Watoto wa ndani ya Ndoa wapewe urithi zaidi ya watoto wa nje ya ndoa

Watoto wa ndani ya Ndoa wapewe urithi zaidi ya watoto wa nje ya ndoa

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
34,059
Reaction score
79,406
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

1. Watu waache dhulma. Watu waache utapeli. Watu waache kula jasho la watu wengine.

2. Asilimia kubwa ya wanaume huoa/kuishi na wanawake wakiwa bado hawajajipata. Yaani vijana wengi almost chini ya miaka 35 maisha yao bado yanakuwa yakuunga unga.

3. Wanapata Wanawake katika umri huohuo wakiwa apeche Alolo. Wanaishi kama Wenza, Mke na mume, wanajenga nyumba na familia yao.

4. Yawezakuwa mwanamke kipato chake kikawa kidogo kuliko mwanaume au hata asiwe na kipato kabisa ila ule uwepo wake tuu ni mchango tosha kwa mwanaume.

5. Wanachuma mali kwa pamoja kwa miaka labda kumi na tano.

6. Watoto wanazaliwa hapo. Baadhi ya miradi na kazi za uzalishaji watoto wanafanya. Kama kwenda shamba, kuchunga mifugo, kuuza duka, kutengeneza bidhaa, kuuza bidhaa n.k. watoto wa ndani ya ndoa wanafanya kazi hizo.

7. Baadaye Mungu amejalia, angalau maisha yanaonekana. Nyumba na vijimali vipo. Mwanaume ikatokea amezalisha mwanamke mwingine huko.

8. Yule mtoto hawezi kuwa Sawa na hawa watoto wa ndani ya ndoa. Yaani hata kimahesabu ya kawaida haiwezekaniki kuwa sawa. Hakunaga haki ya hivyo.

9. Hata ndani ya ndoa tuu watoto sio Sawa. Kuna maeneo kamwe hawatalingana.

10. Mfano. Mtoto mkubwa yaani wakwanza kuna wakati alibeba majukumu ya Mzazi kuwalea ndugu zake.

11. Kuwabeba, kuwaangalia wakati mama na Baba hawapo, kuwaogesha, kuwalinda ndugu zake, na majukumu mengine. Ndio maana zamani mtoto wa kwanza hupewa nafasi ya Mzazi pale wazazi hawapo. Kutokana na majukumu yake. Na yeye ndiye huwa mrithi kwa jamii nyingi.

12. Watoto wa ndani ya ndoa na nje ya ndoa wanachofanana ni suala la DNA zao zote ni za Baba mmoja.

13. Lakini kiuchumi hawawezi kufanana.

14. Kwenye haki, Wale waliozalisha au waliochangia uchumi wanahaki kupata zaidi kuliko wale ambao hawakuchangia Sana.

15. Mwanamke ambaye umekaa naye muda mrefu tangu ukiwa down ukiwa huna maisha, mkapigana tough mpaka ukafika hapo ulipo watoto wake wanahaki ya kupata zaidi kuliko watoto wa wanawake wengine.

16. Vinginevyo hakuna faida ya mwanamke kuolewa na mwanaume fukara, maskini, ambaye Hana maisha,
Kama mambo yenyewe mwishoni yanakuwa yanaenda kama hivyo.

17. Sisi Watibeli tunazingatia Sana suala la Haki, ukweli, upendo na Akili.

18. Yaani mwanaume wa Kitibeli aoe akiwa maskini, kisha akishatajirika amfananishe mkewe na watoto wa mkewe Sawa na wanawake wengine na watoto wa wanawake wengine hao sio watibeli.

19. Kijana usimsahau mke wa ujana wako. Kumaanisha mke ambaye alikustahi ukiwa bado Mdogo kwa Kila kitu, Mdogo kiuchumi, kiuzoefu wa maisha, karibu Kila kitu.

20. Na unapoambiwa usimsahau mke ea ujana wako wanamaanisha hata Watoto wake.

21. Nabii Ibrahim kama Watibeli wengine alifanya hivyo. Alijua wapi alipotoka na Sarah Mkewe, Alijua mchango wa Sarah katika utajiri wake. Hata Kama Sarah alikuwa hana kazi ya uzalishaji lakini uwepo wake kama mwanamke anayempenda ulitosha kuwa nguzo ya utajiri wa Ibrahim.

22. Ndio Maana Ibrahim hakusita kumfukuza Hajiri na Ishmael kwa ajilli ya Sarah mkewe na Isaka mwanaye.

23. Ni kweli mtoto hachagui azaliweje. Lakini ni Jambo la asili mtoto kubeba matokeo iwe hasi au chanya ya wazazi wake hasahasa Mama.

