Watanzania wengi ni wajuaji wasiojua kuhusu ripoti ya CAG

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,519
41,030
Nimeona wengi kwa mihemuko ya umbumbumbu wa kutojua taratibu na sheria zilizopo, wamekuwa wakimlaumu Rais kwa kutochukua hatua mara moja dhidi ya waliotajwa kwenye Report ya CAG.

Watu hao walitarajia baada tu ya report ya CAG, kesho yake Rais afukuze wale wote ambao ofisi zao zimehusishwa ama na upotevu, matumizi mabaya, matumizi hewa au matumizi yasiyofuata taratibu.

Watu hawa wasichojua ni kwa kwamba, kufuatana na taratibu zilizopo za kikatiba na sheria, hawa maofisa ambao ofisi zao zimetajwa na ofisi ya CAG ni lazima waitwe na kuhojiwa na kamati ya Bunge. Ukiwafukuza mapema kwa taarifa tu ya CAG bila ya wao kupewa nafasi au ya kujitetea au kutoa ufafanuzi, hiyo kamati ya Bunge itamhoji nani?

Kumbuka, kamati ya Bunge uwezo wake wa kikatiba kuhusiana na report ya CAG, unaishia kwa wale ambao ni watendaji wa Serikali, na siyo mwananchi ambaye yupo mtaani.

Mambo yale ya overinvoicing, hayapo kwenye report ya CAG. Yale yanaweza kufanyiwa kazi na Rais kwa taratibu zilizopo, lakini Rais hawezi kuanza kuchukua hatua mara moja kwa ofisi zilizotajwa na CAG.

Ikumbukwe kwenye report ya CAG, kuna upotevu, matumizi mabaya, ubadhirifu, kutofuata taratibu, matumizi hewa, n.k. Na hayo yanahusishwa na ofisi, report haitaji mtu specific.

Nadhani baada ya Bunge, kitakachofuatia, ni kuwatambua wahusika wa moja kwa moja. Na hao wahusika itabidi makosa yao yatambulike bayana. Kama ni uzembe, uwezo mdogo au kutojali, huyo kama mimi nikiwa ndiyo ofisi ya uteuze au mwajiri, nafukuza mara moja.

Kama ni wizi, huyo ni kumkabidhi kwa Polisi ili afikishwe mahakamani. Kama ni kutokana na maumuzi yenye uwezekano wa msukumo wa rushwa (kwa mfano utoaji wa tenda zenye gharama kubwa kuliko uhalisia wa gharama), huyu kabidhi kwa TAKUKURU, achunguzwe halafu afikishwe mahakamani.

Japo ni dhahiri tuna Bunge ambalo siyo la wananchi, ni la watu waliopachikwa na mtu mmoja kutoka chama kimoja kwa mapenzi yake, hatuna namna, yatubidi tusubiri.

Hatutegemei makubwa toka Bungeni maana hata hao wabunge wenyewe ni zao la uovu, na wengi wao upeo wao ni mdogo, uadilifu wao ni wa mashaka makubwa, labda pengine mmoja mmoja atajitutumua na kuitafuta hekima.

Ingawa mara nyingi mtu akiwa mwovu, kama walivyo hawa wabunge wengi ambao ni watoa rushwa, wevi wa kura, n.k, dhamira inakosa ujasiri dhidi ya waovu wenzao. Ni nadra sana jambazi akachukua jiwe kumpiga jambazi mwingine, japo kuna wakati anaweza kujitutumua ili kujikosha mbele ya watu wema ili naye aonekane ni mtu mwema.

Tusubiri, hatua zote zipite ili tupate uhalali wa kumlaumu Rais, kama amechukua hatua au hapana.
 
Unajidanganya kujua "sheria na taratibu" ndio kujua kila kitu, wakati wajanja wanatumia hicho kivuli kukwepa lawama, wewe unaimba tu sheria na taratibu, wakati field hali ni tofauti.

Ukiona mtu anaandika jambo, ujue ameshachukua hizo sheria zenu na taratibu zenu, amejumlisha na yale yanayotokea field, ndio akapata majibu anayokuja nayo, kumlaumu Rais aliye dhaifu.

