Watanzania wengi ni wachafu

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,826
9,533
Ukweli utafiti nilioufanya kwenye mazingira kadha wa kadha yanayohitaji usafi nimebaini wananchi wengi hapa Tanzania ni wachafu. Hii hasty generalization ni bila kujali ni wasomi au wananchi wa kawaida.

Mfano nimepita kwenye vyoo vya umma, vile vya kulipia, vyoo katika taasisi za elimu ya juu vikiwemo vyuo vikuu vikongwe hapa nchini kwa kweli mazingira ya vyoo ni machafu sana. Utakutana na mikojo au kinyesi pembeni ya tundu au mtu katumia maliwato hajapaswafi. Aidha, nimeenda uwanja wa Taifa Mara kadhaa vyoo ni vichafu mno.

Hata makazini, wakati fulani niliajiriwa Serikalini kwenye ofisi moja yenye reputation kubwa kabisa lakini ile floor ya idara niliyokuwemo haikuwa ajabu kufika toilet kukuta mtu kany'a au kak'ojoa kaacha haja zake hapo, au katumia toilet papers kazichambua kaziacha hapo au kazilowanisha na maji.

Eneo jingine linalothibitisha kwamba wanajamii wetu ni wachafu, ni unaposafiri kwenda mikoani. Barabarani utakutana na taka za chupa tupu, au masalia ya vifungashio vya vyakula vya haraka almaaruf 'take away'.

Eneo jingine linalothibitisha kwamba sisi ni WACHAFU ni namna tunavyoachia 'gereji bubu' kufanya shughuli zao bila mpangilio, kiasi kwamba wanalundika taka mitaani. Mfano ni hapa Dar es salaam kule Tandale, Mwenge jirani na Mwenge Dispensary, Tandika nk pia, Soweto Mbeya miongoni mwa maeneo mengine.

Eneo ambalo wananchi wanajitahidi kwa usafi ni miili yao. Kusema kweli wananchi wengi ni wasafi kwenye miili yao. Ni watu nadhifu na walimbwende haswa. Ukikutana nao kwenye usafiri wa umma ni nadra kukutana na mtu ananuka kikwapa, au kavalia shabishabi. Sasa najiuliza kwanini kwenye mazingira tunakuwa wachafu hivi!? Tatizo liko wapi?

Ukienda nchi kama Rwanda ndio utagundua kwamba sisi ni wachafu sana.

MY TAKE:
Wabunge pitisheni sheria kali ya ulinzi wa mazingira na usafi. Iwe kosa kubwa mtu kuwa na mazingira machafu. Hapa zisiachiwe local governments. Usafi wa mazingira utasaidia sana kupunguza bajeti za afya. Japo mimi sio mtabibu lakini Nina hakika maradhi mengi yanayopeleka watu wetu Hospitali yanahusiana na uchafu. TUBADILIKE.
 
38deca19-31e0-441f-b114-baa02078fd4a.jpg

Na kweli watanzania wachafu
 
1. Wenye ngozi nyeupe na maji ya kunde (Wabongo) ni wachafu kuliko wenye ngozi nyeusi
2. Wembamba wana hali ya usafi muda mwingi kuliko wanene. Wanene wengi wao wanatumia manukato kuficha uchafu.
3. Wanawake wanachafua zaidi (chooni) kuliko wanaume. Kuna kesi nyingi vyoo vya maofisini aki na dada wanatamani kutumia vyoo na wanaume kuliko kutumia na wanawake wenzao.
 
Napingana na wewe Kwa 100% .ila Mimi naona hasa Kwa upande wa kinywa ( mdomo), Hali ni mbaya Sana jamani watu wananuka midomo hatari !! Mtu kaoga kapendeza ila daa! Mdomo una harufu Kali na mbaya!?
Sori name naungana sio kupingana
 
1. Wenye ngozi nyeupe na maji ya kunde (Wabongo) ni wachafu kuliko wenye ngozi nyeusi
2. Wembamba wana hali ya usafi muda mwingi kuliko wanene. Wanene wengi wao wanatumia manukato kuficha uchafu.
3. Wanawake wanachafua zaidi (chooni) kuliko wanaume. Kuna kesi nyingi vyoo vya maofisini aki na dada wanatamani kutumia vyoo na wanaume kuliko kutumia na wanawake wenzao.
Hii namba tatu imeondoa dhana niliyokuwa nayo. Awali nilidhani uchafu wa vyoo ni zaidi kwa wanaume kumbe haya -ke ni tatizo!?
 
