Spika Dkt. Tulia yuko sahihi sana, CHADEMA wajifunze kufanya vitu kwa usahihi na wafanye kiusahihi

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,428
113,433
Wanabodi,

Leo tena nimepata fursa kuwaletea zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" na issue iliyo mezani ni Sakata la wabunge 19 wa Chadema, Chadema imewatimua ikijua it's done with them, Spika wa Bunge amewakingia kifua, hivyo wanaendelea na ubunge wao kusubiria aumuzi wa mahakama.

Humu JF, tuko wanachama wa aina nyingi, ila pia sisi wanachama wa JF, kuna baadhi yao ambao wana command much respect humu jukwaani, hivyo bandiko hili ni kuwajibu baadhi yao.

Siku zote Chadema imekuwa ikiendesha baadhi ya mambo yake kienyeji enyeji bila kufuata Katiba sheria taratibu na kanuni na haswa timua timua zake, japo Chadema ina katiba, na hiyo katiba imeweka miongozo yote ya kushughulikia nidhamu, kwa lengo la kutenda haki, lakini hakuna hata timua timua moja ambayo Chadema wamefuata katiba yake. Timua timua zote ni kinyume cha katiba yake, and always they have been doing that and go away.

This time around, kwenye hili la kina
Halima Mdee, Chadema imekwaa kisiki, tena kisiki cha mpingo, ukijikwaa kwenye kisiki cha mpingo, lazima utaumia wewe, hivyo hili ni Bandiko la kuwahimiza rafiki zangu wana Chadema, kwa Chadema as chama as well as individually, they should always seek the truth & the truth will set them free. Uamuzi wa Spika wa Bunge, Dr. Tulia Akson kuwakingia kifua, wabunge waliowatimua kikangaroo ni uamuzi sahihi, yaani uamuzi very right, done at the right time and done right.

Ushauri wangu kwa Chadema ni from now, Chadema must learn, the hard way, not only how to do the right things, but also do them right!.

Mimi hili suala hata silielewi. Hivi kwa nini Spika hakuwaita wakina Halima na NEC ili watoe uthibitisho kuwa barua waliyompa ni halali? Maana kama kweli walimpa barua basi Spika ndio injured party na ni yeye ndie aliyepaswa kuchukua hatua dhidi ya waliomdanganya kwa kumpa nyaraka za kughushi. Ukimya wake kwenye suala hii ndio unanitia wasiwasi kuwa hamna nyaraka iliyowasilishwa kuwatambulisha wakina Halima kuwa wateuliwa wa Chadema. Hii ndio inayonifanya nione tuhuma za kughushi hazina mashiko. Labda sasa Chadema watumie Mahakama kumlazimisha NEC atoe nakala za barua alizopokea kutoka Chadema.

Amandla...
Mkuu Fundi Mchundo , vitu vingine sio vya kuuliza ni kutaka tuu kumuonea Spika.
Uchaguzi unasimamiwa na NEC, Wabunge wote wanapewa barua ya utambulisho ya NEC ndio wanatinga Bungeni. Sii kazi ya Bunge au Spika kuhoji wamepatikanaje, as long as Barua ya utambulisho ya NEC imemfikia then ni authentic letter, Bunge halina sababu yoyote kuhoji utambulisho wa NEC.

Humu JF wengi wana mahaba na Chadema hivyo they are just too blind to see jinsi inavyofanya mambo ya hovyo. Hili jambo ni Chadema wenyewe wameli mishandled toka mwanzo.

Naomba niunganishe na hoja ya Mkuu Nguruvi3 nizijibu kwa pamoja kuwaonyesha makosa ya Chadema ya kijinga kabisa.

Mkuu P , kuna hoja moja tusaidie kuielewa ili tusimuonee Spika.

Spika Tulia kasema asubuhi ya jana, 'kuna shauri lipo mahakamani hatawazuia COVID19 bungeni''
Jioni Jaji Mgeta anatoa kauli ya mahakama ya 'status quo' kwa Wabunge

Swali, Spika alipata wapi taarifa za COVID19 kwenda mahakamani?
Kuna sheria gani inayomkataza asiwazuie kuingia Bungeni kabla ya 'hukumu' ya mahakama?
Swali la mwisho, je, Tundu Lissu ambaye shauri lake lipo mahakamani ni Mbunge halali?