Mahaba yenu yaliyopitiliza yamewafunga upeo kifikra, mmekubali kudanganyika na "sheria na taratibu" ambazo hazifuatwi, au kufuatwa ni mpaka pale mambo yawabane ndio watafutie hapo mlango wa kutokea.

Hilo bunge ulilolizungumzia kwenye mada yako ndio hili hapa chini, linaloagizwa na Rais badala lenyewe limuagize Rais kama sheria zenu na taratibu zinavyosema?
Screenshot_20230407-052209_Gallery.jpg


Kwa mantiki hiyo niambie, kwanini Rais asilaumiwe pamoja na hizo "sheria na taratibu" zako unazoandika hapa?

Wengine tulishatoka nje ya box wakati nyie bado mmejificha uvunguni, ukishapata jibu hapo then tell us, nani mbumbumbu wa kweli kati yetu?
 
Even a lay man anajua kwamba hii nchi inatafunwa na sasa hivi inatafunwa madudu yatakayopatika repoti ijayo..., issue sio tu kushughulikia watafunaji pindi wanaposhikwa wametafuna bali kuzuia mianya ya kutafuna..., sasa hata hio mianya kama ipo na bado inaendelea kuwepo means the system and the people involved are rotten, na kama hakuna wa kulaumu wala wa kuweza kuziba hio mianya kabla hatujauza kampuni zetu zote na kuzibinasfisha huenda tungebinafsisha serikali (seems like we have very little capability of managing things)
 
Unajiona mjuaji mwenye sheria na taratibu kichwani mwako, wakati hali halisi field iko tofauti.

Ukiona mtu anaandika jambo, ujue ameshachukua hizo sheria zenu na taratibu zenu, amejumlisha na yale yanayotokea field, ndio akapata majibu anayokuja nayo, kumsema Rais aliye dhaifu.

Mahaba yenu yaliyopitiliza yamewafunga upeo kifikra, mmekubali kudanganyika na "sheria na taratibu" ambazo hazifuatwi, au kufuatwa ni mpaka palemambo yawabane ndio watafutie hapo mlango wa kutokea.

Hilo bunge ulilolizungumzia kwenye mada yako ndio hili hapa chini, linaloagizwa na Rais badala lenyewe limuagize Rais?View attachment 2582866

Kwa mantiki hiyo niambie, kwanini Rais asilaumiwe pamoja na hizo "sheria na taratibu zako" unazoandika hapa?

Wengine tulishatoka nje ya box wakati nyie bado mmejificha uvunguni.
Tatizo unajibu hoja uliyojiandalia mwenyewe kichwani mwako badala ya hoja iliyopo.

Soma tena, uchangie hoja iliyopo.
 
Even a lay man anajua kwamba hii nchi inatafunwa na sasa hivi inatafunwa madudu yatakayopatika repoti ijayo..., issue sio tu kushughulikia watafunaji pindi wanaposhikwa wametafuna bali kuzuia mianya ya kutafuna..., sasa hata hio mianya kama ipo na bado inaendelea kuwepo means the system and the people involved are rotten, na kama hakuna wa kulaumu wala wa kuweza kuziba hio mianya kabla hatujauza kampuni zetu zote na kuzibinasfisha huenda tungebinafsisha serikali (seems like we have very little capability of managing things)
Kuongelea mianya iliyopo na hata mapungufu ya Serikali kiutendaji, wakati wote ni sahihi.

Lakini argument yangu ni spefic kwa report ya CAG.
 
Nimeona wengi kwa mihemuko ya umbumbumbu wa kutojua taratibu na sheria zilizopo wamekuwa wakimlaumu Rais kwa kutochukua hatua mara moja dhidi ya waliotajwa kwenye Report ya CAG.

Watu hao walitarajia baada tu ya report ya CAG, kesho yake Rais afukuze wale wote ambao ofisi zao zimehusishwa ama na upotevu, matumizi mabaya, matumizi hewa au matumizi yasiyofuata taratibu.

