James_patrick_
Senior Member
- Mar 20, 2017
- 106
- 194
Habari ndugu zangu
Mimi naishi uswahilini huku sasa kitu nilichokigundua ni kwamba siku hizi kumeongezeka watu kwenda kwa waganga sana pindi wanapoibiwa kuliko kwenda police.
Utasikia tu mimi lazima nimuonyeshe aliyeniibia yaani nitamkomesha na asilimia kubwa uwa wanaenda kweli kwa waganga.
Cha ajabu hatuoni lolote kutokea kwa mtu anayehisiwa. Sasa sijajua kama waganga wenyewe nao nguvu hamna na pia kwanini watu wanapenda kukimbilia uko.
Mtu unamwambia kabisa nenda police watajua la kukusaidia lakini mtu anaona kwa mganga ndio njia sahihi zaidi. Wadau sijui tatizo liko wapi na mbona siku hizi atuoni tena mashipa wala mabusha waganga nao wamekuwaje
Mimi naishi uswahilini huku sasa kitu nilichokigundua ni kwamba siku hizi kumeongezeka watu kwenda kwa waganga sana pindi wanapoibiwa kuliko kwenda police.
Utasikia tu mimi lazima nimuonyeshe aliyeniibia yaani nitamkomesha na asilimia kubwa uwa wanaenda kweli kwa waganga.
Cha ajabu hatuoni lolote kutokea kwa mtu anayehisiwa. Sasa sijajua kama waganga wenyewe nao nguvu hamna na pia kwanini watu wanapenda kukimbilia uko.
Mtu unamwambia kabisa nenda police watajua la kukusaidia lakini mtu anaona kwa mganga ndio njia sahihi zaidi. Wadau sijui tatizo liko wapi na mbona siku hizi atuoni tena mashipa wala mabusha waganga nao wamekuwaje