JokaKuu Fundi Mchundo
Kwa faida ya wengine naomba nianzie mbali.
  1. Hili jambo limeanzishwa na Chadema kususia kutambua matokeo ya uchaguzi mkuu uliopita, ikasema hailitambui Bunge na haitambui Rais
  2. NEC ikatoa nafasi 19 za viti maalum, Chadema wakasema hawateua na hawana time.
  3. Mdee of course, accompanied by Bulaya, wakam consult a very high ranking Kigogo wa Chadema on the benefits of hizo nafasi 19, Kigogo huyo not only gave them a go ahead, but also facilitated them!.
  4. Introduction credentials from Chadema (a bone of contention) introduced the 19 to NEC.
  5. NEC wakawapa barua za uteuzi, authentic bonafide genuine certificates wakaziwasilisha Bungeni, hivyo Kibunge, hawa ni Wabunge halali kabisa!.
  6. Spika/Bunge has nothing to do with the process iliyotumika kumpata mbunge yoyote, as long as ameteuliwa na NEC.
  7. Kukitokea mgogoro wowote wa Uchaguzi, kwa mtu yoyote kupinga ushindi wa mgombea mahakamani, huyo Mbunge ataendelea kuwa mbunge mpaka mahakama itakapotoa hukumu.
  8. Na kukitokea mgogoro wa kichama, mbunge yoyote kufutwa uanachama na chama chake, anapaswa kupoteza ubunge wake automatically ila akiliarifu Bunge kuwa amepinga mahakamani kuvuliwa kwake uanachama, Bunge litamkingia kifua kusubiria aumuzi wa mahakama.
  9. Hivi ndivyo ilivyofanyika kwa Hamad Rashid Mohammed, David Kafulila na Zitto Kabwe. Na baada ya uamuzi wa mahakama, walivuliwa ubunge, Zitto alijivua na kuaga rasmi Bunge.
  10. Hivyo jana asubuhi kupitia Bunge live, Spika alizungumza huku nikimuona kwa macho yangu na kumsikia kwa masikio yangu, alitangulia kupokea taarifa ya kina Mdee kufungua kesi mahakamani kupinga kuvuliwa uanachama, kwa kutaja siku, saa na dakika, kabla ya kupokea taarifa rasmi ya Chadema kuwafuta uanachama. Hivyo Spika Tulia yuko right na Bunge liko right kuwakingia kifua.
  11. Haya sasa ninayoendelea nayo ni yangu. Watu wengi humu wana mahaba niue na Chadema, na siku zote mapenzi yakizidi huleta upofu hivyo hamuoni makosa ya Chadema.
  12. Baada tuu ya Wabunge hao kuapishwa na Chadema kuwakana, sisi washauri wa bure tukawashauri Chadema wafanye a due process wameingiaje Bungeni, barua ya utambulisho toka Chadema imeandikwa na kusainiwa na nani?.
  13. Hii due process ingebainisha kuna forgery, forgery ni jinai, walipaswa kuripoti polisi ili uchunguzi wa kijinai ufanyike na hiyo barua yao ya utambulisho, iwe authenticated na ingebainika ni forgery, wala sio Bunge bali ni NEC ndio wangetengua zile barua zao za uteuzi na wangevuliwa ubunge.
  14. Chadema ina katiba yake katiba hiyo imeweka sheria taratibu na kanuni za nidhamu. CC ni mamlaka ya nidhamu ya wabunge, kwanini waliliendesha shauri la wabunge hao Kikangroo bila kufuata taratibu na kanuni zao. Kwanini CC ya Chadema wawatimue wabunge hao bila kufanyika kwanza kwa a due process?!
  15. CC ya Chadema sio mamlaka ya nidhamu ya Mwenyekiti wa Bawacha, Halima Mdee, mwisho wa mamlaka ya CC ya Chadema kwa Mwenyekiti wa Bawacha ni kumsimamisha tuu, lakini mamlaka yake ya nidhamu ni Baraza Kuu, sasa hiyo CC ya Chadema, ilipata wapi mamlaka ya kumtiimua Halima Mdee?.
  16. Kikao cha Baraza Kuu kilipoitishwa kwanini hawakupeleka shauri la Mdee kwenye mamlaka yake sahihi ya nidhamu?.
  17. Baraza Kuu linapokaa kama mamlaka ya rufaa kwa wale wabunge 18, ukimuondoa Halima Mdee, kabla ya kupiga kura kuridhia maamuzi ya CC, walipaswa kujiridhisha kuwa taratibu zilifuatwa.
  18. Kile kikao cha CC ya Chadema mimi nimekiita CC ya Chadema imekaa kama a Kangaroo Court, na ule uamuzi wa CC ya Chadema, mimi niliuita ni uamuzi wa Kikangroo, kitendo cha Baraza Kuu kuyabariki maamuzi batili ya Kikangroo bila kufanyika kwanza kwa a due process, kumepelekea Baraza Kuu Chadema kufanya Ukangaroo as well.
  19. A way forward ni Mahakama ambayo ni a proper court itayapindua maamuzi ya Kikangroo ya CC ya Chadema yaliyobarikiwa na Baraza Kuu na kuamuru a due process ifanyike.
  20. Wito wangu kwa wapenzi wa Chadema, seek the truth and the truth will set you free. Iambieni Chadema ukweli, ndio mtaijenga Chadema kuwa ni chama mbadala kuireplace CCM. Kwa haya madudu na maroroso kama haya, Ikulu yetu wangeweza?.
Paskali
 