Watu hawa wasichojua ni kwa kwamba kufuatana na taratibu zilizopo za kikatiba na sheria, hawa maofisa ambao ofisi zao zimetajwa na ofisi ya CAG ni lazima waitwe na kuhojiwa na kamati ya Bunge. Ukiwafukuza mapema kwa taarifa tu ya CAG bila ya wao kupewa nafasi au ya kujitetea au kutoa ufafanuzi, hiyo kamati ya Bunge itamhoji nani? Kumbuka kamati ya Bunge uwezo wake wa kikatiba kuhusiana na report ya CAG, unaishia kwa wale ambao ni watendaji wa Serikali, na siyo mwananchi ambaye yupo mtaani.

Mambo yale ya overinvoicing, hayapo kwenye report ya CAG. Yale yanaweza kufanyiwa kazi na Rais kwa taratibu zilizopo, lakini Rais hawezi kuanza kuchukua hatua mara moja kwa ofisi zilizotajwa na CAG. Ikumbukwe kwenye report ya CAG, kuna upotevu, matumizi mabaya, ubadhirifu, kutofuata taratibu, matumizi hewa, n.k. Na hayo yanahusishwa na ofisi, report haitaji mtu specific.

Nadhani baada ya Bunge, kitakachofuatia, ni kuwatambua wahusika wa moja kwa moja. Na hao wahusika itabidi makosa yao yatambulike bayana. Kama ni uzembe, uwezo mdogo au kutojali, huyo kama mimi nikiwa ndiyo ofisi ya uteuze au mwajiri, nafukuza mara moja. Kama ni wizi, huyo ni kumkabidhi kwa Polisi ili afikishwe mahakamani. Kama ni kutokana na maumuzi yenye uwezekano wa msukumo wa rushwa (kwa mfano utoaji wa tenda zenye gharama kubwa kuliko uhalisia wa gharama), huyu kabidhi kwa TAKUKURU, achunguzwe halafu afikishwe mahakamani.

Japo ni dhahiri tuna Bunge ambalo siyo la wananchi, ni la watu waliopachikwa na mtu mmoja kutoka chama kimoja kwa mapenzi yake, hatuna namna, yatubidi tusubiri.

Hatutegemei makubwa toka Bungeni maana hata hao wabunge wenyewe ni zao la uovu, na wengi wao upeo wao ni mdogo, uadilifu wao ni wa mashaka makubwa, labda pengine mmoja mmoja atajitutumua na kuitafuta hekima. Ingawa mara nyingi mtu akiwa mwovu, kama walivyo hawa wabunge wengi ambao ni watoa rushwa, wevi wa kura, n.k., dhamira inakosa ujasiri dhidi ya waovu wenzao. Ni nadra sana jambazi akachukua jiwe kumpiga jambazi mwingine, japo kuna wakati anaweza kujitutumua ili kujikosha mbele ya watu wema ili naye aonekane ni mtu mwema.

Tusubiri, hatua zote zipite ili tupate uhalali wa kumlaumu Rais, kama amechukua hatua au hapana.
Ukaguzi unafanywa kwa sampling sijui kiswahili chake yawezekana Mkaguzi katika kufanya hivo hakuona baadhi ya nyaraka na hivyo sasa ni jukumu la Afisa Masuhuli kuhakikisha nyaraka zote zilizotajwa kwenye report zinawekwa wazi ili zihakikiwe. Katika hatua hii huwezi kumhukumu mtu yeyote mpaka muda uliotolewa wa kujibu hoja za mkaguzi uishe.
 
Nimeona wengi kwa mihemuko ya umbumbumbu wa kutojua taratibu na sheria zilizopo wamekuwa wakimlaumu Rais kwa kutochukua hatua mara moja dhidi ya waliotajwa kwenye Report ya CAG.

Watu hao walitarajia baada tu ya report ya CAG, kesho yake Rais afukuze wale wote ambao ofisi zao zimehusishwa ama na upotevu, matumizi mabaya, matumizi hewa au matumizi yasiyofuata taratibu.

Watu hawa wasichojua ni kwa kwamba kufuatana na taratibu zilizopo za kikatiba na sheria, hawa maofisa ambao ofisi zao zimetajwa na ofisi ya CAG ni lazima waitwe na kuhojiwa na kamati ya Bunge. Ukiwafukuza mapema kwa taarifa tu ya CAG bila ya wao kupewa nafasi au ya kujitetea au kutoa ufafanuzi, hiyo kamati ya Bunge itamhoji nani? Kumbuka kamati ya Bunge uwezo wake wa kikatiba kuhusiana na report ya CAG, unaishia kwa wale ambao ni watendaji wa Serikali, na siyo mwananchi ambaye yupo mtaani.