24. Desturi hii pia itafanya wanawake kufikiri mara mbilimbili kuzaa na wanaume waliooa(waume za watu) lakini pia kuzaa kabla hawajaolewa kwa kujua matokeo kuhusu watoto kupata shida.

25. Watibeli mfumo wetu ni uleule. Mtoto hurithi kwa Mamaake ikiwa ataishi upande wa mamaake. Na mtoto atarithi kwa Babaake ikiwa ataishi na Babaake.

26. Isipokuwa kama kuna Makubaliano kati ya mwanaume na mwanamke. Kwamba mwanaume akubali kwa hiyari yake, mbele za mashahidi na maandishi kwamba mtoto Fulani kwa jina Fulani aishi na Mamaake Kwa ruhusa ya Baba na atapata haki zote kwa mwanaume.

27. Mtoto anaweza kuishi kwa Mama lakini Baba yake akaamua kumrithisha Mali kwa hiyari ya Baba.
Kwani ni kweli watoto wa ndoa pia wanaweza wasiwe watoto wa mwanaume na watoto wa nje wakawa wa mwanaume.

28. Siku hizi wanawake nao wanatafuta Mali hivyo Sheria za Kitibeli zipo mbele ya muda.

29. Sheria hizi za haki ni Sheria za watu wenye Akili, wenye Utu, wapenda Haki. Na wenye Upendo.

30. Halikadhalika Mtoto ambaye amelelewa na Baba hatakiwi kurithi Mali za mama yake ambaye hakumlea. Isipokuwa kwa hiyari ya Mamaake.

31. Kwa Sisi watibeli, Urithi upo kwaajili ya kuendelezwa sio kutumiwa uishe. Ndio maana watoto uliowalea wewe mwenyewe ndio wanatakiwa Warithi Mali zako. Kwa sababu maadili uliowafundisha utawafundisha kutokana na future unayoiona wewe Kama Baba.

32. Mtoto ambaye hujamlea hana uwezo wa kuendeleza urithi wako kwa sababu Hana mafundisho yako, hajui ulikuwa unataka nini practical, hajui ulikuwa unafanyaje kazi zako, hajawahi kukuona ukifanya kazi za uzalishaji.

33. Mrithi anatakiwa kuwa karibu Yako. Akuone, akuige, ajifunze, awe wewe katika version mpya.

34. Waarabu na jamii za mashariki ya Kati, wahindi wanajua haya. Ndio maana hakuna jamii inayoweza jamii za mashariki ya Kati kwenye suala la mambo ya familia na urithi.

35. Sheria hizi hazilengi kumpendelea mtu. Zinalenga ustawi na haki.

Kufikia hapo sina la ziada.
Ijumaa Kareem

TaikonMaster
Kwa sasa Dar es salaam
 
Una hoja, in a bigger picture…. pengine ndivyo ilivyotakiwa kuwa ila sio sahihi kwasababu; Watoto wana haki tu na hawana wajibu. Sisi binadamu ndio tumewapa watoto wajibu hata kabla ya miaka 18.

Kwa mantiki yangu hoja ya mtoto wa nje kurithi kidogo inakufa.. Watoto wana haki ya kurithi si wajibu wa kuzalisha/kuchangia sababu ni watu ambao tunawaleta duniani bila ridhaa yao wakati huo huo tukiwa katika starehe.

Bado nasubiri kuishi katika jamii ambayo kuzaa ni jambo serious sana, sio hii unfortunately.
 
Hoja ngumu hii. Mambo ya ndoa ni changamoto. Kikubwa kila kaya ipambane kupata uchumi. Urithi kimsingi atabeba mke wangu. Naye alisema watasalia watakutana hukohuko
ila urithi na elimu ni haki ya mtoto hata vitabu vya dini viaagiza ivyo ila ukikosa urithi wa ardhi si mbaya kumpambania kwenye elimu ila si kukosa vyote ni laana kwako wewe kama mzazi
 
Kwanini kuwe na ubaguzi? Je kama hao wa ndani ndio wamewakuta wa nje?

Maisha ndivyo yalivyo.
Ubaguzi kwenye maisha hauepukiki.
Kwa sababu ubaguzi ndio Uhalisia, ukweli, na Haki.

Watoto watoto wa ndoa wakiwakuta watoto wa nje ya ndoa.
Hoja kubwa katika urithi ni kama ifuatavyo;
I) Kwanza lazima wawe watoto kinasaba.
ii) Mrithi lazima aishi na anayemrithi ili afundishwe na anayemrithisha.
Lengo la urithi ni kuendeleza sio kutumia iishe.
Hata kwenye utawala wa kifalme, au utajiri,
Mtoto anayerithi ufalme lazima awe karibu au katika uangalizi wa mfalme ili afundishwe yote anayotakiwa kufanya kabla hajarithishwa.

iii) Mrithi lazima afuate na atii maagizo ya anayemrithisha.
Sio kwa sababu umtoto wa ndoa basi hiyo inatosha kuwa mrithi. Nope!
Lazima uwe mtoto mtiifu. Unayeshika maagizo ya Mzee ili kumhakikishia kuwa Ile ndoto ya kufika Kanaani inatimia.

