yeye anajitambulisha ni CCM wewe unataka awe chama gani?
Hivi kila asemaye ukweli sio CCM bali Chadema?
Tena hayo yanasemwa na nyie CCM hivyo ni kuwa miongoni mwenu hamuamini Luna kusemea kweli!
 
Back
Top Bottom