Elections 2010 Wateule wa JK serikalini sasa tumbo moto na ujio wa utawala mpya wa Dr. Slaa

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,174
Jamaa zangu wa CCM hapa Arusha wamesema watendaji serikalini haswa serikali za mitaa ndiyo tegemeo lao la kuokoa JK kupoteza pango hapo Ikulu.

Tetesi hizi zinazidi kubainisha ya kuwa watendaji serikalini wametahadharishwa kutochemkia kampeni za Chadema kwa sababu wakishinda jamaa hao watakuja na watu wao na watendaji serikalini waliopo watafungashiwa virago vyao.

Hili sasa ni kazi ya kulinda ajira na mlo serikalini na wala siyo kuheshimu matakwa ya walio wengi.....

Kwa hiyo watendaji wote serikalini wameaagizwa wafanye lolote liwezekanavyo kuzuia hili vuguvugu ambalo wanaliita ni balaaaaaaaaaaa ambalo kama likifanikiwa basi CCM itakufa kifo cha asili baada ya miezi sita maana makada wake ambao wengi wao wamo humo kwajili ya kumeza tonge tu na hawana ubia wa kiitikadi watakikimbia chama hicho.

Haya mambo yanatisha......uchakachuaji wa kura tu ndiyo waweza kuzuia kauli ya watanzania isiheshimiwe..................
 
Back
Top Bottom