Ndio maana sisi wote ni watoto wa Mungu. Lakini ukitaka kurithi Ufalme wa Mungo lazima ushike amri na maagizo yake.
Huo sio ubaguzi ni utaratibu wa urithi duniani kote na katika falme zote.

Familia ya Isaka, Esau alikuwa Mkubwa lakini hakuwa mtiifu kwa Baba na mama yake ndio Maana urithi wa Esau ukaenda kwa Yakobo. Kwa sababu Esau alishaanza kukiuka Mila na desturi za Baba yake akaoa mataifa mengine. Jambo Hilo likamtoa kwenye reli.

Ilionekana hatatimiza mpango wa kurithi nchi ya Ahadi aliyoahidiwa Ibrahim na Mungu wao Yehova.

Yakobo pamoja na udogo na udhaifu wake mwingine lakini alikuwa mfuata Mila na desturi za Wazee wake. Hivyo alikuwa successor wa Abraham na Isaka.

So sio ubaguzi. Kwenye suala la urithi vigezo na masharti lazima vifuatwe.

Usipofuata ndio baadaye litazuka swali mbona Waafrika na baadhi ya jamii hawawezi kurithisha utajiri toka kizazi kimoja mpaka cha NNE?
Jibu lipo wazi
 
Una hoja, in a bigger picture…. pengine ndivyo ilivyotakiwa kuwa ila sio sahihi kwasababu; Watoto wana haki tu na hawana wajibu. Sisi binadamu ndio tumewapa watoto wajibu hata kabla ya miaka 18.

Yote hapo unaelezea kuhusu urithi.
Mzazi asipoishi na Mtoto wake hakuna namna ataweza kumrithisha elimu, falsafa, mitazamo, Imani,

Ndio maana mtoto ambaye hujaishi Naye sio mtoto wako na hawezi kukusikiliza ingawaje kibaolojia ni Wako.



Kwa mantiki yangu hoja ya mtoto wa nje kurithi kidogo inakufa.. Watoto wana haki ya kurithi si wajibu wa kuzalisha/kuchangia sababu ni watu ambao tunawaleta duniani bila ridhaa yao wakati huo huo tukiwa katika starehe.

Bado nasubiri kuishi katika jamii ambayo kuzaa ni jambo serious sana, sio hii unfortunately.

Binti Kiziwi,
Kuzaa ni Jambo serious Sana sema usipoliwekewa sheria halina u- serious wowote. Ni kama Wanyama tuu. Tena Bora na wanyama.

Nature haina huruma kwa sababu inazingatia uhalisia, haki na ukweli.
Ukikiuka hayo lazima majibu uyapate.

Kiuhalisia na kiukweli watoto hawafanani na hawawezi kuwa na Haki sawa hata Siku moja. Dunia iende Dunia irudi.

Hata kwa watoto waliozaliwa ndani ya ndoa. Bado hawana haki sawa. Ingawaje wote ni watoto lakini utofauti wao kiwajibu na kimajukumu unawapa haki tofauti zisizo lingana.

Iko hivi, mwenye wajibu mkubwa huwa na haki zaidi. Huku mwenye wajibu Mdogo huwa na Haki pungufu.
Hilo lazima watu waambiwe kwa sababu ndio ukweli.

Kuwa kiongozi ni kubeba wajibu Mkubwaz kutumikia wengine zaidi na ndio maana utapewa haki zaidi kuliko ambaye sio kiongozi.

Kuhusu uzalishaji wa watoto huo nimetoa kama mfano lakini ni mfano muhimu kwa sababu ni halisi katika mazingira yetu ya kiafrika.

Muhimu kuliko, wanawake wahakikishe wanaolewa yaani wanakuwa kwenye ndoa. Hilo ni Jambo la Kwanza.

Pili, Wanawake waruhusu uke wenza lakini kwa kufuata taratibu watakazokuta kwenye nyumba kubwa(mke wa Kwanza) sio mke Mdogo aje na taratibu zake.

Tatu, watoto lazima wakubali kumheshimu Baba na huyu ndiye anamaanishwa zaidi kwa sababu yeye ndiye mzizi wa ukoo.

Nne, watoto lazima wakubali hawajalingana yupo mmoja kati Yao ni mbeba maono wa familia na lazima wampe uongozi wa ukoo.
Mfano kwenye familia ya Yakobo tunaona Yusufu alikuwa ndiye mbeba maono ingawaje hakuwa wakwanza kwa Babaake Yakobo lakini alikuwa wakwanza kuzaliwa kwa Mamaake, Raheli.
Ndugu zake wakubwa walimkatalia.

