Wazazi wanatuchanganya.

Wazazi wanatuchanganya.

Afande Nyati

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2012
Posts
2,385
Reaction score
1,414
Imekuwa ni kama desturi sasa, unakuta mtu unataka kuoa/kuolewa umempata mpenzi wako mnapendana. Unaenda kwa wazazi kujieleza nimepata mchumba anatokea mkoa fulani ni wa kabila fulani...

Basi hapo ukitaja kabila tu weeeeeehh!! Utaona wanavyoanza kukugwaya... Utasikia oa/ olewa kwingine kote ila sio huko.... Usithubutuu...

Ila sasa ukipata mzungu ata hawaulizi ni dini gani wala kabila gani watakupongeza mnooooo

Sasa najiuliza ni kweli watu wa kabila moja huwa wanafanana tabiaa au ni kasumba tu za Ki Africa... Maana kwa upande wangu mpaka sasa nimeshapigwa biti niko njia panda....

Naombeni experience ya hili wajuzi wa mambo....
 
Mambo ya kuwapuuza wazazi ndo yametufikisha hapa, kujifanya tunaenda na wakati kwa kila kitu. Kuna mambo mengine wazazi wakisema inabidi ukae chini utafakari
 
Za kwako changanya na za kuambiwa. Ukabila na udini sio kigezo cha kumpata mke mwema
 
mambo ya kikabila na udini mm nayaona ya kizamani na mara nyng sikuiz unakuta hata huyo mtu unaekatazwa hajakulia huko mkoani/kabila lake. Pamoja na wazazi wetu kuwa na hekima lkn hawapo sawa wakati wote, chambua hoja zao unaeza kosa mke/mume bora kisa mtazamo wa kizaman wa kikabila
 
Wako sahihi kwa kiasi kikubwa, faida pekee iliyopo ya kuoa kabila lingile ni kujenga mahusiano na makabila mengine na kuondoa migogoro. Hasala niliyoipata mimi nikwamba watoto hawajui kuongea lugha yetu wala ya upande wa Mke wangu.
 
mambo ya kikabila na udini mm nayaona ya kizamani na mara nyng sikuiz unakuta hata huyo mtu unaekatazwa hajakulia huko mkoani/kabila lake. Pamoja na wazazi wetu kuwa na hekima lkn hawapo sawa wakati wote, chambua hoja zao unaeza kosa mke/mume bora kisa mtazamo wa kizaman wa kikabila
Hiyo ni changamoto kubwa. Unakuta wote mmezaliwa town, mmekulia town, mmesoma town. Lakini linapokuja suala la kabila tu basi mazima tatizo. Ndo hapo najiulizs kuwa Mhaya, Mpare au msukuma lazima wote wawe the same??? Kwani huwez kuoa/ kuolewa na mmachame ukakuta ana tabia za kihaya?????
 
Hasa ukitaka kuoa Mchagga.

Wazazi wengi sana wa Kanda ya ziwa na Kusini hawataki watoto wao waoe uchagani.
 
Msikilize mzazi maana yeye anajua kuliko ww na ungelikuwa makini utotoni ungeliewa neno kaskazini ina maana gani

Kwenda zao maana nimelizwa sikumoja na mchaga mmoja mpaka taulo lol
 
Hasa ukitaka kuoa Mchagga.

Wazazi wengi sana wa Kanda ya ziwa na Kusini hawataki watoto wao waoe uchagani.
Sio mchaga pekee bali wanawake wengi wa kaskazini imeonekana kama ni tatizo... Hapa ni pamoja na Wapare, Wamachame, Wachaga nk....
 
Back
Top Bottom