Magufuli hakukosea kukuita njaa maana njaa imekuharibu mpaka umekuwa mtu wa hovyo kabisa, Lissu alipinga kufukuzwa mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama na wabunge wa CUF walipinga mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama? umekuwa mtu wa hovyo sn unapewa rushwa unauza utu wako. Kwahiyo wewe unaijua katiba ya CHADEMA kuliko CHADEMA wenyewe? shame on you
 
Kuna mambo ambayo leo hii watu hawaelewi mtu X mwenye uthibitisho wote alini PM tena bado yuko CDM kuwa mwenye kujua Suala hili kote ni Mbowe ndo maana akawa anahangaika sana akina Mdee wajiondoe wenyewe kabla ya kamati kuu kulinda heshima yake!

Kwa logic tu Kwanini anamtuma mtu mpaka amfuate Nairobi kwamba jitoe, baada ya kugundua kwamba mambo yamekuwa mazito akaona credibility yake inaendelea kushuka!

Mbowe anasema ya Kwenda Nairobi na Gerezani tu, Mbona ya hotelini hajayasema?

Mbona wakati wa msiba wa familia Kwa mbowe Matiko, Mdee Na Bulaya walikaa masaa mawili wakimwambia Heche awape Nafasi kidogo hayasemwi? Kama lilikuwa Suala la afya Kwanini Heche aondolewe!

Mbona hawasemi kwamba Mbowe katembelewa kila Jumapili kule Gerezani ? Na maongezi yamekuwa jinsi ya kuongelea haya?

Emanuel Mugaya ananielewa Kwa nayo andika hapa!

Mdee inaonekana ana heshima sana Kwa mbowe tena sana Mbona mazungumzo ya kabla ya Mkutano mkuu Mbowe hayagusii?

Mchezo mchezo wenye uhuni

Wanadanganyana tu na wadanganyane wao kila siku itakuwa Chadema ndo ya Mahakamani wakati Vyama vinginevyo vinajijenga!!!

Chama kina ka Uhuni fulani kwenye maamuzi ni maigizo

Unaweza fika hatua ukaona bora ubaki bila Chama Au ujishkize CCM tu

Britanicca
 
Du Paschal tena,

Swali rahisi sana, wakati Halima na wenzake wameenda bungeni juzi walikua ni wa chama gani mpaka speaker atoe maamuzi ya kuwalinda?