Ukaribu wa mtoto na babaake ndio hutoa mwelekeo wa familia husika.
Yusuph alikuwa karibu na Babaake, Yakobo
Isaka alikuwa Karibu na Babaake, Abraham.
Yakobo alikuwa karibu na Mamaake, kilichomsaiddia ni kushika Mila na desturi

Suleiman alikuwa karibu na Babaake, Daudi,

Mpaka Baba anakuwa karibu na mtoto ujue kuna Jambo kaona. Na anakuwa anamuandaa kushika fimbo za utawala.

Kwenze hili wala haiwezekaniki kuivunja hiyo Kanuni
 
Yote hapo unaelezea kuhusu urithi.
Mzazi asipoishi na Mtoto wake hakuna namna ataweza kumrithisha elimu, falsafa, mitazamo, Imani,

Ndio maana mtoto ambaye hujaishi Naye sio mtoto wako na hawezi kukusikiliza ingawaje kibaolojia ni Wako.





Binti Kiziwi,
Kuzaa ni Jambo serious Sana sema usipoliwekewa sheria halina u- serious wowote. Ni kama Wanyama tuu. Tena Bora na wanyama.

Nature haina huruma kwa sababu inazingatia uhalisia, haki na ukweli.
Ukikiuka hayo lazima majibu uyapate.

Kiuhalisia na kiukweli watoto hawafanani na hawawezi kuwa na Haki sawa hata Siku moja. Dunia iende Dunia irudi.

Hata kwa watoto waliozaliwa ndani ya ndoa. Bado hawana haki sawa. Ingawaje wote ni watoto lakini utofauti wao kiwajibu na kimajukumu unawapa haki tofauti zisizo lingana.

Iko hivi, mwenye wajibu mkubwa huwa na haki zaidi. Huku mwenye wajibu Mdogo huwa na Haki pungufu.
Hilo lazima watu waambiwe kwa sababu ndio ukweli.

Kuwa kiongozi ni kubeba wajibu Mkubwaz kutumikia wengine zaidi na ndio maana utapewa haki zaidi kuliko ambaye sio kiongozi.

Kuhusu uzalishaji wa watoto huo nimetoa kama mfano lakini ni mfano muhimu kwa sababu ni halisi katika mazingira yetu ya kiafrika.

Muhimu kuliko, wanawake wahakikishe wanaolewa yaani wanakuwa kwenye ndoa. Hilo ni Jambo la Kwanza.

Pili, Wanawake waruhusu uke wenza lakini kwa kufuata taratibu watakazokuta kwenye nyumba kubwa(mke wa Kwanza) sio mke Mdogo aje na taratibu zake.

Tatu, watoto lazima wakubali kumheshimu Baba na huyu ndiye anamaanishwa zaidi kwa sababu yeye ndiye mzizi wa ukoo.

Nne, watoto lazima wakubali hawajalingana yupo mmoja kati Yao ni mbeba maono wa familia na lazima wampe uongozi wa ukoo.
Mfano kwenye familia ya Yakobo tunaona Yusufu alikuwa ndiye mbeba maono ingawaje hakuwa wakwanza kwa Babaake Yakobo lakini alikuwa wakwanza kuzaliwa kwa Mamaake, Raheli.
Ndugu zake wakubwa walimkatalia.

Ukaribu wa mtoto na babaake ndio hutoa mwelekeo wa familia husika.
Yusuph alikuwa karibu na Babaake, Yakobo
Isaka alikuwa Karibu na Babaake, Abraham.
Yakobo alikuwa karibu na Mamaake, kilichomsaiddia ni kushika Mila na desturi

Suleiman alikuwa karibu na Babaake, Daudi,

Mpaka Baba anakuwa karibu na mtoto ujue kuna Jambo kaona. Na anakuwa anamuandaa kushika fimbo za utawala.

Kwenze hili wala haiwezekaniki kuivunja hiyo Kanuni
💯 Nature haina huruma, inazingatia haki, uhalisia na ukweli.
 
Unatafutaje pesa huku huko karibu na watoto mangi?

Watoto wapo kwa bibi mama zao wameolewa 😅

Pesa ni tools.
Familia ndio lengo.

Mungu akikujalia ukapata pesa walau kwa mwezi 500k kwa mwezi. Unaweza ishi na watoto wako.

Au vinginevyo uniambie wapo kwa Bibi yao lakini mnaishi mji mmoja na Kila mara lazima uonane nao.

Muombe Mungu Sana akuepushe kukaa mbali na familia yako. Aiseeh nikuambie ukweli kuna umri ukifika utaona ulipoteza kitu kikubwa kwenye maisha. Alafu muda huo haiwezekaniki tena.
 
Back
Top Bottom