MFULULIZO WA MAUAJI YA SIRI JIJINI ARUSHA SI SALAMA KWA CHAMA TAWALA NA TIMU ZAKE ZA KUSAKA URAIS KWA MTAJI WA DAMU YA WENGINE
Jamani hii programu ya mauaji ya msururu mkubwa wa wanachama wa CHADEMA na wafadhili wetu jijini Arusha tangu Askofu Laiser hadi leo mfanyabiashara mmoja baada ya mwingine mwisho wake lini??
Kimsingi kuna mtuanamdanganya Chatanda kwamba ili kuking'oa CHADEMA katika mioyo ya wananchi kule Kaskazini basi unahitaji kumualika Rais Kikwete kuja kuzindua mpango mzima huo kwa kuanza kukimbia mitaani A-Tauni na kupungia watu huku na kule.
Yote juu ya yote, CHADEMA hakiwezi kuondolewa katika mioyo ya wengi kwa kuwaua baadhi ya wakubwa wao.