Wauza mitumba grade "A" kwa Jumla

Wauza mitumba grade "A" kwa Jumla

Kila mtu ana aina ya biashara ya aina yake mwingine anahitaji nguo za watoto, mwingine za kiume mwingine za kike, ninapomwambia mtu njoo whatsapp ni tuweze kuulizana maswali yote hayo, hapa tutajaza uzi na km ukiangalia majibu kuna niloyemjibu bei ni kuanzia 650,000 kuja chini. kila aina ya nguo na bei yake, Nadhani nimeeleweka.

Wengine hatupo huko watsapp usitulazimishe kuja huko,hivi unashindwaje kujibu kila kitu hapa kwa uwazi kama biashara ni yako kweli?? Eti tutajaza uzi.. hivi unafahamu ukubwa wa server za Jf mpaka udhanie tutazijaza kwa hiki ki uzi chako kilichokosa hata picha?
 
Sasa kama kila kitu unasema "NJOO WHATSAPP", sasa umeleta huku JF taarifa ya kazi gani..?? Si ungetusubiri huko huko whatsapp tuje...!!!!

Ukiweka bango la biashara, disclose details zote muhimu ili uache wanunuzi waamue. Sasa kila kitu unaficha, ukiulizwa unasema njoo watsapp.
Shangaa au anafanya udalali au bei sio fixed maana wajinga ndo waliwao
 
Yan ujaze uzi kwa tangazo dogo tu hili na halina picha? Kama ulikuwa hujui, kuficha ficha taarifa ndo utafanya tujaze uzi kwa sababu maswali yatakuwa mengi, na wenye povu watakuwa wengi. Lakini kma tangazo lingekuwa SELF EXPLANATORY, wala tusingeuliza maswali yyt, ungeona meseji za oda tu kwa waliokuwa interested na mzigo.
 
Kila mtu ana aina ya biashara ya aina yake mwingine anahitaji nguo za watoto, mwingine za kiume mwingine za kike, ninapomwambia mtu njoo whatsapp ni tuweze kuulizana maswali yote hayo, hapa tutajaza uzi na km ukiangalia majibu kuna niloyemjibu bei ni kuanzia 650,000 kuja chini. kila aina ya nguo na bei yake, Nadhani nimeeleweka.

sasa kama unafanya biashara kwa whatsapp kwann hukuwatafuta wateja wako kwa whatsapp tambua ukiweka kitu hapa kwa uwazi unapunguza usumbufu.
ushauri ukifanya biashara wacha kuficha mambo utaonekana mwizi hasa hzo biashara za whatsapp weka kila kitu hapa na watu watakuuliza kila kitu mkikubaliana kwenye malipo ndo mnanza kuitana huko whatssapp. Sasa kama saiz tuu unaita mtu wasap kwenye malipo siutamwambia mkalipane BOT
 
Ni wauzaji wa mitumba kwa jumla (Mabalo), tunapatikana Mapambano karibu na Zahanati ya kijitonyama, tuna tunatuma Mikoa yote, kwa mawasiliano zaidi piga/Whatsapp number 0715559494. Karibuni sana (Kwa walio serious tu, km hauko serious waachie kwenye nia)
MNA ball za kilo ngapi Na je ni MX ? Au kama shati nishati tupu Na bei gani ball?
 
MNA ball za kilo ngapi Na je ni MX ? Au kama shati nishati tupu Na bei gani ball?
Mabalo ni ya 45Kg, Mixed niloyonayo ni ya suruali za kike tu. Bei zinategemea na aina ya nguo unazo hitaji, mfano Men Jeans 480,000? ladies' silk dress 550,000,/= ladies cotton dress 500,000/=
 
Ni wauzaji wa mitumba kwa jumla (Mabalo), tunapatikana Mapambano karibu na Zahanati ya kijitonyama, tuna tunatuma Mikoa yote, kwa mawasiliano zaidi piga/Whatsapp number 0715559494. Karibuni sana (Kwa walio serious tu, km hauko serious waachie kwenye nia)
Nina wasiwasi na customer care yenu, mana hiyo mikwara sio ya nchi hii.
 
Mabalo ni ya 45Kg, Mixed niloyonayo ni ya suruali za kike tu. Bei zinategemea na aina ya nguo unazo hitaji, mfano Men Jeans 480,000? ladies' silk dress 550,000,/= ladies cotton dress 500,000/=
sasa mbona umeeleza vizuri, kwenye biashara usifiche kitu weka wazi kila kitu ili upunguze maswali yasiyo ya msingi
 
Kila mtu ana aina ya biashara ya aina yake mwingine anahitaji nguo za watoto, mwingine za kiume mwingine za kike, ninapomwambia mtu njoo whatsapp ni tuweze kuulizana maswali yote hayo, hapa tutajaza uzi na km ukiangalia majibu kuna niloyemjibu bei ni kuanzia 650,000 kuja chini. kila aina ya nguo na bei yake, Nadhani nimeeleweka.
Wewe dada vipi, weka vitu vyote kwenye uzi hapo juu ungeepusha maswali mengi,
Alafu jf hawalipii jaza uzi utakavyo ni free kabisa, ila weka taarifa zote mhimu kwenye uzi, mambo ya kufwatana wasap wengine tukisikia ata stim zenyewe zinakata,
 
Mabalo ni ya 45Kg, Mixed niloyonayo ni ya suruali za kike tu. Bei zinategemea na aina ya nguo unazo hitaji, mfano Men Jeans 480,000? ladies' silk dress 550,000,/= ladies cotton dress 500,000/=
Nuru bello LA vikoti vya like unazo?bei gani
 
Samahani unaposema grade A unamaanisha nn?kwa maana kwa jinsi ninavojua hamnaga grade A ya moja kwa moja yaan belo la A bali unakuta belo lina grade A na ngunya...je grade A unayozungumzia ww ni kwamba haina ngunya kbsa?ni pure grade A?
 
on litaka kujua idadi hata kwa kukadiria tu ,nipige hesabu zangu,nawauziaga wanfunzi nave an a egemea boom
 
Back
Top Bottom