Napingana na wewe Kwa 100% .ila Mimi naona hasa Kwa upande wa kinywa ( mdomo), Hali ni mbaya Sana jamani watu wananuka midomo hatari !! Mtu kaoga kapendeza ila daa! Mdomo una harufu Kali na mbaya!?
Kwamba hauoni taka za magari mabovu?. Huoni vyoo vya uwanja wa Taifa vilivyo vichafu!?. Hauoni jinsi vyoo vya UDSM vya wanafunzi vilivyo vichafu!? Huoni?.

Kama unahitaji haja kubwa na upo katikati ya mji ni hatari sana. Si ajabu magonjwa na mfumo wa mkojo UTI & the like yameshamiri sana siku hizi. Sababu ni moja tu. Uchafu.
 
1. Wenye ngozi nyeupe na maji ya kunde (Wabongo) ni wachafu kuliko wenye ngozi nyeusi
2. Wembamba wana hali ya usafi muda mwingi kuliko wanene. Wanene wengi wao wanatumia manukato kuficha uchafu.
3. Wanawake wanachafua zaidi (chooni) kuliko wanaume. Kuna kesi nyingi vyoo vya maofisini aki na dada wanatamani kutumia vyoo na wanaume kuliko kutumia na wanawake wenzao.
Kuna jamaa alisema watu wengi hasa wa Dar wanaoga bila dodoki, kwa hiyo hawaogi ipasavyo japo sikukubaliana nae, kwenye daladala hapa Dar watu ni wasafi. Ila mazingira wanakotokea ni kuchafu kinoma.
 
Ukienda Rwanda public toilets ziko vizuuri. Hapa Bongo sasaa dah, aibu.
 
Ukweli utafiti nilioufanya kwenye mazingira kadha wa kadha yanayohitaji usafi nimebaini wananchi wengi hapa Tanzania ni wachafu. Hii hasty generalization ni bila kujali ni wasomi au wananchi wa kawaida.

Mfano nimepita kwenye vyoo vya umma, vile vya kulipia, vyoo katika taasisi za elimu ya juu vikiwemo vyuo vikuu vikongwe hapa nchini kwa kweli mazingira ya vyoo ni machafu sana. Utakutana na mikojo au kinyesi pembeni ya tundu au mtu katumia maliwato hajapaswafi. Aidha, nimeenda uwanja wa Taifa Mara kadhaa vyoo ni vichafu mno.

Hata makazini, wakati fulani niliajiriwa Serikalini kwenye ofisi moja yenye reputation kubwa kabisa lakini ile floor ya idara niliyokuwemo haikuwa ajabu kufika toilet kukuta mtu kany'a au kak'ojoa kaacha haja zake hapo, au katumia toilet papers kazichambua kaziacha hapo au kazilowanisha na maji.

Eneo jingine linalothibitisha kwamba wanajamii wetu ni wachafu, ni unaposafiri kwenda mikoani. Barabarani utakutana na taka za chupa tupu, au masalia ya vifungashio vya vyakula vya haraka almaaruf 'take away'.

Eneo jingine linalothibitisha kwamba sisi ni WACHAFU ni namna tunavyoachia 'gereji bubu' kufanya shughuli zao bila mpangilio, kiasi kwamba wanalundika taka mitaani. Mfano ni hapa Dar es salaam kule Tandale, Mwenge jirani na Mwenge Dispensary, Tandika nk pia, Soweto Mbeya miongoni mwa maeneo mengine.

Eneo ambalo wananchi wanajitahidi kwa usafi ni miili yao. Kusema kweli wananchi wengi ni wasafi kwenye miili yao. Ni watu nadhifu na walimbwende haswa. Ukikutana nao kwenye usafiri wa umma ni nadra kukutana na mtu ananuka kikwapa, au kavalia shabishabi. Sasa najiuliza kwanini kwenye mazingira tunakuwa wachafu hivi!? Tatizo liko wapi?

Ukienda nchi kama Rwanda ndio utagundua kwamba sisi ni wachafu sana.

MY TAKE:
Wabunge pitisheni sheria kali ya ulinzi wa mazingira na usafi. Iwe kosa kubwa mtu kuwa na mazingira machafu. Hapa zisiachiwe local governments. Usafi wa mazingira utasaidia sana kupunguza bajeti za afya. Japo mimi sio mtabibu lakini Nina hakika maradhi mengi yanayopeleka watu wetu Hospitali yanahusiana na uchafu. TUBADILIKE.
Naunga mkono hoja, wabongo walio wengi hawajuwi maana ya usafi hata kidogo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom