Watoto na UFO (Unidifined Flying Objects) Aliens

Area 51 iko Nevada
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yah aliens nahisi hufanya vitu vyao kwa siri na mpaka uione flight yao ni mpaka wakuselect, na ni bahati ukifanikiwa kuwaona hata maisha yako nahisi yatakuwa ya tofauti sana
Futa huu ujinga kichwani mwako mkuu usipo nielewa sasa utakuja kunielewa baadae akili yako ikikuwa zaidi ya hapa!!!!
 
Okay siwezi kukubishia ila kwenye haya mambo kuwa makini utachotwa vibaya bado unakasafari kidogo.. endelea na utafiti hata Mimi naamini hatupo peke yetu nisikuvunje moyo ktk hatua yako endelea mkuu..
 
Unafahamu kwamba yupo kijana aliyehojiwa na baadhi ya vyombo vya habari alisema ametokea future? miaka ya mbele kabisa amerudi miaka ya nyuma? Ukikutana na mtu wa namna hii utafanya nini? Na uthibitisho wake ni yeye mwenyewe kuwa ametoka future?

Haya matukio yanatengenezwa! Kwa sababu si kila kitu raia inabidi wavifahamu, kuna baadhi ya vitu raia inabidi wasivifahamu! Kutimiza lengo inabidi wakuandalie mazingira ambayo uta create image ya reality wewe mwenyewe kichwani mwako. Unafikiri ni kwa nini moja ya nukta wanayoitumia ni kwamba hao viumbe wanakuja sehemu ambazo ugunduzi mwingi unafanyika?

Hakuna alien anayekuja duniani! Ni project za kijeshi hizo wanawaficha watu. Ngoja niitafute documentary wanahojiwa majenerali wa kijeshi wanaweka wazi hizo siri nikiipata nitakuwekea.
 
Unafikiri ni kwa nini husikii hizo issue za alien Uarabuni, au Afrika au Amerika ya kusini au Thailand? Wakitaja baadhi ya nchi nilizozitaja au huo ukanda wa nchi nilizozitaja case atakazokumbana nazo ni watoto wadogo ndiyo wanaona wametokewa na Alien na si watu wazima. Hii ni kwa sababu akili ya mtoto bado ni ya kitoto na ni rahisi kurubuniwa! Haya mambo ya Alien utasikia zinatokea nchi kubwa kubwa zilizoendelea kisayansi na teknolojia kwa hiyo yatupasa tujiulize kuna sababu ipi iliyopo nyuma ya pazia?

Historia inakiri na inathibitisha kuwa flying saucer kwa mara ya kwanza ziliibuka na kuongolewa mwishoni mwa vita ya pili ya Dunia. Hii hali iliibuka walivyokuwa wanapambana na majeshi ya Hitler.

British na American bomber crew kipindi wanapigana na Hitler waliripoti kuona hali ya ajabu kwenye eneo la jeshi la Hitler walililokuwa wakipigana, wao walisema wameona kitu mfano wa Bell ambazo zinapaa kama ndege. Ndiyo maana German researchers waliamua kusema ukweli kuwa US government anafanya majaribio ya teknolojia ya kijeshi waliyoipata kipindi cha Nazi ya Hitler. Wakafafanua zaidi wakasema tukio lililotokea Roswell ilikuwa ni ajali ya moja ya majarabio ya Nazi era flying saucer known the Schriever-Habermohk model ambapo kulikuwa na ma-engineer wawili! Rudolf Schriever alikuwa ni engineer na ni test pilot, Engineer mwengine alikuwa ni Otto Habermohl. Hii project ilikuwa centred in Prague Czech Republic kati ya miaka 1941 na 1943, lakini ilihamishiwa America. Kwa nini? Miaka hiyo vita ilikuwa inafikia ukingoni na kipindi hicho scientist wa Hitler na project zake zilikuwa zinasombwa kwa kupiganiwa.

Unajua tukio la Roswell la Julai 8,1947 licha ya kishindo kikubwa kusikika kabla ya kuleta dhana ya alien jeshi la Marekai liliizima vipi hii taarifa unajua? Walisema ni weather balloon ndiyo iliyoanguka.
 
Sema mkuu sikukatalii izo issues unazosema zipo, ila ukitaka upate pia huelewa zaidi kasome icho kitabu nilichokuambia, maana pia mwandishi ameandika kuna vyuo kadhaa vimewahi kupewa fungu la pesa ili kufanya research kuhusu U.F.O na NASA. kakisome kitabu maana kina facts nyingi kuliko maelezo yangu maana ni ngumu kuandika kitabu kizima hapa kilichotumia miaka mingi ya investigation kuandika hapa dakika kadhaa. Japo nakubaliana na wewe kitu unachosema maana hakuna facts za observation za moja kwa moja kati yetu.
 
Nikiwa na miaka kati ya 10 na 12 mida ya saa tatu hivi kukiwa na giza totoro lakini kukiwa hamna mawingu, niliona kiwingu cha mduara kikiwa kinawaka angani chenye ukubwa kama ungo wa kupepetea mchele kikiwa kinawaka angani katikati ya utosi wangu ila sio chombo bali ni mduara tu huku ukizidi kufifia taratibu kwa muda wa madakika kadhaa kuashiria kiwingu kile kilikuwa kinazidi kwenda mbali kuelekea juu.

Wakati huo watu wote walikuwa ndani ila mimi nilitoka na kibalbu changu ambachonnilikichomoa kwenye torch fulani za zamani kwa jina la (ALKAIDA) nimekiunganisha na mabetirii/battery nyingi zilizopondwapondwa ili ziongeze chaji kibalbu hicho nilikuwa nakichezea nje maana ndiko kulikuwa na giza.
Sasa kulingana na tukio lile nikarudi ndani nikawahadithia wazazi ila hata hawakuelewa sanasana waliishia kuniambia ni balbu yangu imenipa mawenge. Kumbuka ilikuwa ni kijijini ambako kulikuwa hamna umeme alafu kulikuwa na miti mingi hivyo ni rahisi kuona mwanga wowote.
Mfano wa mwanga ule hauelezeki maana hakikuwa chombo wala haukuwa mwanga unaomulika kutokea mbali wala karibu ila mfano wake ulikuwa kama wingu jeupe sana la mvua lenye umbo la mviringo kiasi kwamba mviringo ule ulifanya kiwingu kile kionekane kama kinazunguka kwa kasi sana huku kikiishia angani kwa mwendo wa kupungua taratibu.
 
Kuna mambo kadhaa ya kujiuliza kuhusu hii dhana ya UFO.
Ni ajabu kubwa kwamba katika enzi hizi za tekinolojia kubwa tuliyo nayo ikiwemo ya Simu zenye camera bado hakuna hata picha moja isiyotia shaka yoyote ya kuwepo Viumbe hawa na Vyombo vyao??
Viumbe hawa ambao tunaamini kwamba wapo mbele yetu kitekinolojia kwa nini wanakuja duniani kwa namna ya wizi wizi na kuondoka mbio pale wanapoona kuwa wameonekana??
Wanatuogopa?
Wanatuogopaje sisi ambao wanatujua wazi kwamba tupo nyuma yako kiteknolojia?
Katika miaka yote wanayosemwa kuja duniani, haijatokea hata Mara moja vyombo vyao kupata ajali vikalazimika kushindwa kuruka kurudi kwao na kwa hivyo habari hii kuwa Breaking news ya CNN, BBC, REUTER, SKYNEWS NEWSWEEK, TIME na kadhalika?
Ni kweli kuwa mashirika makubwa haya yameshindwa kupata japo picha moja tu ya uhakika ili kuondoa Shaka ya hizi taarifa za uwepo was UFO??
Kama toka miaka 1950 vyombo hivi vilipoanza kudaiwa kwamba vinasuka duniani kutuchunguza, kama mpaka Leo Miaka 70 baadaye havijapata lolote basis having uwezo huo!
Binafsi had I nitakapopata majibu ya kueleweka kuhusu maswali yangu haya, bado nitaendelea kuamini tu kuwa HAKUNA cha UFO wala Nini Bali nimatamanio tu ya Bindamu ya jambo hill kuwepo!.....!!!
Tuendelee tu Kujifariji tu kwa filamu za 'Independence Day' 'War of the Worlds' na nyinginezo ...lakini HAKUNA kitu halisia kinachoitwa UFO!![emoji849][emoji849][emoji853][emoji853]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu watu wanakataa tu iyo inawezakuwa uliona U.F.O , Kuna jamaa anadai ni vifaa vya majeshi ya marekani huwa vinafanyiwa majaribio, swali la kujiuliza je hufanyiwa majaribio hadi africa?
 
mimi nimelipna hilo lidude kama sahani mwaka 2011 Mwanza ilikuwa ni usiku kuanzia sa 8 na saa 10 alfajir likaanza kupotea kwa mfumo wa kufifia kisha kwa kasi ya ajabu lisepa juu! siku hiyo nilikuwa natoka Buja narudi dar lakini nilipitia njia ya runzewe kutoa mwanza hivyo nilipofika mwanza nikachukua hotel maana niliingia kama sa tano usiku! na kilichofanya nisilale ile siku mteja mwenzangu wa chumba ambacho kipo kabla yangu alikuwa anafanya mambo yake huko ndani sasa mimi sikupenda kelele nikatoka nje wakat natoka ndipo nilishuhudia hilo dubwana live lipo chinochini linaonekana vizuri kabisa na ni kubwa na lilikuwa na muungurumo fulani. nilikaa kwa masaa mawili naliangalia na mpaka muda linapotea naliona hivi!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
na ushuhuda wa pili ktk pori la ushirombo niliona jambo ambalo mpaka sasa ninavyoandika hakuna mtu anaweza kuniamini lakini tukio hili lilitokea mbele yangu hivi, tena sio usiku ni mchana kweupe kabisa! tulikuwa gari mbili mwenzangu alikuwa kaniacha kama mita 500 hivi mm nipo nyuma namfuata na siku hiyo kulikuwa na mvua kubwa sana kiasi inabidi uwashe double hazard ili kama kuna mwingine anakuja aweze japo kuona kama kuna gari mbele! nilishuhudia semi ya yule aliyetangulia inainuka juu na inainuliwa na kitu kama miali ya umeme wa bluu yaani kama radi ile miale iliinuliwa usawa wa nguzo wa ya umeme! kisha ilipigwa na kitu kule juu mpaka container ikachanika kule juu huku ikodondoka kama vile mtu ameubetua mpira kisha akapiga shuti kali akidhamiria ule mpira udunde chini basi ilikuwa hivyo. kwa kweli nilipatwa na hofu sana sikusimama nilitembea nikaita pale lilikotokea lile jambo chuma ikapita fresh kabisa nilipogika Runzewe nikapak nikawa nasikilizia wa nyuma kama waliikuta ile ajali na ni kweli ile gari ilipata ajali lakini ilikuwa haitamaniki na tulineba mzigo mmoja machuma ya minala yalikuwa yanapelekwa Buja! hivyo mimi ni mmoja wa wanaoamini hatupo pekeyetu kwa matukio hayo mawili


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…