Watu wa Dar ni wachoyo sana.

Watu wa Dar ni wachoyo sana.

Hyo tu haikufanyi useme watu wa dar kwan hao n jamaa zako na marafiki zako tu na cjui research yako umeifanya mikoa mingap na kwa muda gan hadi umekuja na hitimisho hili
 
Ikiwa assumption yako ya kwanza kabisa ni kwamba hao jamaa ni wachoyo basi ni kweli ungekuwa kimeo... I mean, ulikuwa prepared kuwaongezea watu bajeti kwahiyo the best shot ilikuwa kukuambia wamesafiri!!! Hata mimi ningekuambia nimesafiri!!

Kwanini huku-assume kwamba Dar watu wapo busy sana kiasi kwamba wakigundua upo Dar na utawatembelea basi wanajifanya wamesafiri ili usiwaharibie ratiba zao!!!
Mkuu nilikuwa vizuri, sikuhitaji chochote toka kwao bali salamu tu.
 
Mimi Huwa Nikifika Dar Namwambia Nimekuja Na Mchele Na Samaki Wa Mwanza Utasikia Mzee Karibu Sana Nakusubiri Stend Mpaka Bash Lifike Ila Suala La Uchoyo Wanaambukizana Unashangaa Ndugu Anatoka Mkoani Akifika Dar Anabadilika Kabisa Kuanzia Lifestyle Ila Wenyewe Wakija Kwetu Tunawakirimu Mpaka Basi Na Wakirudi Makwao Tunawafungashia Na Chakula Cha Kutosha Wakale Kwao
 
Hivi karibuni nilikuwa Dar es Salaam kwa safari ya kikazi, nilikaa huko Dar kwa muda wa wiki mbili, hivyo nikaamua kuwatafuta ndugu jamaa na marafiki ili niwasalimie kabla sijarudi kwetu.

Majibu niliyokuwa napata yalinishangaza sana, kila niliyempigia simu na kumwambia nipo Dar aliniambia yupo safarini Bagamoyo mara Zanzibar, nikabaki kujiuliza ina hawa watu wote walipanga kwenda Bagamoyo mimi nikija Dar, nimejaribu kushare jambo hili na watu mbalimbali wameniambia hata wao yaliwahi kuwakuta hayo.

Jambo lingine ambalo nimeligundua watu wa Dar wana maisha magumu tofauti na wanavyojikweza hivyo wanaona ukiwatembelea au ukikutana nao wataumbuka.

Watu wa Dar acheni uchoyo, mbona nyie mkija huku Mwanza na mikoani tunawapokea vizuri na kuwakarimu vizuri kwanini tukija huko kwenu mnaanza visingizio vya safari.
Umekuja Dar kikazi kwa nini unataka kuwachosha watu!? Ungeenda kushangaa Coco beach na uwanja wa Taifa. Watu wa Dar hatupendi usumbufu. Safari yako ya kikazi unataka kutupa Kazi ya kutuchosha. Huku huwa hatupelekeani maboga na matembele.
 
Sio Uchoyo Tu Bali Na Msongo Wa Mawazo Unaosababishwa Na Ukosefu Wa Fedha Jiji Gumu Sana La Dar Kila Kitu Hela.Siku Za Nyuma Watu Wa Dar Hawakuwa Wachoyo Pia Pesa Ilikuwepo Tuwaonee Huruma Jamani Dar Pazuri Kwa Baadhi Ya Watu Tu Hasa Magogoni
 
Mfumo wa maisha ndio wa kulaumiwa sio watu. We umeachwa na mmeo unakimbilia dar nani akulishe
 
Hivi karibuni nilikuwa Dar es Salaam kwa safari ya kikazi, nilikaa huko Dar kwa muda wa wiki mbili, hivyo nikaamua kuwatafuta ndugu jamaa na marafiki ili niwasalimie kabla sijarudi kwetu.

Majibu niliyokuwa napata yalinishangaza sana, kila niliyempigia simu na kumwambia nipo Dar aliniambia yupo safarini Bagamoyo mara Zanzibar, nikabaki kujiuliza ina hawa watu wote walipanga kwenda Bagamoyo mimi nikija Dar, nimejaribu kushare jambo hili na watu mbalimbali wameniambia hata wao yaliwahi kuwakuta hayo.

Jambo lingine ambalo nimeligundua watu wa Dar wana maisha magumu tofauti na wanavyojikweza hivyo wanaona ukiwatembelea au ukikutana nao wataumbuka.

Watu wa Dar acheni uchoyo, mbona nyie mkija huku Mwanza na mikoani tunawapokea vizuri na kuwakarimu vizuri kwanini tukija huko kwenu mnaanza visingizio vya safari.
😄😄😄😄Mara nyingi wanadai wameenda kibaha safari ya ghafla, Maisha yanakaba watu
 
wamekuona mzigo watu wa daslam kwa fursa hawajambo wakiona mgen mweny pesa kdg ndio utakaribishwa,huku maisha ni magum kwel tofaut na mikoani hata fungu la mboga ya majan huku inaanzia na 1k...fanya mchezo ww
 
Back
Top Bottom