Kiongozi Miongoni
Senior Member
- Feb 6, 2021
- 197
- 255
Katika mizunguko yangu ya hapa na pale nilifika katika ofisi za mamlaka ya mapato Tanzanian TRA mkoa wa Shinyanga nikiwa na shida ya kupata TIN number kwa ajili ya matumizi yangu nikiwa nimeambatana na baadhi ya wafanyazi katika kampuni yangu.
Nilimkuta dada mmoja ana kauli mbaya sana, ana majivuno, anawajibu watu jinsi anavyotaka lakini zaidi ya yote anafanya kazi kwa taratibu sana huku mda mwingi akiongea na simu tena akiongea maswala ambayo siyo ya kazi.
Siku hiyo sikuweza kupata TIN na ilinibidi niondoke baada ya kukaa hapo ziadi ya masaa manne.
Kesho yake nilirudi nikakutana na dada mwingine ambaye pia ana tabia kama za yule wa mwanzo tena kibaya zaidi huyu ana hata kisilani kwa wateja. Siku hiyo pia sikufanikiwa kupata TIN baada ya kuambiwa kuwa information zangu zimetumwa Dar HQ kwa ajili ya kutengezewa TIN ,hii ni baada ya awali kutumia passport yangu ya kusafiria kutengeneza driving license.
Siku ya ijumaa na leo jumatatu nimeenda pia na bado nimeendea kukumbana na vikwazo vile vile na nimeshuhudia pia wafanyazi hao wakiendelea kuwasumbua wateja.
Nilimkuta dada mmoja ana kauli mbaya sana, ana majivuno, anawajibu watu jinsi anavyotaka lakini zaidi ya yote anafanya kazi kwa taratibu sana huku mda mwingi akiongea na simu tena akiongea maswala ambayo siyo ya kazi.
Siku hiyo sikuweza kupata TIN na ilinibidi niondoke baada ya kukaa hapo ziadi ya masaa manne.
Kesho yake nilirudi nikakutana na dada mwingine ambaye pia ana tabia kama za yule wa mwanzo tena kibaya zaidi huyu ana hata kisilani kwa wateja. Siku hiyo pia sikufanikiwa kupata TIN baada ya kuambiwa kuwa information zangu zimetumwa Dar HQ kwa ajili ya kutengezewa TIN ,hii ni baada ya awali kutumia passport yangu ya kusafiria kutengeneza driving license.
Siku ya ijumaa na leo jumatatu nimeenda pia na bado nimeendea kukumbana na vikwazo vile vile na nimeshuhudia pia wafanyazi hao wakiendelea kuwasumbua wateja.