ionosphere
Member
- Oct 25, 2014
- 25
- 3
Wenzangu mnisaidie nipo njia panda nina mchumba wangu ambaye tulikubaliana kuoana baada ya miaka 3 na sasa imebaki miezi saba tu kiukweli nampenda kwa dhati naye pia ananipenda kama anavyodai kwa sababu siwezi kuusemea moyo wa mtu ila kwa mtazamo wangu mimi naona pia ananipenda japo sina uhakika sana.
Sasa huyu mpenzi wangu n jirani yangu hivyo wazazi wetu wanafahamiana.
Makwazo yakaanza baada ya wazazi wangu kufahamu mwaka mmoja tu ndani ya mahusiano yetu sababu mwanamke ni muislamu na pia kubwa zaidi wanasema wanahofia uchawi kwa kuwa bibi yake mzaa mama wa mpenzi wangu alikuwa mchawi na wakanikanya nisiendelee nae.
Ila sikuwasikiliza na baada ya muda nae mpenzi wangu akasikia kwamba nmekatazwa nisiendelee nae, akaniulza swali moja kwamba linasema wewe unawasikilza wazazi wako au unafanya maamuzi yako nikamjibu mimi lazima nikuoe sitawasikilza naye akanijbu nami sipo tayari kukuacha hata kama ni bila harusi.
Wanajamiiforums tukaendelea na mahausiano yetu mpaka sasa hivi karibuni Mpenzi wangu kanipa taarifa za kunichoma moyo kwamba nae mama yake kamwambia akikubali kuolewa na mimi ahesabu hana wazazi na hawatakaa wamuelewe na sababu zao ni kwamba mimi mkristo na pia sisi majirani wa karibu mno kwa hiyo haitapendeza yeye aolewe karibu na nyumbani, na mpenzi wangu nae anasema hata kama wazazi wake hawataki yeye ni lazima aolewe na mimi.
Ila mimi naona giza tu hata pa kuelekea sioni jamani ushauri wenu ni muhimu nipo njia panda kwa nyongeza mpenzi wangu anamalizia chuo mwakani na mimi mfanyakazi kampuni fulani hivi.
Sasa huyu mpenzi wangu n jirani yangu hivyo wazazi wetu wanafahamiana.
Makwazo yakaanza baada ya wazazi wangu kufahamu mwaka mmoja tu ndani ya mahusiano yetu sababu mwanamke ni muislamu na pia kubwa zaidi wanasema wanahofia uchawi kwa kuwa bibi yake mzaa mama wa mpenzi wangu alikuwa mchawi na wakanikanya nisiendelee nae.
Ila sikuwasikiliza na baada ya muda nae mpenzi wangu akasikia kwamba nmekatazwa nisiendelee nae, akaniulza swali moja kwamba linasema wewe unawasikilza wazazi wako au unafanya maamuzi yako nikamjibu mimi lazima nikuoe sitawasikilza naye akanijbu nami sipo tayari kukuacha hata kama ni bila harusi.
Wanajamiiforums tukaendelea na mahausiano yetu mpaka sasa hivi karibuni Mpenzi wangu kanipa taarifa za kunichoma moyo kwamba nae mama yake kamwambia akikubali kuolewa na mimi ahesabu hana wazazi na hawatakaa wamuelewe na sababu zao ni kwamba mimi mkristo na pia sisi majirani wa karibu mno kwa hiyo haitapendeza yeye aolewe karibu na nyumbani, na mpenzi wangu nae anasema hata kama wazazi wake hawataki yeye ni lazima aolewe na mimi.
Ila mimi naona giza tu hata pa kuelekea sioni jamani ushauri wenu ni muhimu nipo njia panda kwa nyongeza mpenzi wangu anamalizia chuo mwakani na mimi mfanyakazi kampuni fulani hivi.