Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Nashangaa sana kusikia huyu mgombea urais kupitia CHADEMA maneno ya kejeli na dharau kwa taifa lake anayavyoyatoa hadharani dhidi ya Watanzania.
Hajui au hatambui kuwa anatudhalilisha na kututukana hata kampeni hazijaanza?
Mtu na akili zako timamu unaongea na waandishi wa habari unaweza kudiriki kusema taifa lako linapewa chakula na mabeberu.
Yaani bila aibu unasema Tanzania inalishwa na mabeberu! Na wakati huo unategemea watanzania wenye akili timamu wakupigie kura? Kisa hao mabeberu unaowasifia walikupa chakula na hifadhi kwa miaka mitatu pale uliposhambuliwa na wahalifu wasiofahamika?
Je, ulipozunguka kutafuta wadhamini hukuona chakula ambacho watanzania wanazalisha na kujilisha kwa mikono yao? Hukuona mipunga ilivyojazana huko Kagongwa, Kahama? Hukuona Mipunga ilivyojazana huko Igunga?
Wewe mgombea wa CHADEMA ambaye unataka uwe Rais wa JMT hujui kuwa mahindi ya Tanzania yanalisha nchi za jirani kama Kenya, Uganda, South Sudan n.k? Kama hujui hili alafu unatudhalilisha kuwa tunalishwa na mabeberu unadhani nani atakupa kura? Au una mpango gani na mabeberu kutupa chakula wakati tunajilisha wenyewe?
Pia nimesikia unalalama kuwa una kesi za kipuuzi na kijinga ambazo eti serikali ya CCM imekubambikia. Kama ni kesi za kipuuzi na kijinga nenda kazimalize mahakamani acha kubwabwaja mitaani.
Hajui au hatambui kuwa anatudhalilisha na kututukana hata kampeni hazijaanza?
Mtu na akili zako timamu unaongea na waandishi wa habari unaweza kudiriki kusema taifa lako linapewa chakula na mabeberu.
Yaani bila aibu unasema Tanzania inalishwa na mabeberu! Na wakati huo unategemea watanzania wenye akili timamu wakupigie kura? Kisa hao mabeberu unaowasifia walikupa chakula na hifadhi kwa miaka mitatu pale uliposhambuliwa na wahalifu wasiofahamika?
Je, ulipozunguka kutafuta wadhamini hukuona chakula ambacho watanzania wanazalisha na kujilisha kwa mikono yao? Hukuona mipunga ilivyojazana huko Kagongwa, Kahama? Hukuona Mipunga ilivyojazana huko Igunga?
Wewe mgombea wa CHADEMA ambaye unataka uwe Rais wa JMT hujui kuwa mahindi ya Tanzania yanalisha nchi za jirani kama Kenya, Uganda, South Sudan n.k? Kama hujui hili alafu unatudhalilisha kuwa tunalishwa na mabeberu unadhani nani atakupa kura? Au una mpango gani na mabeberu kutupa chakula wakati tunajilisha wenyewe?
Pia nimesikia unalalama kuwa una kesi za kipuuzi na kijinga ambazo eti serikali ya CCM imekubambikia. Kama ni kesi za kipuuzi na kijinga nenda kazimalize mahakamani acha kubwabwaja mitaani.