Mambo yale ya overinvoicing, hayapo kwenye report ya CAG. Yale yanaweza kufanyiwa kazi na Rais kwa taratibu zilizopo, lakini Rais hawezi kuanza kuchukua hatua mara moja kwa ofisi zilizotajwa na CAG. Ikumbukwe kwenye report ya CAG, kuna upotevu, matumizi mabaya, ubadhirifu, kutofuata taratibu, matumizi hewa, n.k. Na hayo yanahusishwa na ofisi, report haitaji mtu specific.

Nadhani baada ya Bunge, kitakachofuatia, ni kuwatambua wahusika wa moja kwa moja. Na hao wahusika itabidi makosa yao yatambulike bayana. Kama ni uzembe, uwezo mdogo au kutojali, huyo kama mimi nikiwa ndiyo ofisi ya uteuze au mwajiri, nafukuza mara moja. Kama ni wizi, huyo ni kumkabidhi kwa Polisi ili afikishwe mahakamani. Kama ni kutokana na maumuzi yenye uwezekano wa msukumo wa rushwa (kwa mfano utoaji wa tenda zenye gharama kubwa kuliko uhalisia wa gharama), huyu kabidhi kwa TAKUKURU, achunguzwe halafu afikishwe mahakamani.

Japo ni dhahiri tuna Bunge ambalo siyo la wananchi, ni la watu waliopachikwa na mtu mmoja kutoka chama kimoja kwa mapenzi yake, hatuna namna, yatubidi tusubiri.

Hatutegemei makubwa toka Bungeni maana hata hao wabunge wenyewe ni zao la uovu, na wengi wao upeo wao ni mdogo, uadilifu wao ni wa mashaka makubwa, labda pengine mmoja mmoja atajitutumua na kuitafuta hekima. Ingawa mara nyingi mtu akiwa mwovu, kama walivyo hawa wabunge wengi ambao ni watoa rushwa, wevi wa kura, n.k., dhamira inakosa ujasiri dhidi ya waovu wenzao. Ni nadra sana jambazi akachukua jiwe kumpiga jambazi mwingine, japo kuna wakati anaweza kujitutumua ili kujikosha mbele ya watu wema ili naye aonekane ni mtu mwema.

Tusubiri, hatua zote zipite ili tupate uhalali wa kumlaumu Rais, kama amechukua hatua au hapana.
Sikubaliani na wewe kwa sababu CAG anapogundua makosa ya kifedha na utendaji hujadiliana na wahusika kupata majibu. Ni wakati ambao wahusika wanapaswa kuwajibika kwa kuchukua hatua pasipo kusubiri mamlaka za uteuzi wao, au maamuzi ya Bunge. Kutokuchukua hatua ni tabia ya hovyo iliyojengeka kiasi kwamba makosa hayo hayo hujirudia kila ripoti ya CAG
 
Unajiona mjuaji mwenye sheria na taratibu kichwani mwako, wakati hali halisi field iko tofauti.

Ukiona mtu anaandika jambo, ujue ameshachukua hizo sheria zenu na taratibu zenu, amejumlisha na yale yanayotokea field, ndio akapata majibu anayokuja nayo, kumlaumu Rais aliye dhaifu.

Mahaba yenu yaliyopitiliza yamewafunga upeo kifikra, mmekubali kudanganyika na "sheria na taratibu" ambazo hazifuatwi, au kufuatwa ni mpaka pale mambo yawabane ndio watafutie hapo mlango wa kutokea.

Hilo bunge ulilolizungumzia kwenye mada yako ndio hili hapa chini, linaloagizwa na Rais badala lenyewe limuagize Rais?View attachment 2582866

Kwa mantiki hiyo niambie, kwanini Rais asilaumiwe pamoja na hizo "sheria na taratibu" zako unazoandika hapa?

