Watu kama kina "Pesa Ndesa" walifaa kuwa Mawaziri: Tanzania ingefaidi kipaji chake cha ujasiriamali

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Walioko msibani Moshi, wametuhabarisha historia na waliyoyaona kwa Hayati Mzee Dr. Ndesamburo. Alikuwa na mpangilio wa kuigwa kwenye biashara tangu akiwa kijana mdogo. Alianza na biashara ndogondogo hadi kumiliki magari,mahotel ya kitali, hatua kwa hatua. Wanasema hajawahi kukwepa kodi za serikali kama matajiri wengine wanavyofanya. Na kila jambo la kibiashara alilolianzisha,lilifanyika kihalali na kwa mafanikio makubwa,na waliopata ushauri kwake walifanikiwa. Kwa mtizamo wa karibu,alikuwa na kipaji cha kipekee kwenye masuala ya biashara. Laiti angekuwa serikalini,naamini juhudi zake zingekuwa za kitaifa zaidi,na nchi ingevuna kutokana na kipaji chake. RIP Mzee wetu.
 
  • Thanks
Reactions: SIM
Labda ndiyo sababu alikuwa mtoaji maana anajua alipoanzia
 
  • Thanks
Reactions: SIM
Back
Top Bottom