Kwa upande mmoja chama kimewafukuza na kutoa taarifa bungeni. Bunge ilipaswa kufuata sheria ....mbunge lazima atokane na chama.

Upande wa pili waathirika walisema nao wamepata taarifa za kufukuzwa kwao ila wana nia ya kwenda mahakani. Hivyo hawakuwa na amri ya mahakama inayomzuia speaker kuwafukuza.

Je speaker alipata wapi mamlaka au sheria ipi kuwaacha bungeni kabla ya amri ya mahakama?

Je nani mwenye maamuzi ya hovyo?
Refer case ya Lema, wabunge wa CUF etc.

Paschal hujadeclare interest kwamba wewe ni CCM hivyo andiko lako liko biased na sababu zipo wazi na ndio maana utapingwa sana hapa. Pia una ajenda mbaya dhidi ya Chadema kwani kwa siku nne mfululizo umeandika mada moja umebadili jina la title. Hata kama ni spinning kuna njia ya kufanya na sio kwa njia unayotumia ipo wazi mno.

Uteuzi hauji kwa kuandika biased ideas bali kutumia critical thinking plus proffessionalism
 
Mtoa hoja hii ni Mr. Paschal au kuna mtu ametumia status yake? binafsi ni mfuasi sana wa hoja zake but this one it's one of the worst, mbona na wewe mkuu unafikiria kwa kutumia tumbo badala ya kichwa chenye ubongo?all political parties ni vya hiari!, kama hutakiwi jiondoe huwezi lazimisha, katiba ya CDM je inaruhusu kwa member to seek remedy in the courts of law?

Courts haziwezi kulazimisha uanachama kwa chama cha hiari, halafu cases zote za kibunge, bunge lilikua linatumia ubabe wake kufanya maamuzi, refer Mr.Lissu, Mrs . Simba etc etc, na yanayotokea hapa tunajionyesha ni jinsi gani tumo ndani ya shithole country, hii case ni ya kisiasa sio kikatiba na imegubikwa na uroho wa pesa, Mr. Mayala definitely u can do better than this, always Rudina kwenye uandishi wako wenye facts
 
Magufuli hakukosea kukuita njaa maana njaa imekuharibu mpaka umekuwa mtu wa hovyo kabisa, Lissu alipinga kufukuzwa mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama na wabunge wa CUF walipinga mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama? umekuwa mtu wa hovyo sn unapewa rushwa unauza utu wako. Kwahiyo wewe unaijua katiba ya CHADEMA kuliko CHADEMA wenyewe? shame on you
Tulikubaliana Ndugai hakufuata utaratibu. Spika wa sasa anafuata sheria, kanuni na utaratibu.

CHADEMA mjiepushe kupindisha sheria in your favour, hamtakuwa na utofauti na hao CCM mnaotuaminisha wabadhirifu.
 
CHADEMA kama haiwezi kufuata katiba yao wenyewe wataweza kweli kufuata katiba ya nchi wakiwa na madaraka?😁

Anyway; mimi binafsi nitakuwa mtu wa mwisho kuamini kuwa wabunge 19 walifoji barua ya chama kwa sababu kwa jinsi tinavyoinua CHADEMA kama kweli halima na wenzake walifoji barua ingekuwa tayari wameshawafungulia kesi tangu mwanzo.
 
Wanabodi
Leo tena nimepata fursa kuwaletea zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" na issue iliyo mezani ni Sakata la wabunge 19 wa Chadema, Chadema imewatimua ikijua it's done with them, Spika wa Bunge amewakingia kifua, hivyo wanaendelea na ubunge wao kusubiria aumuzi wa mahakama...
Mayalla zikijitokeza Issues za chadema huwa anawashwa mwili mzima.
 
Wanabodi
Leo tena nimepata fursa kuwaletea zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" na issue iliyo mezani ni Sakata la wabunge 19 wa Chadema, Chadema imewatimua ikijua it's done with them, Spika wa Bunge amewakingia kifua, hivyo wanaendelea na ubunge wao kusubiria aumuzi wa mahakama...
Hapa yote uliyoyasema ni sahihi ila yote haya aliinjinia yule alikuitaga Nzala hivyo kuhoji barua kaandika nani siyo sahihi swala liko wazi jinsi walivyoingia ila kwakuwa swala lipo mahakamani ni bora wakasubiri ila kimsingi vikao vyote kuanzia kamati kuu hadi baraza kuuu ni halali na vimefuata katiba ya CHADEMA na na ya Jamuhuri.
 