Wengine tulishatoka nje ya box wakati nyie bado mmejificha uvunguni, ukishapata jibu hapo tell us, nani mbumbumbu wa kweli kati yetu?
Huyo ni mmoja wa CHAWA
 
Kuna awamu yoyote ndani nchi yetu, report ya CAG ili fanyiwa kazi na wahusika kufikishwa mahakamani?
Sina kumbukumbu sahihi kama Mahalu alifikishwa mahakamani kutokana na report ya CAG au ni kutokana na uchunguzi wa ndani ya Serikali yenyewe.

Hata suala la Lowasa kujiuzulu, zaidi ilikuwa ni hekima yake lakini Bunge halikuazimia kuwa ajiuzulu, lilisema ajitafakari. Akajitafakari akaamua kujiuzulu.

Lakini hekima hiyo wengine wote hawana. Wengine mpaka wameambiwa wapishe (siyo wajitafakari kama alivyoambuwa Lowasa na Bunge), lakini hata kupisha wamegoma.
 
Huyo ni mmoja wa CHAWA
Ukiwa chawa, fikira zako zinakuwa zimeishia hapo. Ukiamini kuwa kila mtu ni wa namna ambayo wewe upo.

Wewe endelea kuwa chawa, lakini tupo tuliozaliwa tukiwa na mawazo huru, tunaishi katika mawazo huru, na tutayamaliza maisha yetu katika uhuru.
 
Tatizo unajibu hoja uliyojiandalia mwenyewe kichwani mwako badala ya hoja iliyopo.

Soma tena, uchangie hoja iliyopo.
Tena naona bora unishukuru nimekuongezea nyama kwenye thread yako iliyojaa matundu ya kila aina.

Paragraph yako ya tano umelizungumzia bunge, tena kuonesha huna hakika na kile unachoandika umetumia neno "nadhani" [ usije kulifuta], baada ya hapo umeonesha kile kinachotakiwa kufuatwa baada ya ripoti kujadiliwa bungeni, tena ukajitolea mfano mwenyewe kwa kusema ungewafukuza...

Sasa niambie, nilichoandika mimi mwanzo nilikosea wapi? hilo bunge lina uwezo wa kumuagiza Rais kipi afanye? bahati nzuri nawe umekiri ni dhaifu la chama kimoja, na ndio maana nikakuwekea kipande cha gazeti kuthibitisha haliwezi kumuagiza Rais.

Moreover, umewazungumzia wahusika wale ambao wataitwa na bunge kuhojiwa, vipi kwa wale ambao hawataitwa lakini uzembe umefanyika ofisini kwao wakiwa ndio mabosi wa hizo ofisi? hawa unataka washughulikiwe na nani?

Ajabu unasema nimejibu hoja niliyojiandalia!.
 
Ni kweli mara nyingi huyu John hajui anachokishabikia.
Kama ni dhaifu Mbowe anayelambishwa Asali ni nani?

Mbowe hajalamba sali, mtu mwelewa kama wewe ukisema hivyo ndiyo maana nakutania kuwa pumbavu wewe. . Alitoka mtu katili magufuli, akaja mwingne Samia akasema njoo tuzungumze, tatizo liko wapi? nambie Mbowe ame compromise demand ipi walizokuwa wanazipigania?
 
Kuongelea mianya iliyopo na hata mapungufu ya Serikali kiutendaji, wakati wote ni sahihi.

Lakini argument yangu ni spefic kwa report ya CAG.
Tutaongea mpaka maneno ya kusema yaishe lakini kama jitihada za kuziba mianya mpaka sasa hazipo kinachoendelea ni maigizo na at best kubadilisha waigizaji at worse waigizaji wanaendelea na plot ni ile ile - sometimes plot inazaa plot inayoongeza gharama; Usishangae Tume za Kuchunguza Tume za Kuchunguza Tume zikatengenezwa

Wanaolalamika huenda wamechoka kuuza mbuzi kwa ajili ya kukomboa kuku..., In short accountability pekee uozo ukitokea in your watch hata kama haukuiba ni kwamba haukuwajibika ipasavyo kuzuia huo wizi; ungeweza kupisha na kukaa kando wakati uchunguzi unaendelea - Unless CAG anasema kitu kimepotea wakati hakijapotea and if that is the case atakuwa hajafanya kazi yake vema....
 
Back
Top Bottom