Watumishi wa umma, leo hamtangaziwi nyongeza, bali kulipwa sehemu ya madeni yenu ya nyongeza

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Ik8fika July mwaka huu,tutakuwa tunaingia mwaka wa sita tangu watumishi wa umma waongezewe kwa mara ya mwisho mishahara pamoja na nyongeza ya mishahara ya Kia mwaka mpya wa fedha (annual increament).

Annual increament hii ambayo iko kisheria, kwa miaka hii sita kwa mtumishi mwenye mshahara wa kawaida tu serikalini haipungia jumla ya shilinhi 50,000/= mpaka 60,000/=. hii ikiwa ni mbali na nyongeza inayotolewa kwa ridhaa ya Raisi na serikali yake.

Piga ua garagaza, Raisi Samia hawezi toa nyongeza itayozidi shilingi 50,000 hata kwa watumishi wa kima cha chini hivyo atachofanya Mama leo ni kuanza tu kuwalipa watumishi sehemu ya kile walichostahili kwa miaka 6 iliyopita.

Hivyo, leo hakuna hakuna kutangaziwa increament kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022 zaidi ya kulipwa sehemu ya increament watuhumiwa walizostahili kulipwa tangu July 2016(madeni ya increament).Huu ndio ukweli mchungu.

Kwahiyo, watumishi wanapaswa sana sana kumshukuru Mama walau kwa kuwalipa sehemu ya madeni yao ya miaka mitano iliyopita na si kushangilia nyongeza ya mishahara kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.

Walioshangia mwendazake kuwakandamiza kwa miaka 6 iliyoita, ndio hao hao leo wataendesha propaganda kuwa mmeongezewa mishahara wakati kiuhalisia mnalipwa tu sehemu ya mnachoidai serikali unless watatangaza kuwalipa malimbikizo yenu yote na nyongeza juu kitu ambacho sio rahisi kutokea.

Ukweli ndio huo japo ni mchungu.
 
Kama CCM hamtaki kuongeza mishahara, tegemeeni wapiga kura wenu wataanza kuteseka zaidi kwenye kupata huduma za jamii kupitia taasisi na mashirika ya umma.
 
Serikali haiwezi kutangaza nyongeza ya mishahara kwa wafanyakaziawafanyakazi wataongezewa Bei ya vitu,
Alisikija mlevi mmoja akisema.
 
Back
Top Bottom