G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 12,279
- 38,855
Seif Shariff anamaanisha kuwa dr. Shein ni kibaraka wa bara....anasema kuwa yeye ni kiongozi wa kwanza Zanzibar kuridhia kuwa raia wake akashtakiwe kwenye mahakama kuu ya Tanzania bara ambapo ni kinyume na katiba ya Zanzibar inayoitambua Tanzania bara kama nchi nyingine...Anasema kuwa enzi za Amani Abeid Karume wale wazee waliopekeka barua UN kudai mamlaka ya Zanzibar walipelekwa kushtakiwa Tanzania bara yeye akiwa Marekani na aliporudi alimuuliza Othman aliyekuwa AG wake akamjibu kuwa wamemwambia awashtaki akawaambia haoni kosa la kuwashtaki ndipo wakachukuliwa kupelekwa bara. Amani Karume aliamuru warejeshwe na wakarejeshwa Zanzibar mara moja!