Swali rahisi sana, wakati Halima na wenzake wameenda bungeni juzi walikua ni wa chama gani mpaka speaker atoe maamuzi ya kuwalinda?
Wameenda kama Wanachadema.

Kwa upande mmoja chama kimewafukuza na kutoa taarifa bungeni. Bunge ilipaswa kufuata sheria ....mbunge lazima atokane na chama.
Hawakutenda haki katika kuwafukuza. Ni mahakama pekee ndio imepewa mamlaka Kikatiba ya kuamua uhalali au uharamu wa uanachama wao katika muktadha huu.

Upande wa pili waathirika walisema nao wamepata taarifa za kufukuzwa kwao ila wana nia ya kwenda mahakani. Hivyo hawakuwa na amri ya mahakama inayomzuia speaker kuwafukuza.

Je speaker alipata wapi mamlaka au sheria ipi kuwaacha bungeni kabla ya amri ya mahakama?
The moment walipoonesha nia ya kwenda mahakamani tayari walithibitisha kuhisi kutokutendewa haki na nia yao ya kupigania haki yao.

Katika muktadha huu, Spika anawajibika kuwalinda mpaka mahakama itakapoamua vinginevyo.

Punguzeni mahaba.
 
Kuna mambo ambayo leo hii watu hawaelewi mtu X mwenye uthibitisho wote alini PM tena bado yuko CDM kuwa mwenye kujua Suala hili kote ni mbowe ndo maana akawa anahangaika sana akina Mdee wajiondoe wenyewe kabla ya kamati kuu kulinda heshima yake!

Kwa logic tu Kwanini anamtuma mtu mpaka amfuate Nairobi kwamba jitoe, baada ya kugundua kwamba mambo yamekuwa mazito akaona credibility yake inaendelea kushuka!

Mbowe anasema ya Kwenda Nairobi na Gerezani tu , Mbona ya hotelini hajayasema?

Mbona wakati wa msiba wa familia Kwa mbowe Matiko , Mdee Na Bulaya walikaa masaa mawili wakimwambia Heche awape Nafasi kidogo hayasemwi? Kama lilikuwa Suala la afya Kwanini Heche aondolewe!

Mbona hawasemi kwamba Mbowe katembelewa kila Jumapili kule Gerezani ? Na maongezi yamekuwa jinsi ya kuongelea haya?

Emanuel Mugaya ananielewa Kwa nayo andika hapa!

Mdee inaonekana ana heshima sana Kwa mbowe tena sana Mbona mazungumzo ya kabla ya Mkutano mkuu mbowe hayagusii?

Mchezo mchezo wenye uhuni

Wanadanganyana tu na wadanganyane wao kila siku itakuwa Chadema ndo ya Mahakamani wakati Vyama vinginevyo vinajijenga!!!

Chama kina ka Uhuni fulani kwenye maamuzi ni maigizo


Unaweza fika hatua ukaona bora ubaki bila Chama Au ujishkize CCM tu


Britanicca
Mbona mnawasemea ,kwanini wao wasiseme nani aliyepeleka bungeni?
 
Magufuli hakukosea kukuita njaa maana njaa imekuharibu mpaka umekuwa mtu wa hovyo kabisa, Lissu alipinga kufukuzwa mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama na wabunge wa CUF walipinga mahakamani kwanini Ndugai hakusubiri uamzi wa mahakama? umekuwa mtu wa hovyo sn unapewa rushwa unauza utu wako. Kwahiyo wewe unaijua katiba ya CHADEMA kuliko CHADEMA wenyewe? shame on you
Kwanza inabidi tujue,aliyefoji barua kutoka Chadema kwenda NEC ni. Nani?,hili swali Chadema Bado hamjajibu.
 
Back
Top Bottom